Nav bar

Alhamisi, 31 Agosti 2023

ULEGA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MSAFARA KUTOKA TAASISI YA WORLDLINE YA UFARANSA

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (wa pili kutoka kulia) akiongea na Mkuu wa msafara kutoka taasisi ya Worldline ya Ufaransa, Bi. Caroline Jesequel (wa pili kutoka kushoto) alipofika ofisini kwa Waziri huyo jijini Dar es Salaam leo Agosti 28, 2023. Lengo la ziara ya Bi. Jesequel na wenzake ni kujitambulisha na kujenga mazingira ya ushirikiano baina yao na Wizara katika kuboresha mfumo wa utambuzi na takwimu za mifugo. Wa tatu kutoka kulia  ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Daniel Mushi. Wa kwanza kushoto ni Mtaalam wa masuala ya ushirikiano wa kimkakati kutoka Worldline, Bi. Yulia Kostenko.

Ujumbe  kutoka taasisi ya Worldline ya Ufaransa ukiongozwa na  Bi. Caroline Jesequel (wa kwanza kulia) wakifuatilia wasilisho kuhusu taarifa ya ufuatiliaji na utambuzi wa mifugo katika kikao kilichofanyika kwenye Ofisi za Wizara zilizopo jijini Dar es Salaam leo Agosti 28, 2023. Wa kwanza kushoto ni Mtaalam wa Mifumo ya Utambuzi ya masuala mbalimbali, Bw. Sebastien Spanneut. Katikati ni Mtaalam wa masuala ya ushirikiano wa kimkakati, Bi. Yulia Kostenko.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Prof. Hezron Nonga akiwasilisha taarifa kuhusu ufuatiliaji na utambuzi wa mifugo Wakati wa kikao baina ya Wageni kutoka taasisi ya Worldline ya Ufaransa na Viongozi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kilichofanyika jijini Dar es Salaam Agosti 28, 2023.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (kulia) akisalimiana na Mkuu wa msafara kutoka taasisi ya Worldline ya Ufaransa, Bi. Caroline Jesequel alipofika ofisini kwa Waziri huyo jijini Dar es Salaam leo Agosti 28, 2023. Lengo la ziara ya Bi. Jesequel na wenzake ni kujitambulisha na kujenga mazingira ya ushirikiano baina yao na Wizara katika kuboresha mfumo wa utambuzi na takwimu za mifugo. Katikati ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni