Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema wamejizatiti kuhakikisha Tanzania inakuwa mzalishaji mkubwa wa chakula kwa ajili ya matumizi ya ndani na nje ya nchi. Ameyasema hayo leo Agosti 22 jijini hapa alipokuwa akifungua warsha ya siku tatu ya wahariri na waandishi wa habari, ikiwa ni maandalizi ya Jukwaa la Mifumo ya Chakula (AGRF) linalotarajiwa kufanyika Septemba. "Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwani tayari tumeanza na BBT LIFE (Building a Better Tomorrow- Livestock and fisheries Enterpreneurs), ili tuwe na uzalishaji mkubwa. "Tuna vijana 700 wanaofundishwa kule Tanga, Mwanza na Kagera," alisema. "Sasa kuna fedha za mabadiliko ya tabia nchi, ambazo mkulima anaweza kulima majani ya mifugo ambayo yatasaidie kuondoa hewa ukaa na kufanya biashara. "Tunaitaka bandari ije haraka ili tusafirishe mifugo, tutasafirishe mbuzi, maana wengine wanataka wachinje wenyewe. Sio tunavutana tu, tunataka mambo yatokee haraka," amesisitiza. Kuhusu masoko, a...