Nav bar

Jumatano, 21 Desemba 2022

MAFUNZO KWA MAAFISA UGANI


 Afisa Tawala Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. John Kusaja akitoa maelezo ya mambo ya msingi ya kuzingatiwa kwa maafisa ugani (hawapo pichani) wakiwa kwenye mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora yakihusisha baadhi ya maafisa hao kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022)

Afisa Mifugo Mtafiti Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Felister Kimario akifafanua kwa maafisa ugani waliohudhuria mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, juu ya kuboresha mbari za mifugo na ufugaji kibiashara. Mafunzo hayo yalihudhuriwa na baadhi ya maafisa ugani kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022)

Afisa Mifugo Msaidizi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Sebastian Shilangila akiwafahamisha maafisa ugani juu ya matumizi ya mfumo wa M-Kilimo wakati wa mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, yaliyohudhuriwa na baadhi ya maafisa ugani kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022)

Afisa Utafiti Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Grace Masolwa akifafanua juu ya matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika ugani kwa maana ya ugani kiganjani wakati wa mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, yaliyohudhuriwa na baadhi ya maafisa ugani kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022)

Afisa Mifugo Mwandamizi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Atupele Mohamed akiwaelekeza baadhi ya maafisa ugani namna ya kutumia mfumo wa M-Kilimo na ugani kiganjani kwa kutumia simu janja, wakati wa mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, yaliyohudhuriwa na baadhi ya maafisa ugani kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022)

Afisa Mfawidhi kutoka Kituo cha Mifugo Kanda ya Tabora Bi. Adelina Mkumbukwa akiwakumbusha maafisa ugani juu ya umuhimu wa kudhibiti magonjwa ya mifugo na namna ya kuwaelekeza wafugaji, ufugaji bora unaozingatia udhibiti wa magonjwa. Bi. Mkumbukwa alikuwa akieleza hayo wakati wa mafunzo rejea ya siku mbili yaliyofanyika katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, yaliyohudhuriwa na baadhi ya maafisa ugani kuanzia ngazi ya kata kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora na Kigoma pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi. (16.12.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni