SIJARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI - DKT. TAMATAMAH.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah hajaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Jeongo la Utawala la Ofisi ya Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) unaoendelea katika Kisiwa cha Mafia.

Dkt. Tamatamah aliyasema hayo baada ya kukagua kazi za ujenzi zinazoendelea ambapo hakuridhishwa na kasi ya ujenzi kwani haiendani na muda uliotumika kwa mujibu wa mkataba.

"Sijaridhishwa na kasi ya ujenzi niliyoikuta hapa hivyo ninakuagiza mkandarasi kuhakikisha unazingatia ratiba na muda uliopangwa kulingana na mkataba" Alisisitiza Dkt. Tamatamah.

Jengo hilo linasimamiwa na mkandarasi mwelekezi "Y&P architects" linatarajiwa kutumiwa na MPRU kama ofisi mara baada ya kukamilika kwake ambapo litasaidia kuongeza ufanisi wa taasisi hiyo.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto), baadhi ya watendaji wa sekta ya Uvuvi na baadhi ya watendaji wa kampuni ya "Y & P Architects" wakiangalia hatua ya ujenzi iliyofikiwa kwenye jengo la Utawala la Ofisi ya Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) lililopo kwenye kisiwa cha Mafia jana (18.07.2020).

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO