Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2022

ULEGA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA MTEPELEA WILAYANI KILWA MKOANI LINDI

Picha
  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Mtepela kilichopo Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi, ambapo aliwahimiza kupima, kuyatangaza na kumilikisha maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya malisho ya Mifugo ili yaweze kulindwa na kuepusha migogoro ya mara kwa mara. (29/12/2022) Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akizungumza katika kikao cha Kamati ya Mawaziri wa Kisekta Mkoani Lindi. Pamoja na mambo mengine alitoa rai kwa viongozi wa mkoa huo kulinda misitu ambayo imeendelea kuteketezwa na wakulima wa zao la ufuta kwa kuwa jambo hilo lisiposimamiwa ipasavyo litaleta madhara makubwa ya kimazingira. (29/12/2022) Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri wa Kisekta ambaye pia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Angeline Mabula (Mb) (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack na waheshimiwa mawaziri, naibu mawaziri na wakuu wa wilaya. Naibu Waziri wa Mifugo...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Picha
 

KIKAO CHA KAMATI YA MAWAZIRI WA KISEKTA MKOANI MTWARA

Picha
  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Abdallah Ulega (Mb.) akitoa salaam za Wizara wakati wa kikao cha Kamati ya Mawaziri wa Kisekta Mkoani Mtwara Disemba 28, 2022. Pamoja na mambo mengine alisisitiza umuhimu wa kupima, kuyalinda, kuyatangaza na kutoa Hati kwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji. Sehemu ya Kamati ya Mawaziri wa Kisekta (meza kuu), baadhi ya Wabunge wenyeji na wataalam walipowasili Wilaya ya Nanyumbu - Kijiji cha Mbangara kutatua migogoro ya ardhi Disemba 28,2022. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb.),  akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed(kushoto) muda mfupi baada ya kuwasili Ofisi za Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kikao cha Kamati ya Mawaziri wa Kisekta kuhusu migogoro ya Vijiji 975, Disemba 28,2022. Sehemu ya Wananchi wa Kijiji cha Mbangara - Mbuyuni Wilaya ya Nanyumbu, Mtwara wakisikiliza kwa makini maelezo ya Kamati ya Mawaziri wa Kisekta kuhusu utatuzi wa Migogoro ya maeneo yao,  Disemb...

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

VIFARANGA 62,730 VYAZUILIWA KUINGIA NCHINI

Picha
Na Mbaraka Kambona, Wakaguzi wa Mifugo na Mazao yake kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi walio katika kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wamevizuia vifaranga vya kuku wa mayai 62,730 ambavyo ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited ya Mkuranga, Pwani vilivyofikishwa uwanjani hapo vikitokea nchini Ubeligiji bila ya kuwa na vibali. Akitoa taarifa ya zuio la vifaranga hivyo wakati akiongea na Waandishi wa Habari jijini Disemba 24, 2022, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Prof. Hezron Nonga alisema Vifaranga hivyo vilivyowekwa kwenye makasha 697, stakabadhi yake ya mauziano  ya mzigo inaonesha vina gharama ya shilingi 200,262,706. “Mkurugenzi wa Kampuni pamoja na Wakala wa Mmiliki wa vifaranga hivyo walikiri kutokuwa na kibali cha kuingiza vifaranga hivyo na kwa msingi huo amevunja Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Sura ya 156 na Kanuni za Udhibiti wa Usafirishaji wa Wanyama na Mazao yake ya GN. Na. 28/2007,” alisema Prof. Nonga Alisema kutokana na tafsiri hiyo vi...

SEMINA KUHUSU MASUALA YA SUMUKUVU YAFANYIKA KWA WAKUU WA IDARA NA VITENGO WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI (SEKTA YA MIFUGO)

Picha
  Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Huduma za Ugani, Dkt. Angello Mwillawa akiongea na wajumbe (hawapo pichani) wa semina ya wakuu wa Idara wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi masuala yanayohusu  sumukuvu, wakati alipokuwa akifunga semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa African Dream, Dodoma 22.12.2022. Muwasilisha Mada, Dkt. Jamal Kusaga akiwasilisha mada kuhusu hali ya sasa ya sumukuvu nchini, kwenye semina ya kuwapatia wakuu wa Idara wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi masuala yanayohusu sumukuvu, semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa African Dream, Dodoma. 22.12.2022. Mkufunzi wa chuo cha Kilimo (MATI) cha Ilonga, Ms. Mariam Joseph akiwasilisha mada inayohusu "Njia iliyopendekezwa  ya kuzingatia jinsia wakati wa kudhibiti sumukuvu kwenye Semina ya kuwapitisha wakuu wa Idara masuala yanayohusu Sumukuvu, Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa African Dream, Dodoma. 22.12.2022. Afisa TEHAMA kutoka sekta ya Mifugo, Bi Priscilla Joseph (aliyesimama) akichangia mada kwenye...

CHANJO DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA MAPAFU YA NG'OMBE

Picha
 

MABORESHO YA MWONGOZO WA UWEKEJI HERENI YATAMFIKIA KILA MDAU-NDAKI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.  Mashimba Ndaki amebainisha kuwa Wizara yake inaendelea kufanya maboresho ya Mwongozo unaosimamia zoezi la uwekaji wa hereni za kielektroniki kwenye mifugo ili kufanya zoezi hilo kuwa shirikishi kwa pande zote zinazohusiana na sekta ya ufugaji. Mhe. Ndaki ameyasema hayo jana (20.12.2022) wakati akifunga mkutano wa Wadau wa sekta ya Mifugo uliofanyika kwa siku mbili kwenye jengo la PSSSF, Makole jijini Dodoma ambapo amebainisha kuwa mara baada ya kukamilika kwa mchakato wa kuboresha mwongozo huo utakabidhiwa kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu ili atoe hatma ya zoezi hilo. “Kwenye maboresho ya mwongozo huu tutamfikia kila mdau anayehusika na sekta ya mifugo kwa nafasi yake ili baada ya kukamilika kwake kusiwe na malalamiko ya baadhi ya wadau kutoshirikishwa” Amesisitiza Mhe. Ndaki. Mhe. Ndaki ametoa rai kwa wafugaji wote walioshiriki kwenye mkutano huo kuwafikishia wafugaji wenzao elimu waliyoipata kupitia mada mbalimbali zilizowasilishwa wakati wote wa mkutan...

MAFUNZO REJEA KWA WATAALAM WA MIFUGO

Picha
 Afisa Mifugo Mtafiti Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Felister Kimario akizungumzia juu ya uboreshaji wa kosaafu za mbari za mifugo na umuhimu wake katika kukuza sekta ya mifugo wakati wa siku ya pili ya mafunzo rejea ya siku mbili yaliyokuwa yakifanyika katika Mji wa Hai Mkoani Kilimanjaro yakihusisha baadhi ya maafisa ugani kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara. (20.12.2022) Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi katika Halmashauri ya Mji wa Handeni Mkoani Tanga Bw. Zakaria Swai akifafanua juu ya muhtasari ya yaliyojadiliwa katika siku ya kwanza ya mafunzo rejea ya siku mbili yaliyokuwa yakifanyika katika Mji wa Hai Mkoani Kilimanjaro yakihusisha baadhi ya maafisa ugani kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara. (20.12.2022) Afisa Mifugo Daraja la Pili kutoka Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) kilichopo Mkoani Arusha Bw. Samwel Kakungu akielezea umuhimu na hatua mbalimbali zinazof...

CHANJO DHIDI YA UGONJWA WA HOMA YA MAPAFU YA MBUZI

Picha
 

CHANJO DHIDI YA UGONJWA WA KIMETA KWA NG'OMBE, MBUZI NA KONDOO

Picha
 

MAJALIWA ATOA DIRA YA KUBORESHA SEKTA YA MIFUGO NCHINI

Picha
◼️ Aagiza Msomera kutumika kama darasa la Ufugaji nchini  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewataka wadau wa Sekta ya Mifugo kuboresha mifumo ya ufugaji  ili kufanya shughuli hiyo kwa tija ambapo amesisitiza umuhimu wa sekta hiyo kwa Serikali na Mwananchi mmoja mmoja. Mhe. Majaliwa ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Mifugo uliolenga kujadili mwelekeo mpya wa sekta hiyo nchini  uliofanyika katika moja ya kumbi zilizopo jengo la PSSF jijini Dodoma leo (19. 12.2022). Mhe. Majaliwa amesema kuwa licha ya kiasi kidogo cha mchango wa asilimia 7 kwenye pato la Taifa unaotolewa na sekta ya Mifugo, bado ushiriki wa wadau kwenye mabadiliko ya kuelekea kwenye ufugaji wa kisasa upo chini hivyo ameiagiza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanahamasisha zaidi jamii ili  kuboresha Sekta ya Ufugaji ikiwemo kutatua  changamoto  mbalimbali zinazowakumba wafugaji p...

MAFUNZO REJEA KWA MAAFISA UGANI YATAJWA KUTATUA CHANGAMATO ZA SEKTA YA MIFUGO

Picha
Na. Edward Kondela Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepongezwa kwa kutoa mafunzo rejea kwa maafisa ugani kote nchini ikiwa ni njia mojawapo ya mikakati ya kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya mifugo nchini. Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mhe. Juma Irando amebainisha hayo leo (19.12.2022) wakati akifungua mafunzo rejea ya siku mbili kwa maafisa ugani kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara ambapo amesema baadhi ya maafisa hao wanaohudhuria mafunzo wanatakiwa kuwashirikisha maafisa wengine pamoja na wafugaji juu ya mafunzo hayo ili sekta ya mifugo iwe na tija zaidi. Mhe. Irando amesema sekta ya mifugo imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali hali inayosababisha baadhi ya wafugaji kutofuga kibiashara hivyo mafunzo rejea yanayotolewa na wizara hiyo yataleta matokeo chanya kwa maafisa ugani ambao wanategemewa kuwahudumia wafugaji. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Bw. David Lekei amesema wafug...

CHANJO DHIDI YA UGONJWA WA MDONDO (TEMAVAC)

Picha
 

MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO

Picha
 

MAFUNZO KWA MAAFISA UGANI

Picha
 Afisa Tawala Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. John Kusaja akitoa maelezo ya mambo ya msingi ya kuzingatiwa kwa maafisa ugani (hawapo pichani) wakiwa kwenye mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora yakihusisha baadhi ya maafisa hao kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022) Afisa Mifugo Mtafiti Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Felister Kimario akifafanua kwa maafisa ugani waliohudhuria mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, juu ya kuboresha mbari za mifugo na ufugaji kibiashara. Mafunzo hayo yalihudhuriwa na baadhi ya maafisa ugani kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022) Afisa Mifugo Msaidizi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Sebastian Shilangila akiwafah...

WAWEKEZAJI WATAKIWA KUTOA FURSA ZA AJIRA KWA WAZAWA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Pwani Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amewataka wawekezaji katika sekta ya mifugo kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha ajira kwa vijana ili waweze kufaidika moja kwa moja na uwekezaji wao unaofanyika hapa nchini. Waziri Ndaki alitoa kauli hiyo wakati akizindua rasmi ujenzi wa Kiwanda cha Nyama na Machinjio ya Kisasa cha Union Meat Abattoirs Limited (UMAL) unaofanyika katika Kata ya Vigwaza, Halmashauri ya Chalinze, mkoani Pwani Disemba 15, 2022. Alisema ni muhimu sana kwa wawekezaji kutoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi wenye ujuzi na hata wale wasio na ujuzi wakafikiriwe kupewa fursa za ajira ndogo ndogo ili waweze kufaidika na uwekezaji unaoendelea kufanyika katika sekta ya mifugo. "Ndugu zangu, kiwanda hiki kipo miongoni mwa watu hapa Vigwaza, ni wazi kuwa wananchi watakuwa na matumaini kutokana na uwepo wa  kiwanda hiki, naamini mtawapa kipaumbele mtakapoanza uzalishaji wenu, nimeambiwa mtaajiri watu 1500 na kuna watu 300 pia watapata ajira a...