Nav bar

Jumapili, 19 Julai 2020

ZIARA YA KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI (MIFUGO) WILAYANI KONGWA


Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo, Prof. Elisante Ole Gabriel, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Elligy Shirima, uongozi wa taasisi ya PASS, pamoja na wafanyakazi wa TALIRI na vijana wanaopatiwa mafuzo ya ufugaji bora wa mbuzi na PASS. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyesimama) akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Wilaya ya Kongwa pamoja na vijana wanaopatiwa mafunzo ya unenepeshaji wa mbuzi na taasisi ya PASS, ambapo amewataka kuhakikisha mafunzo hayo yanakuwa chanzo cha wao kujiajiri na kuajiri vijana wengine kupitia ufugaji. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (akitembelea) jengo la kituo cha mauzo ya nyama ya mbuzi linalojengwa katika kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Wilaya ya Kongwa kwa kushirikiana na taasisi ya PASS ambayo pia inatoa mafunzo kwa vijana namna ya kunenepesha mbuzi na kufanya biashara ya ufugaji kwa tija. (17.07.2020)



Muonekano wa shamba la malisho ya mifugo la Bw. Mnyonaki Saileni lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma, ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel ameridhishwa na ubora wa malisho hayo. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyesimama katikati) akikagua moja ya mbegu bora ya mbuzi alipotembelea shamba la mifugo la Bw. Mnyonaki Saileni (wa kwanza kulia) alipofanya ziara katika shamba lake lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma. aliyesimama kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Elligy Shirima. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akikagua viwele vya moja ya ng'ombe wa Bw. Mnyonaki Saileni (hayupo pichani) baada ya kutembelea shamba la malisho la mfugaji huyo lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ambapo aliridhishwa na ubora wa mifugo yake kutokana na kupatiwa malisho bora. (17.07.2020)



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (aliyevaa miwani) akikagua malisho ya mifugo katika shamba la mifugo la Bw. Mnyonaki Saileni (aliyeshika fimbo) alipofanya ziara katika shamba lake lililopo Kijiji cha Msujile Kata ya Sejeli wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ambapo aliitaka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kuongeza wigo kwa wafugaji kuwa na mashamba ya malisho. (17.07.2020)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni