Machapisho

TALIRI YATAKIWA KUFANYA TAFITI ZITAKAZOLETA TIJA SEKTA YA MIFUGO.

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel ameiagiza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), kufanya tafiti zitakazo lisaidia taifa kupiga hatua kupitia sekta ya mifugo.   Prof. Ole Gabriel, aliyasema hayo wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya jiji   Mkoani Dodoma Aprili 23, 2021.   Akizungumza na Wajumbe wa baraza hilo Prof. Ole Gabriel alisema   kuwa, hakuna Taasisi nyingine ambayo Wizara hiyo inaweza kuitegemea katika suala la utafiti zaidi ya TALIRI, hivyo ni lazima ifanye tafiti zitakazo boresha sekta ya mifugo nchini na kuchangia pato la taifa. “Tusibakie kujisifu tuu kuwa Tanzania ni nchi ya pili barani Afrika kwa idadi kubwa ya mifugo lazima tujisifie kwa namna tutavyoweza kutumia sekta hii kukuza uchumi wa taifa” alisema Prof. Ole Gabriel   Alisema kuwa tafiti ndizo zinaweza kulisadia taifa kutoka h...

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KUDHIBITI MLIPUKO WA MAGONJWA YA NGURUWE

Picha
Serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa mlipuko wa magonjwa ya Nguruwe hayajitokezi mara kwa mara nchini.   Haya yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega leo (23.04.2021) wakati akijibu swali Bungeni lililoulizwa na Mbunge wa Jiombo la Ndanda, Cecil Mwambe.   Ulega amesema serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeweka mikakati kuhakikisha inadhibiti mlipuko wa magonjwa ya nguruwe. Mikakati hiyo ni pamoja na Kuhimiza wafugaji kuacha kufuga nguruwe kwa njia huria, Kuzuia wageni kuingia kwenye mabanda ya nguruwe, Kuhimiza wafugaji kupulizia dawa za kuua virusi na kupe kwenye mabanda na kuweka dawa ya kuchovya kwenye milango ya mabanda, Kuweka katazo la kusafirisha nguruwe na mazao yake kutoka sehemu zenye ugonjwa.   Vilevile Kuhimiza wafugaji kutokuruhusu wachinjaji au wafanyabiashara kuingia katika mabanda na kuchagua nguruwe wa kununua, Wafugaji kuepuka kulisha nguruwe mabaki ya vyakula kutoka kwenye hoteli na migahawa, Kuacha kuc...

NDAKI AWATAKA WAFUGAJI KUSIMAMIA MAENEO YALIYOTENGWA KWA AJILI YA MALISHO

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka wafugaji kusimamia maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji na kuhakikisha wanayatunza.   Ndaki ameyasema hayo jana (21.04.2021) wakati akifungua mkutano wa kumi na moja (11) wa siku ya Nyanda za Malisho Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Edema katika mkoani Morogoro.   Wafugaji wametakiwa kuhakikisha wanayasimamia na wanayatunza maeneo yote yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli za ufugaji na kuyaendeleza kwa kupanda malisho na kuweka miundombinu ya maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo yao.   “Ni lazima maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli za ufugaji tunayalinda na kuyaendeleza kwa kupanda malisho na kuweka miundombinu ya maji na siyo kuyaacha yabaki kama mapori kwani watumiaji wengine wa ardhi wanaweza kuanza kuyatumia na baadae migogoro inaanza,” alisema Ndaki.   Ndaki pia amewataka wafugaji kuhakikisha wanaendelea kuomba ardhi kwa ajili ya shughuli za ufugaji katika vijiji na kumili...

DAWATI LA JINSIA LATAKIWA KUANDAA MPANGO KAZI WA KURATIBU SHUGHULI ZA KIJINSIA WIZARANI.

Picha
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji Dkt. Imani Kapinga amelitaka dawati la waratibu wa dawati la uvuvi la jinsia la wizara ya mifugo na uvuvi  kuhakikisha wanaandaa mpango kazi ambao utabainisha shughuli mbalimbali zinazohusu masuala ya kijinsia.   Dkt. Kapinga ametoa kauli hiyo wakati akifungua warsha ya mafunzo ya waratibu wa dawati la uvuvi la jinsia la Wizara ya Mifugo na Uvuvi inayofanyika Mkoani Morogoro Aprili 21-23/2021.     Amesema mafunzo hayo wanayoyapata ni muhimu   sana katika kujenga uwezo wa utekelezaji wa mpango kazi ambao utaongeza ufanisi katika dawati na kuwataka kuwa wasikivu ili kufikia malengo tarajiwa.   “Baada ya mafunzo haya tunaanza mpango kazi ambao utabainisha shughuli mbalimbali za kijinsia na hii itasaidia sana kuongeza ufanisi wa dawati lakini pia kuongeza ujumuishi wa masuala ya jinsia katika shughuli za wizara za kila siku” amesema Dkt. Kapinga.   Dkt. Kapinga ameongeza kuwa Serikali inatamb...

NDAKI AWATAKA WATUMISHI KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA

Picha
Na Mbaraka Kambona,   Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kujiepusha na vitendo vya rushwa huku akionya kuwa yeyote atakayebainika kuhusika na vitendo hivyo hatua stahiki zitachukuliwa dhidi yake.   Ndaki aliyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, sekta ya Mifugo uliofanyika jijini Dodoma Aprili 20, 2021.   Akizungumza na Wajumbe wa baraza hilo, Ndaki aliwataka watumishi hao kuzingatia uadilifu na uwajibikaji katika utekelezaji wa shughuli za serikali huku akisema siyo vyema kwa mtumishi wa umma kutajwatajwa kuhusika na matukio maovu yanayoharibu taswira ya serikali.   "Niwaombe watumishi wote mjiepusha na vitendo vinavyokwenda kinyume cha Sheria za nchi na taratibu za kazi, haipendezi kuona mtumishi wa umma anatajwatajwa kwenye kashfa za rushwa, hili siyo jambo jema hata kidogo, epukeni rushwa,”alisema Ndaki   Aliongeza kuwa watumishi n...

MKANDARASI BWAWA LA CHAMAKWEZA ATAKIWA KUKAMILISHA MRADI KWA WAKATI NA KUZINGATIA UBORA

Picha
Na. Edward Kondela   Serikali imemtaka mkandarasi anayejenga bwawa la Kijiji cha Chamakweza kilichopo Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani, kukamilisha bwawa hilo kwa wakati pamoja na kuzingatia ubora ili liweze kuwa na tija kwa jamii ya wafugaji.   Akizungumza (16.04.2021) mara baada ya kufanya ziara ya kikazi ya siku moja kujionea ujenzi wa bwawa hilo, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema endapo kukitokea dosari yoyote katika bwawa hilo wakati wa kipindi cha mwakwa mmoja wa uangalizi mkandarasi atapaswa kugharamia hasara zote pamoja na kuchukuliwa hatua za kisheria.   “Tungetamani hili jambo lifike ukomo ili tupokee huu mradi, na umalize haraka kwa wakati na kingine ubora kwa kuwa usipofanya hivyo kile kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kama kuna kilichoharibika kwanza utalipa fidia, nitakutoza na riba ya kuharibu.” Amesema Prof. Gabriel   Ameongeza kuwa bwawa hilo ambalo lipo katika Jimbo la...

KAMPUNI YA ISRAEL YAANZA MAZUNGUMZO YA AWALI YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA MIFUGO NCHINI

Picha
Na. Edward Kondela. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amekutana na kufanya mazungumzo ya awali na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Smart Holding ya nchini Israel Bw. Avi Postelnik yenye lengo la kuwekeza hapa nchini kupitia sekta mbalimbali zikiwemo za mifugo na uvuvi. Akizungumza jana (16.04.2021) mara baada ya kuhitimisha mazungumzo yao ya awali katika ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo jijini Dar es Salaam, Prof. Gabriel amesema katika mazungumzo yao wameainisha fursa kubwa zilizopo hapa nchini ikiwemo ya unenepeshaji mifugo na uongezaji thamani wa bidhaa zitokanazo na mazao ya mifugo. Amesema nchi ya Israel ina ng’ombe ambao wana uwezo wa kutoa lita 40 hadi 50 za maziwa kwa siku moja na kwamba Bw. Postelnik amewaona ng’ombe wa aina hiyo hapa nchini katika Mkoa wa Kagera. “Kwa bahati nzuri tayari kosaafu hiyo ya ng’ombe ameiona hapa Tanzania katika Mkoa wa Kagera na tuna dume la ng’ombe kutoka nchini Israel, ambalo l...