WAFUGAJI MKURANGA WAWEZESHWA MADUME YA NG'OMBE AINA YA BORANI*
Wafugaji Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani wawezeshwa na Serikali madume matatu ya ng'ombe aina ya borani ikiwa ni pamoja na kuwakwamua wafugaji hao kiuchumi. Wakati akikabidhi madume hayo Januari 27. 2022, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega alisema madume hayo matatu ya ng`ombe aina ya borani yatakwenda kuboresha koosafu za ng`ombe wa asili kwa wafugaji watakao yatumia. "ugawaji wa madume haya bora ya ng'ombe ni kwa lengo la kuboresha kosaafu za Mifugo Ili waelekee kwenye ufugaji wa kisasa na hii inaenda sambamba na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM (2020 – 2025) inayolenga kuwakwamua kiuchumi wafugaji nchini. Naye Mkurugenzi wa ranch ya Mbogo, Chalinze Mkoani Pwani, Naweed Mulla ambaye wameshirikiana na Serikali kugawa madume hayo alisema thamani ya madume ni shilingi milioni 15. “Uzalishaji wa Ng’ombe hawa aina ya borani utasaidia kuboresha koosafu bora ambayo watakuwa bora kwenye uzalishaji wa mazao ya mi...