Nav bar

Jumamosi, 31 Desemba 2022

KIKAO CHA KAMATI YA MAWAZIRI WA KISEKTA MKOANI MTWARA

 


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Abdallah Ulega (Mb.) akitoa salaam za Wizara wakati wa kikao cha Kamati ya Mawaziri wa Kisekta Mkoani Mtwara Disemba 28, 2022. Pamoja na mambo mengine alisisitiza umuhimu wa kupima, kuyalinda, kuyatangaza na kutoa Hati kwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji.


Sehemu ya Kamati ya Mawaziri wa Kisekta (meza kuu), baadhi ya Wabunge wenyeji na wataalam walipowasili Wilaya ya Nanyumbu - Kijiji cha Mbangara kutatua migogoro ya ardhi Disemba 28,2022.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb.),  akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed(kushoto) muda mfupi baada ya kuwasili Ofisi za Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kikao cha Kamati ya Mawaziri wa Kisekta kuhusu migogoro ya Vijiji 975, Disemba 28,2022.

Sehemu ya Wananchi wa Kijiji cha Mbangara - Mbuyuni Wilaya ya Nanyumbu, Mtwara wakisikiliza kwa makini maelezo ya Kamati ya Mawaziri wa Kisekta kuhusu utatuzi wa Migogoro ya maeneo yao,  Disemba 28, 2022.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni