Nav bar

Ijumaa, 19 Mei 2023

UIMARISHWAJI WA TVLA UNAENDA KUSAIDIA KUIMARIKA KWA MIFUGO NCHINI KUWEZA KUPATA MASOKO NJE YA NCHI-PROF.SHEMDOE

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe amefanya ziara kutembelea Maabara za Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kufahamu na kujionea kazi ambazo zinafanywa na Wakala hiyo.

 

Akizungumza wakati wa Ziara yake leo Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam, Prof. Shemdoe amesema uimarishwaji wa TVLA unaenda kusaidia kuimarika kwa mifugo nchini na kuweza kupata masoko mengi nje ya nchi.

 

Amesema TVLA wamekuwa wakifanya maandalizi ya utengenezaji wa chanjo mbalimbali za mifugo ambazo zinasaidia kwa kiasi kikubwa kuzuia maambukizi ya magonjwa mbalimbali kwenye mifugo.

 

"Miaka michache iliyopita tulikuwa tunapeleka nyama nje ya nchi tani elfu moja, lakini sasa mwaka huu ambao tunamalizia mwaka wa fedha tayari tumeshavuka tani elfu 12, kwahiyo tunapoelekea ni mahala pazuri". Amesema Prof. Shemdoe.

 

Aidha amewapongeza TVLA kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya ikiwemo kutambua magonjwa ya mifugo ambayo yapo nchini ili kuweza kuyazuia na kuyatokomeza.

 

Pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha ambazo zimesaidia kuimarisha TVLA na kuweza kufanya kazi kwa weledi mkubwa katika kuhakikisha wanadhibiti magonjwa ya mifugo.

 

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi amesema kuwa wanategemea kwa kiasi kikubwa ziara ya Katibu Mkuu kuzaa matunda kwani ameona ni kwa namna gani TVLA wamekuwa wakijtahidi kuhakikisha inafanya vizuri katika kutekeleza majukumu yake.

 


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kushoto) akipata ufafanuzi kuhusiana na shughuli za kiuchunguzi wa magonjwa yanayoambukizwa na Bioteknolojia kutoka kwa Meneja wa kituo cha Uchunguzi wa Magonjwa yanayoambukiza na Bioteknolojia (CIDB) Dkt Jelly Senyagwa Chang'a aliptembelea Maabara hiyo Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali za Kimaabara.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kushoto) akipata maelezo kuhusiana na namna Maabara ya utambuzi wa magonjwa ya virusi vya mlipuko (CIDB) inavyofanya kazi kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi alipombelea Ofisi ya TVLA Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na TVLA pamoja na kujionea shughuli mbalimbali za Kimaabara.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (wa pili Kulia) akimsikiliza kwa umakini Meneja wa Maabara Kuu ya Mifugo (CVL) Dkt. Geofrey Omarch alipokuwa akitoa maelezo jinsi Maabara kuu ya Mifugo kitengo cha upimaji wa Ubora wa Vyakula vya Mifugo inavyofanya kazi alipombelea Ofisi ya TVLA Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na TVLA pamoja na kujionea shughuli mbalimbali za Kimaabara.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kulia) akipata maelezo wa namna ya upimaji wa vyakula vya Mifugo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Maabara ya Vyakula vya Mifugo wa TVLA Dkt. Scholastica Dotto alipombelea Ofisi ya TVLA Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na TVLA pamoja na kujionea shughuli mbalimbali za Kimaabara.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kulia) akipata maelezo kuhusiana na namna Kitengo cha Uthibiti wa Ubora wa Chanjo kinavyofanya uhakiki wa taarifa zilizochapishwa kwenye Chanjo kama ziko sahihi kabla Chanjo hazijaruhusiwa kupelekwa sokoni. Maelezo hayo aliyapata  kutoka kwa Fundi Sanifu Maabara Bi. Shukuru Joseph Nganga wa Taasisi ya Chanjo Tanzania (TVI - Kibaha),  alipotembelea Taasisi hiyo iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani Mei 12, 2023 kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na Taasisi hiyo hususan utafiti na uzalishaji wa Chanjo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (wa pili kutoka kushoto) akipata maelezo kuhusiana na namna Taasisi ya Chanjo Tanzania (TVI Kibaha) inavyofanya kazi zake kutoka kwa Meneja wa Taasisi ya Chanjo Tanzania (TVI) Dkt. Charles Mayenga alipotembelea Taasisi hiyo iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani Mei 12, 2023 kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na Taasisi hiyo na Uwekezaji wa Serikali katika Uboreshaji wa Miundombinu ya majengo na vifaa.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (Kushoto) akipata maelezo kuhusiana na majukumu yanayofanywa na Wakala kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi (kulia) alipombelea Ofisi ya TVLA Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na TVLA pamoja na kujionea shughuli mbalimbali za Kimaabara.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (kulia) akiongea na vyombo vya Habari mbele ya baadhi ya watumishi wa Makao Makao Makuu ya Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kuhusiana na ziara aliyoifanya Mei 12, 2023 Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu kazi zinazofanywa na TVLA pamoja na kujionea shughuli mbalimbali za Kimaabara.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni