MAUZO YA NYAMA NJE YA NCHI YAONGEZEKA - DKT. MUSHI
Mauzo ya nyama nje ya nchi yameongezeka kutoka tani 1,774.00 mwaka 2020/2021 hadi kufikia tani 10,415 katika mwaka 2020/2022. Hayo yamesemwa na Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) Dkt. Daniel Mushi Oktoba 28,2022 Jijini Dodoma wakati akieleza utekelezaji wa majukumu ya bodi hiyo kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Amesema mwaka 2018/2019, waliuza tani za nyama 1,759 wakati mwaka 2019/2020 waliuza tani za nyama 692.46. “Kwa mwaka wa fedha uliopita tuliuza nyama nje ya nchi tani 10,415 ni kiasi ambacho hatujawahi kufikia kukiuza na hii imetupatia Sh96 bilioni...Kiasi kikubwa cha fedha kimepatikana kutokana na kuuza nyama nje ya nchi,”amesema. Amesema katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 wameuza tani 3,256.60 za nyama nje ya nchi. Amesema mkakati wao kwa mwaka 2022/2023 ni kuongeza kiasi cha nyama kinachouzwa nje ya nchi ambapo hadi sasa wanauza kwa kiasi kikubwa katika nchi za Mashariki ya Kati. Amezitaja nchi zinazouzwa nyama kutoka Tanzania ni Qatar,...