Nav bar

Ijumaa, 23 Desemba 2022

MAFUNZO REJEA KWA MAAFISA UGANI YATAJWA KUTATUA CHANGAMATO ZA SEKTA YA MIFUGO

Na. Edward Kondela


Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepongezwa kwa kutoa mafunzo rejea kwa maafisa ugani kote nchini ikiwa ni njia mojawapo ya mikakati ya kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya mifugo nchini.


Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mhe. Juma Irando amebainisha hayo leo (19.12.2022) wakati akifungua mafunzo rejea ya siku mbili kwa maafisa ugani kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara ambapo amesema baadhi ya maafisa hao wanaohudhuria mafunzo wanatakiwa kuwashirikisha maafisa wengine pamoja na wafugaji juu ya mafunzo hayo ili sekta ya mifugo iwe na tija zaidi.


Mhe. Irando amesema sekta ya mifugo imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali hali inayosababisha baadhi ya wafugaji kutofuga kibiashara hivyo mafunzo rejea yanayotolewa na wizara hiyo yataleta matokeo chanya kwa maafisa ugani ambao wanategemewa kuwahudumia wafugaji.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Bw. David Lekei amesema wafugaji katika wilaya hiyo wameanza kubadilika na kufuga kibiashara kwa kuwashirikisha maafisa ugani ili kuwapatia mafunzo ya ufugaji wenye tija.


Bw. Lekei amesema wafugaji wa Wilaya ya Hai wameanza kutambua juu ya uchaguzi wa mbegu bora za mifugo pamoja na malisho ambayo yatakuwa na matokeo mazuri ya mazao yatokanayo na mifugo yao ikiwemo nyama na maziwa.


Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani (Ugani) kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi amesema lengo la mafunzo rejea kwa maafisa ugani nchini ambapo wizara imepanga kuwafikia maafisa hao 800 kuanzia ngazi ya kijiji, kata na halmashauri katika mwaka huu wa fedha ni kuwajengea uwezo katika utendaji wao wa kazi.

Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mhe. Juma Irando akizungumza leo (19.12.2022) Mjini Hai, wakati akifungua rasmi mafunzo rejea ya siku mbili kwa baadhi ya maafisa ugani (hawapo pichani) kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara ambapo amesema baadhi ya maafisa hao wanaohudhuria mafunzo wanatakiwa kuwashirikisha maafisa wengine pamoja na wafugaji juu ya mafunzo hayo kwa kuwa ni nia ya serikali kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya mifugo nchini. (19.12.2022)

kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Bw. David Lekei akizungumza leo (19.12.2022) Mjini Hai, wakati wa kufunguliwa rasmi mafunzo rejea ya siku mbili kwa baadhi ya maafisa ugani (hawapo pichani) kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara ambapo amesema wafugaji katika wilaya hiyo wameanza kubadilika na kufuga kibiashara kwa kuwashirikisha maafisa ugani ili kuwapatia mafunzo ya ufugaji wenye tija pamoja na kuchagua mbegu bora za mifugo na malisho. (19.12.2022)

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani (Ugani) kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi akifafanua juu ya mwendelezo wa jitihada za wizara kuwaongezea uwezo maafisa ugani ili kuwasaidia wafugaji katika kutatua changamoto zinazowakabili, ambapo amesema katika mwaka huu wa fedha wizara imepanga kuwafikia maafisa ugani 800 kote nchini. Bw. Mdachi amebainisha hayo leo (19.12.2022) katika Mji wa Hai, Mkoani Kilimanjaro wakati wa ufunguzi wa mafunzo rejea ya siku mbili kwa baadhi ya maafisa ugani kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara. (19.12.2022)

Afisa Tawala Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. John Kusaja akitoa maelezo ya mambo ya msingi ya kuzingatiwa kwa maafisa ugani wakiwa kwenye mafunzo rejea ya siku mbili yanayofanyika katika Mji wa Hai Mkoani Kilimanjaro yakihusisha baadhi ya maafisa hao kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara. (19.12.2022)

Picha ya pamoja ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mhe. Juma Irando baada ya kufungua rasmi mafunzo rejea ya siku mbili kwa maafisa ugani kutoka Kanda ya Kaskazini inayohusisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara. Mafunzo hayo yanatolewa na maafisa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi. (19.12.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni