Nav bar

Alhamisi, 17 Novemba 2022

SEKTA YA UVUVI YAFANYA KIKAO KAZI KWA AJILI YA KUIMARISHA DAWATI LA JINSIA

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Sekta ya Uvuvi imefanya kikao kazi kwa ajili ya kuandaa nyaraka zitakazosaidia kuimarisha utendaji kazi wa Dawati la Jinsia la sekta hiyo.

 

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Uendelezaji wa Rasilimali za Uvuvi, Bi. Meresia Mparazo wakati akifungua kikao hicho kilichofanyika kwenye hotel ya Kings Way mkoani Morogoro.

 

Sekta ya Uvuvi imeanzisha Dawati la Jinsia ili liweze kushughulikia masuala yote yanayohusu sekta ya uvuvi katika muktadha wa jinsia yanashughulikiwa katika uendelezaji, uimarishaji na usimamizi wa rasilimali za uvuvi.

 

Bi. Mparazo amesema kuwa dawati hilo limeanzishwa ili kutatua changamoto za jinsia kwa wanaume na wanawake wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi. Kupitia dawati hilo wameweza kuanzisha Jukwaa la Wanawake Tanzania wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi (TAWFA).

 

Mratibu wa Dawati la Jinsia kutoka Sekta ya Uvuvi, Bi. Upendo Hamidu amesema kuwa watu waliochangia kuanzishwa kwa Dawati la Jinsia ni Jukwaa la Wanawake Tanzania wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi (TAWFA) pamoja na wanaume na wanawake wanaojishughulisha na Uvuvi.

 

Upendo amesema lengo la dawati kutatua changamoto zinazowagusa wanawake na wanaume katika shughuli za uvuvi na sio wanawake peke yake katika masuala ya kijinsia japo kwa takwimu za sasa wanawake wanachangamoto nyingi zaidi.

 

Hivyo uwepo wa dawati hili utakuwa mkombozi kwa wadau kwa kuwa dawati litakwenda kutatua changamoto za kijinsia zinazowakabili ili kila mmoja anayejishughulisha na uvuvi aweze kunufaika na rasilimali hizo.

Naye Lilian Ibengwe ambaye ni Afisa Uvuvi Mwandamizi amesema kuwa kupitia kikao kazi hicho, mipango ya kuimarisha dawati inakwenda kuandaliwa, hivyo wadau wanaojishughulisha na uvuvi watambue kuwa serikali inafuatilia masuala ya jinsia katika Sekta ya Uvuvi.

Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Uendelezaji wa Rasilimali za Uvuvi, Bi. Meresia Mparazo (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya kuandaa nyaraka za dawati la jinsia la sekta ya uvuvi iliyofanyika mkoani Morogoro mara baada ya kufungua warsha hiyo. (14.11.2022)


Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Uendelezaji wa Rasilimali za Uvuvi, Bi. Meresia Mparazo akifungua warsha ya kuandaa nyaraka za dawati la jinsia la sekta ya uvuvi iliyofanyika mkoani Morogoro. (14.11.2022)


Baadhi ya washiriki wa warsha ya kuandaa nyaraka za dawati la jinsia la sekta ya uvuvi wakifuatilia mada zilizokuwa zinawasilishwa. (14.11.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni