Machapisho

TANZANIA KUONGEZA NGUVU KUTOKOMEZA SOTOKA YA MBUZI NA KONDOO

Picha
Tanzania imeendelea kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Sotoka ya Mbuzi na Kondoo (Peste des Petits Ruminants - PPR) kwa kutengeneza Mpango Mkakati wa hadi mwaka 2030, na kuimarisha ushirikiano wa kikanda na nchi jirani katika kudhibiti na hatimaye kutokomeza ugonjwa huo unaoathiri mifugo na maisha ya wafugaji, hatua itakayoiweka Tanzania katika mstari wa mbele barani Afrika katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo unaodhuru mifugo. Akizungumza wakati wa kuhitimisha Mkutano wa Kikanda wa PPR uliofanyika leo Septemba 16, 2026 Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Mikutano wa White Sands Resort, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, amesema Mpango huo ni wa kimkakati na ushirikiano wa nchi hizo ni hatua muhimu katika kukabiliana na magonjwa ya mifugo yanayovuka mipaka ya nchi. Mhe. Kamani, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano huo akimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Tanzania imekuwa ikikabiliwa...

DKT. MADELE AFUNGUA MAFUNZO YA ENEO LA KAZI KWA WATUMISHI

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele Septemba 16,2026 amefungua mafunzo kwenye eneo la kazi kwa watumishi wa Wizara hiyo waliopo makao makuu jijini Dodoma ambayo yametolewa na Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi (WCF), Wakala wa usalama na afya mahala pa kazi na Mfuko wa hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma.

DKT. MADELE AFANYA MAZUNGUMZO NA WATAALAM KUTOKA MAURITIUS KUHUSU MIFUMO YA HUDUMA ZA MIFUGO

Picha
Katibu Mkuu wa Mifugo Dkt. Fabian Madele  leo Septemba 15, 2026  amepokea timu ya wataalam kutoka Jamhuri ya Mauritius  iliyoongozwa na Chief Veterinary Officer, Dkt. Beeharry Pitambarsing, na Senior Epidemiologist, Dkt. Bhishnee Devi Mungur, katika kikao kilochofanyika Ofisi za Wizara zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Wataalam hao wamefika nchini kufanya uchambuzi wa utendaji wa mifumo ya huduma za mifugo  pamoja na kutathmini uwezekano wa kusafirishwa kwa vimelea vya magonjwa kupitia biashara ya mifugo na mazao yake kwenda Mauritius. Timu hiyo itakuwa nchini hadi Septemba 18, 2026 ambapo watatembelea maeneo mbalimbali yanayohusiana na huduma za mifugo na usalama wa biashara ya mifugo, yakiwemo Eneo la Kupumzisha Mifugo Kizoto, Kituo cha Karantini cha Alyakeen, Tanga, Bandari ya Tanga, Machinjio ya UMAL, Mashamba mawili yanayouza mifugo kwa ajili ya Machinjio ya UMAL na Maabara Kuu ya Mifugo (TVLA).  Ziara hiyo inalenga kupata uelewa wa kina kuhus...

UVUVI HARAMU KUTAFUTIWA MWAROBAINI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani amewataka watendaji wa Wizara kuja na mwarobaini ambapo utakuwa ni tiba katika kudhibiti uvuvi haramu, na amewataka watendaji hao kuangalia mifumo yao kama inafanya kazi vizuri na kuboresha pale ambapo panahitaji kuboreshwa ili uvuvi haramu ufike kikomo. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 14, 2026, jijini Mwanza, wakati wa kupokea wasilisho la andiko dhana la kudhibiti Uvuvi haramu, andiko ambao litasaidia katika kutokomeza tatizo hilo sugu, andiko ambalo limeandaliwa na Mkufunzi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) Mwanza, Bw. Jackson Bulili pamoja na Mtaalam wa mambo ya Teknolojia kutoka Kampuni ya Affordable Computes and Technology for Tanzania (ACTT) Mwanza, Bw. Amos Zacharia. "Uandishi wa andiko hili linaonesha fika kuwa Wizara inaungwa mkono na wananchi katika kutokomeza Uvuvi haramu" amesema Mhe. Kamani  Aidha, Mhe. Kamani amesema hii inaonesha Wizara itapata namna nyingine ya kupambana na...

WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI MKOANI KIGOMA WAMETAKIWA KWENDA KUZALISHA SAMAKI

Picha
Rai hiyo imetolewa 14 Septemba, 2026 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Bw. Hassan Rugwa Wakati akifunga mafunzo ya wiki nne kwa washiriki 57 wa mafunzo ya ufugaji samaki yaliyoendeshwa  Mkoani Kigoma na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Kigoma kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Ubegiji Enabel kupitia mradi wa wezesha binti. Bw. Rugwa amesema mafunzo waliopata washiriki hawa yawe chachu kwa wao kwenda kufanya shughui za uzalishaji, ufugaji na uchakataji wa samaki kwani Taifa linawategemea waweze kuongeza tija katika sekta ya ufugaji samaki. Naye Mtendaji Mkuu wa FETA Dkt. Semvua Mzighani ambao ndio walioendesha mafunzo hayo amesema kuwa mafunzo haya ni kipaumbele cha Taifa kwa hivi sasa kwani serikali inaweka mkazo katika ukuzaji wa viumbe maji na ufugaji wa samaki. Kwa upande wake Meneja wa FETA kampasi ya Kigoma Bw August Shirima amesema Mafunzo haya yalianza tarehe 17 Agosti mpaka tarehe 11 September 2026 ambapo washiriki kutoka Halmashauri ya kigoma vij...

MHE. KAMANI AKUTANA NA MENEJA TADB KANDA YA ZIWA KUJADILI UWEZESHAJI WA MIKOPO KWA VIJANA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo Septemba 14, 2026 Jijini Mwanza, amekutana na Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) Kanda ya Ziwa, Bw. Ally Janja, katika Ofisi za Benki hiyo na kujadiliana kuhusu Utoaji wa mikopo kwa vijana, mikopo ambayo inatolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kuwezesha vijana kufanya shughuli za uzalishaji katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi.

MHE. KAMANI AWAITA WAWEKEZAJI KUWEKEZA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
◾Ataka wawekezaji kuzingatia ustawi wa wafanyakazi wao.  ◾Ataka wataalam kutatua changamoto za uhaba wa chakula cha samaki na mifugo. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani amewataka wawekezaji nchini kuendelea kuwekeza katika sekta ya mifugo na uvuvi, huku wakizingatia ustawi na usalama wa wafanyakazi wao pamoja na kuhakikisha wanazalisha kwa tija. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 14, 2026, wilayani Magu mkoani Mwanza, wakati wa ziara maalum ya kikazi ya kuwatembelea wawekezaji katika tasnia yaukuzaji viumbemaji, ikiwemo Tangreen Farming Company na M/S ROFI Farming Company Limited, kwa lengo la kujionea shughuli za uzalishaji zinazofanyika katika sekta hiyo. Amesema uwekezaji katika sekta ya mifugo na uvuvi una umuhimu mkubwa katika kuongeza uzalishaji wa chakula, kutoa ajira na kukuza uchumi, hivyo wawekezaji wanapaswa kuhakikisha wafanyakazi wanapata mazingira salama na stahiki za msingi katika maeneo yao ya kazi. Aidha, Mhe. Kamani amewataka wananchi...