Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2023

KUELEKEA MKUTANO WA AGRF

Picha
  #MifugoNaUvuviNiUtajiri

KUELEKEA MKUTANO WA AGRF 2023

Picha
  #MifugoNaUvuviNiUtajiri

WALIOCHOCHEA MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI LINDI KUKIONA

Picha
◾ Silinde na Sagini wacharuka!  Aliyekuwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. David Silinde na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Jumanne Sagini wameamuru kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria wale wote waliohusika kwenye mauaji yaliyotokana na mgogoro wa wafugaji na wakulima kwenye kijiji cha Ngunichile wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi. Viongozi hao wamebainisha hayo leo Agosti 30, 2023 muda mfupi baada ya kufika kijijini hapo kwa ajili ya kuona hali halisi ya mgogoro huo ambapo wamevitaka vyombo vya usalama kuwakamata watuhumiwa wote wa mauaji yaliyotokana na mgogoro huo na kuwafikisha mahakamani. "Wakulima na wafugaji wote ni Watanzania na ni wajibu wetu kama viongozi na watendaji kuhakikisha wanatekeleza shughuli zao kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi na ndio maana Mhe. Rais Dkt. Samia ametuamini na kutuweka katika nafasi tulizonazo" Ameongeza Mhe. Silinde. Aidha Mhe. Silinde amebainisha kuwa uchunguzi wake umebaini migogoro hiyo inachochewa na baadhi ya Vi...

ULEGA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MSAFARA KUTOKA TAASISI YA WORLDLINE YA UFARANSA

Picha
  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (wa pili kutoka kulia) akiongea na Mkuu wa msafara kutoka taasisi ya Worldline ya Ufaransa, Bi. Caroline Jesequel (wa pili kutoka kushoto) alipofika ofisini kwa Waziri huyo jijini Dar es Salaam leo Agosti 28, 2023. Lengo la ziara ya Bi. Jesequel na wenzake ni kujitambulisha na kujenga mazingira ya ushirikiano baina yao na Wizara katika kuboresha mfumo wa utambuzi na takwimu za mifugo. Wa tatu kutoka kulia  ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Daniel Mushi. Wa kwanza kushoto ni Mtaalam wa masuala ya ushirikiano wa kimkakati kutoka Worldline, Bi. Yulia Kostenko. Ujumbe  kutoka taasisi ya Worldline ya Ufaransa ukiongozwa na  Bi. Caroline Jesequel (wa kwanza kulia) wakifuatilia wasilisho kuhusu taarifa ya ufuatiliaji na utambuzi wa mifugo katika kikao kilichofanyika kwenye Ofisi za Wizara zilizopo jijini Dar es Salaam leo Agosti 28, 2023. Wa kwanza kush...

WAZIRI ULEGA ANADI FURSA ZA AJIRA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI KWA WAKUU WA MIKOA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewahimiza Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala kuwahamasisha wananchi kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta za mifugo na uvuvi ili waweze kujiongezea kipato na kujikwamua kimaisha. Waziri Ulega aliyasema hayo muda mfupi baada ya kutoa mada kuhusu fursa za ajira zinazopatikana kwenye sekta za mifugo na Uvuvi wakati wa mafunzo ya uongozi kwa Viongozi hao yanayoendelea kufanyika kwenye shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha, Mkoani Pwani Agosti 26, 2023. "Naomba nitumie fursa hii kuwashawishi hata nyinyi Viongozi kuingia katika fursa hizi hususan za ufugaji wa ng'ombe, kwani zina manufaa makubwa sana, kwa mfano ukianza kufanya unenepeshaji wa ng'ombe nakuhakikishia huwezi kuacha kwa jinsi ilivyo nzuri", alisema Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akitoa ufafanuzi kwa baadhi ya hoja zilizoibuliwa na  Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala muda mfupi baada ya kutoa mada kuhusu fursa za ajira zinazopatikana ...

KUELEKEA KWENYE JUKWAA LA MIFUMO YA CHAKULA AFRIKA (AGRF)

Picha
 

PONGEZI NA SHUKRAN

Picha
 

KUELEKEA KWENYE JUKWAA LA MIFUMO YA CHAKULA AFRIKA (AGRF)

Picha
 

WAZIRI ULEGA AELEZA MIKAKATI YA UKUZAJI CHAKULA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema wamejizatiti kuhakikisha Tanzania inakuwa mzalishaji mkubwa wa chakula kwa ajili ya matumizi ya ndani na nje ya nchi. Ameyasema hayo leo Agosti 22 jijini hapa alipokuwa akifungua warsha ya siku tatu ya wahariri na waandishi wa habari, ikiwa ni maandalizi ya Jukwaa la Mifumo ya Chakula (AGRF) linalotarajiwa kufanyika Septemba. "Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwani tayari tumeanza na BBT LIFE (Building a Better Tomorrow- Livestock and fisheries Enterpreneurs), ili tuwe na uzalishaji mkubwa. "Tuna vijana 700 wanaofundishwa kule Tanga, Mwanza na Kagera," alisema. "Sasa kuna fedha za mabadiliko ya tabia nchi, ambazo mkulima anaweza kulima majani ya mifugo ambayo yatasaidie kuondoa hewa ukaa na kufanya biashara. "Tunaitaka bandari ije haraka ili tusafirishe mifugo, tutasafirishe mbuzi, maana wengine wanataka wachinje wenyewe. Sio tunavutana tu, tunataka mambo yatokee haraka," amesisitiza. Kuhusu masoko, a...

SILINDE AONGOZA MAPOKEZI YA TANI 25.8 ZA SAMAKI WASIOLENGWA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. David Silinde leo Agosti 20, 2023 ameongoza mapokezi ya tani 25.8 ya samaki wasiolengwa au "bycatch" kama inavyojulikana kitaalam ambao wamevuliwa katika ukanda wa bahari kuu. Katika hafla ya mapokezi ya samaki hao wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 85 za kitanzania iliyofanyika Wilaya ya Mwanakwerekwe visiwani Zanzibar Mhe. Silinde ameipongeza kampuni ya "Albacora" inayomiliki meli ya "Pasific Star" kwa kuanza kutekeleza sehemu ya makubaliano baina yake na mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu ambapo Meli hiyo itakuwa ikishusha kiasi cha tani 100 za samaki wasiolengwa kila mwaka. "Samaki hawa tulioanza kuwapokea leo wataongeza mapato ya Serikali kupitia chanzo hiki kipya, usalama wa chakula na lishe na kutokana na wingi wa samaki watakaokuwa wakishushwa nina uhakika hata bei ya samaki hapa nchini itapungua na hivyo kuwawezesha wananchi wengi hususan wenye kipato cha chini kumudu gharama za bidhaa hii" Amesem...

KIKAO KAZI

Picha
 

MAFUNZO YA UFUGAJI MAJONGOO BAHARI YATOLEWA WILAYANI BAGAMOYO

Picha
  Mkurugenzi Msaidizi wa Ugani na Ukuzaji wa Viumbe Maji Bw. Anthony Dadu akitoa salama za utangulizi katika mafunzo hayo kwa vikundi vitano (5) kutoka Bagamoyo ambavo vimepatiwa Elimu ya  muendelezo wa Shuguli za Ufugaji wa Majongoo Bahari,  Ukulima wa Mwani na Unenepeshaji wa Kaa katika kuelekea katika Uchumi wa Buluu. Mkufunzi kutoka Wakala wa Mafunzo ya Uvuvi FETA - Mikindani Bw. Hamis Salehe akitoa elimu ya Ufugaji wa Jongoo Bahari, Kilimo Cha Mwani na Unenepeshaji wa Kaa kwa wanachama wa vikundi kutoka Bagamoyo, tarehe 18/08/2023. Wanachama wa vikundi waliopata elimu ya ukuzaji wa viumbe maji ikiwemo Unenepeshaji wa Kaa, ufugaji wa Jongoo Bahari na Kilimo cha mwani wakimsikiliza Mkufunzi kutoka Wakala wa Mafunzo ya Uvuvi FETA kutoka  Kampasi ya Mikindani Hajupo pichani tarehe 18/08/2023 Wilayani Bagamoyo. Juu: Picha ya pamoja na wana vikundi waliopata mafunzo, na     Chini:  Muonekano wa shamba la Jongoo Baharii Kaole - Bagamoyo Ufugaji wa J...

WAZIRI ULEGA AFANYA MAZUNGUMZO NA MBUNGE WA AFRIKA MASHARIKI MHE. JAMES OLE MILLYA

Picha
  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega(Mb) amekutana  Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. James Ole Millya, na kufanya mazungumzo kuhusu Maendeleo ya sekta ya Mifugo, mazungumzo hayo yamefanyika ofisini kwake Jijini Dodoma,  Agosti 17,2023. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. James Ole Millya, alipoenda kumtembelea ofisini kwake jijini Dodoma Agosti 17,2023.

UFUGAJI WA SAMAKI CHANZO MBADALA CHA KIPATO KWA WAVUVI - ULEGA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema Serikali inaweka msisitizo mkubwa katika ufugaji wa kisasa wa samaki kwa njia ya vizimba ili kuwawezesha wavuvi kuwa na chanzo mbadala cha kipato  na kupunguza utegemezi wa shughuli za uvuvi katika maji ya asili. Mhe. Ulega ameyasema hayo Agosti 16, 2023 wakati wa kufungua Kongamano la wadau la kujadili Sera, Sheria na kanuni za Uvuvi za kimataifa ili ziweze kutumika katika mabadiliko ya mfumo wa Sekta za Uvuvi Barani Afrika  Amesema kwamba lengo la Serikali ni kuweka nguvu kubwa katika ufugaji wa samaki ili kuacha maji ya asili yaweze kupumua na kuondoa wasiwasi wa kipato  kwa wavuvi kila siku "Mtu akiwa na  vizimba vyake  na kufuga samaki vizuri na kuwapeleka sokoni  ana uhakika wa kupata kipato  Alisema Mhe. Ulega Aidha ameongeza  kuwa katika jitihada hizo za Serikali ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi juu ya kulinda rasilimali za uvuvi huku akiongeza kuwa  ni muhimu wadau wenyewe wa...