Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2020

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

MAZIWA BONANZA

Picha
 

WAFUGAJI NA WAKULIMA KUNUFAIKA KUPITIA KIWANDA CHA NYAMA NGURU HILLS

Picha
Serikali imesema katika kuboresha na kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali nchini ukiwemo Mkoa wa Morogoro, inasisitiza uwepo wa miradi ambayo itakuwa na manufaa makubwa kwa makundi yote mawili.   Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema hayo (28.11.2020) katika Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro alipotembelea ujenzi wa mradi wa kiwanda cha nyama katika Ranchi ya Nguru Hills na kubainisha kuwa mradi huo unaotarajia kukamilika mwezi Aprili Mwaka 2021 utakuwa na manufaa makubwa kwa wafugaji na wakazi wa Mkoa wa Morogoro.   “Tumekuja kuangalia shughuli zinazoendelea kutokana na kikao ambacho tulikuwa nacho katika ofisi ya katibu tawala wa mkoa na mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika kuboresha shughuli za mifugo kwenye mkoa huo na kuondoa changamoto za migogoro ya wafugaji ambapo uongozi wa mkoa waliniambia juu ya mradi huu ambao utakuwa na msaada mkubwa sana kwa wakulima na wafugaji wa mkoa wa M...

WAFUGAJI WASHAURIWA KUWEKEZA KATIKA KILIMO CHA MALISHO.

Picha
WAFUGAJI WASHAURIWA KUWEKEZA KATIKA KILIMO CHA MALISHO   Wafugaji wa Ng’ombe wameshauriwa kujikita katika kilimo cha Malisho ili wawe na uhakika wa malisho bora kwa ajili ya mifugo yao na kuachana na uchungaji wa kutafuta malisho.   Mtendaji Mkuu wa Shamba la Ndoto, Hartmut Rottcher aliyasema hayo kwa Wakurugenzi na Mameneja wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi waliotembelea shamba la mfano la Ndoto lililopo Mkoani Iringa Novemba 27, 2020.   Rottcher alisema kilimo cha malisho yaliyo bora kinasaidia kuwapatia mifugo uhakika wa chakula bora huku akieleza kuwa mifugo ni muhimu kupewa pumba kwa kiasi na sio kuzidisha kwani kufanya hivyo hupelekea ng’ombe kupata asidi tumboni na kuuwa bakteria ambao husaidia kukata kata majani tumboni kwa mnyama.   Alisema kuwa yeye anafanya kilimo cha malisho kwa kumwagilia na ametenga maeneo katika mashamba yake illi kusaidia kulisha mifugo kwa mzunguko na kuipatia mifugo  mahitaji  wanayotaka na sio kuletewa cha...

SERIKALI YAJIPANGA KUIMARISHA SEKTA YA UVUVI NCHINI

Na Mbaraka Kambona, Singida.   Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ipo katika mchakato wa kukamilisha Mpango kabambe wa miaka 15 ijayo kuanzia 2021 utakaosimamia sekta ya Uvuvi na kutoa dira ya kulinda rasilimali za uvuvi ili sekta hiyo iweze kutoa mchango mkubwa na endelevu katika pato la taifa.   Hilo limefahamika wakati Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akifungua Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Uvuvi wa kupitia, kujadili na kuidhinisha masuala ya kipaumbele yanayopaswa kuingizwa katika Mpango huo Kabambe unaofanyika Mkoani Singida Novemba 26-28, 2020.   Dkt. Tamatamah alisema kuwa lengo la Serikali ni kuona sekta ya Uvuvi inaendelea kutoa mchango mkubwa katika pato la taifa zaidi ya ilivyosasa na ndio maana inaanda Mpango huo ili usimamizi wa rasilimali za uvuvi uwe imara.   “Ni mategemeo yetu kuwa mpango huu utatoa hamasa kwa sekta ya uvuvi katika kulinda usalama wa chakula kuanzia ngazi ya kaya na taifa, vi...

PROF. OLE GABRIEL AWAFUNDA WASOMI HOMBOLO

Picha
Na Mbaraka Kambona,   Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel amewaeleza wanafunzi wa Chuo cha Serikali za Mitaa- Hombolo kuwa wao ni Viongozi watarajiwa hivyo wanawajibu wa kuhakikisha watakapokuwa viongozi wanakidhi matarajio ya wale watakaokuja kuwaongoza.   Prof. Gabriel aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada iliyohusu nafasi ya viongozi wa kuchaguliwa katika kuleta maendeleo kwa jamii anayoiongoza kwenye hafla ya kuwatunuku zawadi wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao na wafanyakazi bora wa chuo cha Hombolo iliyofanyika katika chuo hicho kilichopo Dodoma Novemba 25, 2020.   Alisema kuwa katika kipindi hiki ambacho nchi ya Tanzania imeingia katika uchumi wa kati viongozi wanawajibu mkubwa wa kuhakikisha kwamba wanakidhi matarajio ya Watanzania.   Prof. Gabriel aliongeza kuwa nchi nyingi na taasisi zimekuwa zikikwama kufikia malengo tarajiwa kwa sababu ya kukosa usimamizi mzuri.   “Kuwa na rasil...

BARAZA LA VETERINARI LAKIFUNGIA KITUO CHA AFYA SENDEU

Picha
Baraza la Veterinari Tanzania limekifungia kituo cha huduma ya afya ya wanyama cha Sendeu kilichopo Wilayani Longido, Mkoani Arusha kwa kubainika kutokuwa na wataalam waliosajiliwa na Baraza hilo.   Baraza limefikia hatua hiyo mkoani humo Novemba 22, 2020 kufuatia ukaguzi unaoendelea kufanywa katika mikoa mbalimbali nchini na wakaguzi wa baraza hilo ikiwa ni sehemu ya majukumu yao ya kila siku.     Msajili wa Baraza Veterinari Tanzania, Dkt. Bedan Masuruli alieleza kuhusu uamuzi huo wa baraza ofisini kwake, jijini Dodoma Novemba 23, 2020.   Dkt. Masuruli alisema kuwa uamuzi huo wa baraza umefikiwa baada ya kujiridhisha kuwa kituo hicho cha afya ya wanyama kinaendesha shughuli zake kinyume cha taratibu.   Aliongeza kuwa wakaguzi wa baraza walipoenda kufanya ukaguzi katika kituo hicho walibaini mapungufu hayo ambayo kimsingi ni kinyume cha taratibu na ni hatari kwa afya ya wanyama.     Aidha, Dkt. Masuruli aliwahimiza wamiliki wote wa...

JINSI YA "KU-SUBSCRIBE" MIFUGOUVUVI ONLINE TV

Picha
 

WADAU WA UVUVI WAKUTANA KUPITIA MPANGO KAZI UVUVI MDOGO

Picha
 Na Mbaraka Kambona, Wadau wa Sekta ya Uvuvi kutoka maeneo mbalimbali wamekutana kujadili na kupitisha rasimu ya mpango wa kitaifa wa kutekeleza mwongozo wa hiari wa kuhakikisha uvuvi mdogo unakuwa endelevu nchini. Akiongea wakati akifungua kikao kazi cha kupitia mpango huo wa kitaifa kilichofanyika jijini Dodoma Novemba 21, 2020, Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Emmanuel Bulayi alisema sekta ya uvuvi inatoa ajira ya moja kwa moja kwa wavuvi wadogo wapatao 202,053 na zaidi ya wananchi milioni 4.5 wanategemea shughuli zinazohusiana na uvuvi ikiwemo uchakataji na biashara ya samaki na mazao mengine. Aliongeza kuwa pamoja na hali hiyo bado wananchi wengi wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi ni masikini huku akisema kuwa hali hiyo haikubaliki na ni kinyume na maelekezo ya sera na miongozo mbalimbali ya maendeleo ya kitaifa ya nchi yetu ikiwemo Sera ya Uvuvi ya mwaka 2015. Bulayi aliendelea kueleza kuwa Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kutatua changamo...

MRADI WA SWIOFISH WASHIRIKISHA WANANCHI KULINDA RASILIMALI ZA UVUVI NCHINI

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah amesema Mradi wa Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi Kusini Magharibi Mwa Bahari ya Hindi (SWIOFish) umewezesha uboreshaji wa miundombinu ya taasisi za wizara hiyo katika kuhakikisha serikali kwa kushirikiana na wananchi inalinda rasilimali za uvuvi katika Ukanda wa Bahari ya Hindi.   Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini katika ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwafahamisha manufaa ya mradi wa SWIOFish, Dkt Tamatamah amesema mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia umewanufaisha pia wavuvi wa Pwani ya Bahari ya hindi, wakulima wa Mwani, wafugaji wa viumbe maji na wachakataji wa mazao ya uvuvi wakiwemo wanawake na jamii inayozunguka maeneo hayo.   “Lengo kuu la mradi huu ni kuimarisha usimamizi madhubuti wa uvuvi katika ngazi ya kijamii, kitaifa na kimataifa na malengo mengine ni kujenga uwezo wa nchi katika kusimamia rasilima...

USHIRIKIANO WA BODI YA MAZIWA NA SEKTA BINAFSI KUONGEZA USINDIKAJI WA MAZIWA HAPA NCHINI

Picha
Bodi ya Maziwa yasisitiza ushirikiano na sekta binafsi katika kuongeza usindikaji wa maziwa nchini.   Hayo yamesemwa na Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa, Bw. Noely Byamungu wakati wa kikao kazi cha kubainisha maeneo ya ushirikishwaji na Sekta Binafsi kilichofanyika jana (20.11.2020) jijini Dar es Salaam.   Kikao kazi hicho kililenga kupitia Mpango Mkakati wa miaka mitano 2020/21-2025/26 wa Bodi ya Maziwa na kubainisha namna ya bora ya ushirikishwaji wa sekta binafsi katika utekelezaji wa majukumu ya Bodi.   Kikao hicho kilihudhuriwa na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda na Makampuni ya Wasindikaji Maziwa ya UHT nchini kutoka kampuni ya Asas Dairies, Tanga Fresh, Milkcom na Azam Dairies, Wabia wa maendeleo kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Mradi wa Wasindikaji wa Maziwa Tanzania (TMPP).   Bw. Byamungu alisema kuwa lengo la Bodi ya Maziwa ni kuwezesha viwanda kuongeza uwezo wa kusindika maziwa ambao kwa s...