Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2020

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

DKT. TAMATAMAH AKISAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Hayati Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mara baada ya kuhudhuria ibada ya misa takatifu ya kumuombea Hayati Mkapa katika uwanja wa uhuru jijini Dar es Salaam. (26.07.2020)

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

BODI YATAKIWA KUWA BUNIFU KUBORESHA HUDUMA ZA LITA

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mifugo (LITA) kuwa bunifu ili kuboresha huduma na kuleta tofauti katika shughuli zao na kufikia malengo yake. Prof. Ole Gabriel aliyasema hayo alipokuwa akifungua kikao kazi cha kwanza cha Bodi mpya ya ushauri ya LITA kilichofanyika jijini Dar es Salaam Julai 25, 2020. Akizungumza katika kikao hicho, Prof. Gabriel aliwahimiza wajumbe wa bodi hiyo kutumia vyema taaluma zao na kuwa wabunifu katika kuhakikisha LITA inaboresha huduma zake na kuleta mabadiliko chanya ya kiutendaji ya Wakala hiyo. "Nawaomba bodi mfanye kazi yenu vizuri na mfanye maboresho kadri itakavyowezekana, shirikianeni kwa ukaribu na wadau wengine ili kusaidia kuboresha shughuli zenu," alisema Prof. Gabriel. Sambamba na hilo, Prof. Gabriel ameitaka bodi hiyo kuhakikisha inasimamia vyema rasilimali fedha za taasisi hiyo huku akiwaeleza kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuv...

MAKATIBU WAKUU WAKUTANA KUJADILI MAANDALIZI YA NANE NANE 2020

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya leo (24.07.2020) ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu wa wizara za kisekta kujadili maandalizi ya Maonesho ya Kilimo Nane nane yatakayofanyika kitaifa mkoani Simiyu kuanzia tarehe 01 Agosti, 2020. Katika kikao hicho, Bw. Kusaya   alieleza kuwa ni matarajio ya wizara ya kilimo na zile za kisekta kuona maonesho ya Nane nane mwaka huu yanakuwa tofauti katika kuleta mapinduzi ya, ufugaji na uvuvi ili wananchi wapate kuongeza tija na ufanisi kukuza uchumi wa kaya na taifa. Kikao hicho kimehusisha Makatibu Wakuu ambao ni Prof. Riziki Shemdoe (Viwanda na Biashara), Prof. Elisante Ole Gabriel (Mifugo), Mhandisi Anthony Sanga (Maji) na Dkt. Rashid Tamatamah (Uvuvi) na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Miriam Mmbaga pamoja na kamati ya maandalizi. “Tunapenda kuona maonesho ya Nane nane mwaka huu yanakuwa tofauti na yaliyopita katika kuwafanya wakulima, wafugaji na wavuvi   wabadilike kutoka katika   kilimo cha kujikimu kuwa ki...

TANZIA

Picha

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

WARSHA YA KAMATI YA KITAIFA YA MWONGOZO WA HIARI WA KUHAKIKISHA UVUVI MDOGO UNAKUWA ENDELEVU

Picha
Picha ya Pamoja ya baadhi ya Washiriki wa warsha ya kutoa maoni juu ya Mwongozo wa Hiari wa kuhakikisha Uvuvi Mdogo unakuwa endelevu iliyofanyika katika Kata ya Kilwa Kivinje,Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020) Mratibu wa Mpango wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Uvuvi Mdogo, Bi. Lilian Ibengwe (picha ya pili kulia) akikusanya Maoni ya wadau kwenye Warsha ya kutoa Maoni ya Wadau wa Uvuvi Mdogo katika Kata ya Kilwa Kivinje,Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020) Mdau wa Uvuvi Mdogo, Bw.Faridu Shaweji wa Kilwa Kivinje akitoa Maoni yake leo kwenye Warsha ya utoaji maoni kwenye Warsha ya kutoa Maoni ya Wadau wa Uvuvi Mdogo katika Kata ya Kilwa Kivinje, Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020) Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Mwongozo wa Hiari wa kuhakikisha Uvuvi Mdogo unakuwa endelevu, Bw.Yahaya Mgawe akitoa maelezo kwenye Warsha ya kutoa Maoni ya Wadau wa Uvuvi Mdogo katika Kata ya Kilwa Kivinje, Halmashauri ya Kilwa Masoko. (22.07.2020)

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

TANGAZO KWA UMMA

Picha

EXAMINATION NUMBERS FOR CANDIDATES EXPECTING TO SIT FOR QUALIFYING EXAMINATION.

kupata orodha,  bofya hapa

ADDITION EXAMINATION NUMBERS FOR CANDIDATES EXPECTING TO SIT FOR QUALIFYING EXAMINATION.

ADDITION EXAMINATION NUMBERS FOR CANDIDATES EXPECTING TO SIT FOR QUALIFYING EXAMINATION. kupata orodha ,  bofya hapa

KUELEKEA NANENANE 2020

Picha

NANENANE 2020

Picha

NARCO YAMSIMAMISHA KAZI MENEJA WEST KILIMANJARO

Picha
Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO), Masele Mipawa amemsimamisha kazi Meneja wa Ranchi ya West Kilimanjaro iliyopo Kilimanjaro, Hezron Kyaruzi kwa tuhuma za kukosa uadilifu kwa mali za Umma na kusababisha upotevu wa Ng’ombe takriban 32. Akiwa katika ziara ya kutembelea Ranchi hiyo ya West Kilimanjaro Mipawa alisema kuwa waliamua kufanya maamuzi hayo kufuatia changamoto nyingi zinazolikumba shamba hilo ambazo kwa kiasi kikubwa zimechangiwa na uongozi mbovu wa meneja huyo. “Kutokana na upotevu wa Ngombe, uzembe na ukosefu wa maadili tumeamua kumsimamisha kazi Meneja wa Ranchi na Msaidizi wake na hatua nyingine za kisheria na kinidhamu zitafuata ", alisema Mipawa Mipawa alisema ziara hiyo aliyoifanya katika Ranchi hiyo ilikuwa na lengo la kufanya ukaguzi kutokana na taarifa walizokuwa wakizipata ambazo zilionesha kuwa katika shamba hilo kumetokea upotevu wa Ng’ombe ambao Kampuni ya NARCO haina taarifa nao. Ziara hii pia imesaidia kubaini kuwa kun...

SIJARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI - DKT. TAMATAMAH.

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah hajaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Jeongo la Utawala la Ofisi ya Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) unaoendelea katika Kisiwa cha Mafia. Dkt. Tamatamah aliyasema hayo baada ya kukagua kazi za ujenzi zinazoendelea ambapo hakuridhishwa na kasi ya ujenzi kwani haiendani na muda uliotumika kwa mujibu wa mkataba. "Sijaridhishwa na kasi ya ujenzi niliyoikuta hapa hivyo ninakuagiza mkandarasi kuhakikisha unazingatia ratiba na muda uliopangwa kulingana na mkataba" Alisisitiza Dkt. Tamatamah. Jengo hilo linasimamiwa na mkandarasi mwelekezi "Y&P architects" linatarajiwa kutumiwa na MPRU kama ofisi mara baada ya kukamilika kwake ambapo litasaidia kuongeza ufanisi wa taasisi hiyo. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto), baadhi ya watendaji wa sekta ya Uvuvi na baadhi ya watendaji wa kampuni ya "Y & P Architects" wakianga...

MSAJILI WA BARAZA LA VETERINARI AKAGUA BAADHI YA MADUKA YA HUDUMA ZA PEMBEJEO ZA MIFUGO - DODOMA

Picha
Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania, Dkt. Bedan Masuruli akikagua moja ya Duka la utoaji huduma za Pembejeo za Mifugo la Blessing Agrovet Techical. Kushoto ni Bi.   Upendo Hamisi ambae ni mtoa huduma katika duka hili. (17.07.2020) Msajili wa Baraza la Veterinari picha ya kwanza (kulia) akifunga Duka la Blessing Agrovet Technical kwa kufuli lake. Wa kwanza kushoto ni mtoa huduma za Mifugo katika duka hilo, Bi. Upendo Hamisi akitii amri ya kufunga duka kwa kufuli kutokana na kushindwa kutimiza baadhi ya masharti muhimu ya utoaji huduma kwa kutokuwa na daktari wa mifugo aliyesajiliwa na kutohuisha jina la mtoa huduma katika Baraza la Vetenari ili awe kuwa na uhalali wa kutoa huduma. (17.07.2020) Msajili wa Baraza la Veterinari picha ya kwanza (kulia) akifunga Duka la Blessing Agrovet Technical kwa kufuli lake. Wa kwanza kushoto ni mtoa huduma za Mifugo katika duka hilo, Bi. Upendo Hamisi akitii amri ya kufunga duka kwa kufuli kutokana na kushindwa kutimiza baadh...

ZIARA YA KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI (MIFUGO) WILAYANI KONGWA

Picha
Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo, Prof. Elisante Ole Gabriel, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Elligy Shirima, uongozi wa taasisi ya PASS, pamoja na wafanyakazi wa TALIRI na vijana wanaopatiwa mafuzo ya ufugaji bora wa mbuzi na PASS. (17.07.2020) Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyesimama) akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Wilaya ya Kongwa pamoja na vijana wanaopatiwa mafunzo ya unenepeshaji wa mbuzi na taasisi ya PASS, ambapo amewataka kuhakikisha mafunzo hayo yanakuwa chanzo cha wao kujiajiri na kuajiri vijana wengine kupitia ufugaji. (17.07.2020) Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (akitembelea) jengo la kituo cha mauzo ya nyama ya mbuzi linalojengwa katika kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Wilaya ya Kongwa kwa kushirikiana na taasisi ya PASS ambayo...

SAUTI YETU WIKI HII

Picha

SAUTI YETU WIKI HII

Picha

DKT. NANDONDE ATEMBELEA KIWANDA CHA MOTHER DAIRIES LIMITED

Picha
Mkurugenzi wa uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Felix Nandonde jana alitembelea kiwanda cha kusindika maziwa cha Mother Dairies Limited kilichopo Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Katika ziara hiyo ya kikazi Meneja wa uzalishaji wa kiwanda hicho Bw. Alle Makene alimweleza Dkt. Nandonde kuwa kiwanda kina uwezo wa kusindika lita za maziwa 5000 kwa siku na sasa kinasindika lita 2000 kwa siku sawa na asilimia 40 ya uwezo wa kiwanda hicho. Kituo kinakusanya maziwa kutoka kwa wafugaji kupitia vituo vitatu (Milk collection centres) ambapo kiwanda kinanunua maziwa kwa bei ya shilingi 900 kwa lita moja kutoka kwa wafugaji. Kiwanda cha Mother Dairies Limited kinatengeneza maziwa fresh na mtindi ambayo huuzwa katika masoko ya mikoa ya Lindi, Dar es Salaam na Pwani. Kiwanda hicho kina utaratibu wa kuuza maziwa kabla ya kuwekwa kwenye vifungashio (bulk sale) kwa bei ya shilingi 1200 kwa lita moja ya maziwa fresh na shilingi 1300 kwa maziwa ya mtindi. Aidh...

ZIARA YA KATIBU MKUU UVUVI - FETA & TAFIRI

Picha
Mkandarasi kutoka kampuni ya PETRA ENGINEERING, Eng. Basem Abu Ghalyoun akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa pili kutoka kulia mbele) wakati wa ziara yake aliyoifanya ya kukagua maendeleo ya ujenzi kwenye taasisi hiyo Dar es Salaam. (16.07.2020) Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto) akioneshwa michoro ya jengo la    Taasisi ya Utafiti wa masuala ya Uvuvi (TAFIRI) wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye taasisi hiyo na Chuo cha Uvuvi (FETA). (16.07.2020) Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Menejiment ya chuo cha Uvuvi (FETA) wakati wa ziara yake chuoni hapo. (16.07.2020)