Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2022

WAFUGAJI MKURANGA WAWEZESHWA MADUME YA NG'OMBE AINA YA BORANI*

Picha
Wafugaji Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani wawezeshwa na Serikali madume matatu ya ng'ombe aina ya borani ikiwa ni pamoja na  kuwakwamua wafugaji hao kiuchumi. Wakati akikabidhi madume hayo Januari 27. 2022, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega alisema madume hayo matatu ya ng`ombe aina ya borani yatakwenda kuboresha koosafu za ng`ombe wa asili kwa wafugaji watakao yatumia. "ugawaji wa madume haya bora ya ng'ombe ni  kwa lengo la kuboresha kosaafu za Mifugo Ili  waelekee kwenye ufugaji wa kisasa na hii inaenda sambamba na  utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM (2020 – 2025) inayolenga kuwakwamua kiuchumi wafugaji nchini. Naye Mkurugenzi wa ranch ya Mbogo, Chalinze Mkoani Pwani, Naweed Mulla ambaye wameshirikiana na Serikali kugawa madume hayo  alisema thamani ya madume ni shilingi milioni 15. “Uzalishaji wa Ng’ombe hawa aina ya borani utasaidia  kuboresha koosafu bora ambayo watakuwa bora kwenye uzalishaji wa mazao ya mi...

UCHUMI WA BULUU KUWANUFAISHA WANANCHI - MHE. ULEGA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa kupitia kampeni ya uchumi wa buluu wanakwenda kuimarisha hali za kiuchumi za mwananchi mmoja mmoja hususan wanaoishi katika mikoa ya Pwani ya bahari ya Hindi na Taifa kwa ujumla. Hayo aliyasema wakati wa ziara yake ya kutembelea vikundi vinavyojihusisha na shughuli za kilimo cha mwani, na unenepeshaji kaa katika Wilaya za Pangani, Tanga jiji na   Mkinga, Mkoani Tanga Januari 25, 2025. Alisema kuwa kupitia kampeni hiyo Serikali inakwenda kufanya mapinduzi makubwa ya namna ya rasilimali za bahari zitakavyotumika kuweza kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa wananchi ambao wanategemea bahari kwa ajili ya shughuli za uzalishaji. "Serikali ya Mama Samia inakwenda kuondoa hali duni za wavuvi kwa kuwaunganisha na fursa za kiuchumi zilizopo kwenye ukanda wa bahari ya hindi kwa kushiriki kwenye   fursa zilizopo badala ya kutegemea uvuvi   pekee" alisema Mhe. Ulega. Aidha alisema wanataka watanzania kuhamasika n...

ULEGA AELEZA FURSA ZINAZOPATIKANA KWENYE UCHUMI WA BULUU.

Picha
Serikali ya awamu ya Sita ya Mhe. Samia Suluhu Hassan kupitia programu ya kuendeleza kilimo na uvuvi (AFDP) imetenga takribani sh Bil 29 mwaka 2022/2023 kwa ajili ya kuwezesha kiuchumi shughuli za uvuvi na mikopo kwa wananchi waliopo kwenye sekta hiyo pamoja na kukuza pato la Taifa. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega Januari 24, 2022 wakati wa ufunguzi wa kikao   kazi cha mkakati na kampeni ya   kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe maji bahari kwa viongozi na   wataalam katika Mamlaka za Serikali za mitaa mkoani Tanga. Alisema kuwa sehemu ya fedha hizo takribani sh Bil. 2.1 zinakwenda kukopeshwa kwa vikundi vya wafugaji wa samaki, wakulima wa mwani,wafugaji wa majongoo bahari,   wanenepeshaji wa kamba koche na   kaa, katika ukanda wa bahari ya Hindi.   "Tumekutana sisi wataalamu kwa ajili ya kupeana mbinu na mikakati ya kuweza kuwafikia wananchi ambao ndio walengwa wakuu wa Mradi huo ili kuona namna ambavyo tuta...

WAZIRI NDAKI ATOA MAELEKEZO KWA WAKUSANYA MADUHULI YA SERIKALI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki ametoa maelekezo manne kwa wataalam wa mifugo wanaohusika na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali kwa lengo la kuhakikisha wanafikia lengo lililowekwa.   Waziri Ndaki ametoa maelekezo hayo leo (20.01.2022) kwenye kikao na wataalam hao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Royal Village ambapo aliwaeleza kuwa mwenendo wa ukusanyaji wa maduhuli ya serikali sio mzuri kwani kati ya bilioni 50 zilizokusudiwa kukusanywa ni bilioni 13.9 ndio zimekusanywa.   Katika kikao hicho taarifa za ukusanyaji wa maduhuli ya serikali ziliwasilishwa kwa kila kituo ambapo pia changamoto ziliwasilishwa na kujadiliwa namna gani ya kuweza kukabiliana nazo ili kuhakikisha ukusanyaji wa maduhili unafikia malengo yaliyowekwa   Akizungumza na wataalam hao Waziri Ndaki amesema kuwa wizara iliamua kuunda timu ya ufuatiliaji kwa lengo la kuangalia hali ya ukusanyaji wa maduhuli ya serikali kwenye minada na vituo vilivyo chini ya wizara. Timu hiyo ilibai...

WATAALAM SEKTA YA UVUVI WATAKIWA KUTIMIZA LENGO LA UKUSANYAJI MADUHULI YA SERIKALI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amewataka wataalam wa sekta ya Uvuvi kuhakikisha wanakusanya maduhuli ya serikali ili kutimiza lengo la kukusanya bilioni 40 kwa mwaka wa fedha 2021/2022.   Waziri Ndaki ameyasema hayo leo (15.01.2022) kwenye kikao cha wataalam wa sekta ya uvuvi kilichojadili hali ya ukusanyaji wa maduhuli ya serikali kupitia sekta ya uvuvi ambapo mpaka sasa sekta hiyo imekusanya bilioni 10 kati ya bilioni 40 zilizolengwa.      Katika kikao hicho taarifa za ukusanyaji wa maduhuli ya serikali ziliwasilishwa kwa kila kituo ambapo pia changamoto ziliwasilishwa na kujadiliwa namna gani ya kuweza kukabiliana nazo ili kuhakikisha ukusanyaji wa maduhili unafikia malengo yaliyowekwa.   Akizungumza na wataalam hao Waziri Ndaki amesema kuwa ni lazima wataalam kuhakikisha wanaongeza usimamizi kwenye maeneo yao ili malengo ya ukusanyaji wa maduhuli yatimie. Ili kuhakikisha malengo ya ukusanyaji maduhuli yanafikiwa Waziri Ndaki amese...

ULEGA: SERIKALI YAJA NA SULUHISHO KUKABILIANA NA UKAME, VIFO VYA MIFUGO NCHINI

Picha
Serikali imekuja na suluhisho katika kukabiliana na changamoto za ukame uliosababisha vifo vingi vya mifugo kwa kutumia Sh bilioni 130 ili kuchimba visima, kukarabati na kujenga mabwawa ikianza na maeneo yaliyoathirika zaidi. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe.Abdallah Ulega alieleza mkakati huo wa Serikali Januari 14,2022 wakati alipofanya ziara Wilaya ya Kiteto,Mkoani Manyara ili kuwapa pole kwa kufiwa na ng'ombe 1,874 kati ya Septemba 2020 hadi Januari mwaka huu. "Serikali ya Mama Samia ni sikivu na inawajali wananchi wake, imenituma kuja kuwapa pole kwa kufiwa na ng'ombe wengi waliokufa kutokana na ukame kutokana na kukosa maji na malisho" alisema. Aidha Mhe. Ulega baada ya kushuhudia mizoga ya ng'ombe katika kijiji cha Makame kata ya Makame akiwa katika mikutano ya hadhara kwenye kijiji cha Makame na Ndede alisema, Serikali inawapa Pole lakini imekuja na suluhisho la kukabiliana na ukame huo kwa kuchimba visima na mabwawa kwa ajili ya kunywesha mifugo...

WIZARA YAHIMIZA USHIRIKI WA WAZEE WA KIMILA KATIKA ZOEZI LA UTAMBUZI WA MIFUGO KIELEKTRONIKI

Picha
Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Ukaguzi na Ustawi wa Wanyama kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi,  Dkt. Annette Kitambi amewaomba Viongozi wa Vyama vya Wafugaji nchini kufikisha elimu ya utambizi wa mifugo kwa njia ya hereni za kielektroniki kwa wazee wa kimila ili kusaidia kufanikisha zoezi hilo bila vikwazo. Dkt. Kitambi alitoa rai hiyo  wakati wa kufungua mafunzo ya siku moja ya utambuzi wa mifugo kwa kutumia hereni za kielekroniki jijini Dodoma Disemba 24,2021. Alisema katika jamii za wafugaji hasa wamasai wazee wa kimila ndio wenye nguvu na kusikilizwa na vijana na watu wao wanaowaongoza hivyo endapo elimu hiyo itawafikia itasaidia wafugaji hao kutambua mifugo yao kirahisi. "Chama cha Wafugaji tunawategemea sana kufikisha elimu kwa wafugaji lakini msiwasahau wale wazee maarufu na wazee wa mila kwa sababu akishaelewa akiwaambia watu wa jamii yake wanatekeleza kwa kuwa wanaheshimika", alisema Aliongeza kuwa pamoja na mambo mengine Wizara ya Mifugo imeweka milango wazi k...

WALIOVAMIA KARANTINI YA MIFUGO WATAKIWA KUONDOKA KWA HIYARI*

Picha
Na Mbaraka Kambona, Pwani Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amewataka Wananchi wakiwemo Wafugaji waliovamia eneo la kuhifadhia na kuiangalia kwa muda Mifugo  inayosafirishwa kwenda nje ya nchi kuondoka katika eneo hilo kwa hiyari huku akionya kuwa atakayekaidi Serikali itatumia nguvu kuwaondoa. Waziri Ndaki alitoa wito huo alipotembelea eneo la Karantini ya Kwala iliyopo katika Wilaya ya Chalinze, Mkoani Pwani Disemba 23, 2021.  Alisema kuwa eneo hilo lina maslahi mapana kitaifa na hivyo wananchi kuvamia na kufanya shughuli zao katika eneo hilo linafanya karantini hiyo kupoteza sifa ya kibiashara kimataifa. "Hili eneo lina  maslahi ya kitaifa hivyo wananchi walioingia na kukaa huku bila utaratibu wowote tuwaambie waondoke kwa hiyari, wale tutakaowakuta wakati tutakapoanza kazi ya ujenzi wa Karantini ya kisasa basi tutatumia nguvu kuwaondoa", alisema Mhe. Ndaki Aidha, alisema kuwa mwaka wa fedha ujao watatenga fedha kwa ajili ya kuanza kujenga Karant...

UZINDUZI WA MWONGOZO WA UPATIKANAJI, USIMAMIZI NA UENDELEZAJI WA MAENEO YA MALISHO.

Picha
Waziri ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mwongozo wa Upatikanaji, Usimamizi na Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho katika hafla fupi ya kuzindua mwongozo huo iliyofanyika Mkoani Pwani Disemba 22, 2021. Wakati akizindua Mwongozo huo, Mhe. Ndaki alisema mwongozo huo ukitekelezwa vizuri utatatua changamoto ya malisho na maji kwa mifugo na itasaidia kupunguza migogoro ya Wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katikati) akimkabidhi Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kushoto) nakala ya mwongozo ili awagawie baadhi ya Wakuu wa Mikoa waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa Upatikanaji, Usimamizi na Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho iliyofanyika Mkoani Pwani Disemba 22, 2021.    Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT), Bw. Jeremiah Wambura nakala ya Mwongozo wa Upatikanaji, ...

WATAKAOSHINDWA KUSAJILI MIFUGO KWA HIYARI KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA.

Picha
Serikali imesema itawachukulia hatua wafugaji watakaoshindwa kusajili mifugo yao kwa njia ya utambuzi wa hereni za kielekroniki pindi zoezi hilo litakapofungwa agosti 2022. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Ukaguzi na Ustawi wa Wanyama, Dkt. Annette Kitambi wakati wa utoaji mafunzo ya utambuzi wa mifugo kwa kutumia hereni za kielekroniki Disemba 21,2021 Mkoani Morogoro. Alisema kwa sasa zoezi hilo linaendelea kwa utoaji elimu kwa wataalam na viongozi kutoka Serikali za mitaa ngazi ya mkoa na wilaya pamoja na wafugaji ambao kwa pamoja watahusika katika kutekeleza zoezi hilo linalotarajiwa kuanza mapema Januari mwakani. "Sheria zipo lakini kwa sasa hivi tunafanya kwa kuwahamasisha na kuwaelimisha, zoezi hili litaenda mpaka agosti mwakani tutakuwa tumemaliza kwa hiyari ndipo sheria zitaanza kutumika na sheria imeweka wazi kwamba ikibainika haijatambulika utapigwa faini ya shilingi milioni 2 au kwenda jela miezi sita au vyote kwa pamoja" alisema Akisoma ...