Nav bar

Alhamisi, 17 Novemba 2022

ULEGA AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA TASNIA YA KUKU

 


Mheshimiwa Abdallah Ulega (Mb.), Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi akihutubia wadau wa tasnia ya kuku wakati wa semina iliyoandaliwa na Ubalozi wa Uholanzi Jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Four Points By Sheraton hotel (11/11/2022)


Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania, Mheshimiwa Wiebe de Boer akiwa pamoja na Mgeni Rasmi Mhe. Abdallah Ulega (Mb.), Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi katika semina ya wadau wa tasnia ya kuku iliyoandaliwa na Ubalozi wa Uholanzi Jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Four Points By Sheraton hotel. Semina hiyo ililenga kuwapa ujuzi wadau wa tasnia ya kuku na iliambatana na tukio la kuzinduliwa kwa kitabu cha Mwongozo wa ufugaji kuku (Poultry Signals - A practical Guide to Bird - Focused Poultry Farming). (11/11/2022)


Mheshimiwa Abdallah Ulega (Mb.), Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa tasnia ya kuku pamoja na Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania mara baada ya kufunga semina hiyo (11/11/2022)



Mheshimiwa Abdallah Ulega (Mb.), Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi akimfafanulia jambo na kuelezea fursa za Uwekezaji katika tasnia ya kuku Tanzania. Kulia kwake ni Mheshimiwa Wiebe de Boer, Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania. Hii ilikuwa muda mchache kabla ya kuingia ukumbi wa semina. (11/11/2022)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni