ULEGA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA MTEPELEA WILAYANI KILWA MKOANI LINDI
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Mtepela kilichopo Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi, ambapo aliwahimiza kupima, kuyatangaza na kumilikisha maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya malisho ya Mifugo ili yaweze kulindwa na kuepusha migogoro ya mara kwa mara. (29/12/2022) Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akizungumza katika kikao cha Kamati ya Mawaziri wa Kisekta Mkoani Lindi. Pamoja na mambo mengine alitoa rai kwa viongozi wa mkoa huo kulinda misitu ambayo imeendelea kuteketezwa na wakulima wa zao la ufuta kwa kuwa jambo hilo lisiposimamiwa ipasavyo litaleta madhara makubwa ya kimazingira. (29/12/2022) Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri wa Kisekta ambaye pia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Angeline Mabula (Mb) (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack na waheshimiwa mawaziri, naibu mawaziri na wakuu wa wilaya. Naibu Waziri wa Mifugo...