Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2021

GEKUL AMSIMAMISHA KAZI MKUU WA KITUO CHA UKAGUZI WA MIFUGO RUVU DARAJANI

Picha
Na Mbaraka Kambona, Pwani   Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul amemsimamisha kazi Mkuu wa Kituo cha Ukaguzi wa Mifugo cha Ruvu Darajani, Gabriel Lyakurwa kwa tuhuma za kutorosha mifugo na kusababisha upotevu wa mapato ya Serikali, huku akimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi, Evarist Ndikilo kuwachukulia hatua Watumishi waliochini ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo ambao walikuwa wanashirikiana na Mkuu huyo wa kituo.     Gekul alitoa maamuzi hayo baada ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani kuibua tuhuma hizo katika ziara yake aliyoifanya kwenye kituo hicho kilichopo Ruvu Darajani, Wilayani Bagamoyo Februari 24, 2021.   Mhandisi Ndikilo alisema uchunguzi alioufanya umebaini kuwa Mkuu wa kituo hicho amekuwa akishirikiana na wenzake wasiowaaminifu kutorosha mifugo inayopelekwa katika kituo hicho kwa ajili ya kukaguliwa kabla ya kuruhusiwa kupelekwa katika maeneo mengine ya minada.   “Mhe. Naibu Waziri nimefanya uchunguzi wa ki...

WAZIRI NDAKI ATAKA KUAINISHWA MIPAKA YA HIFADHI YA BAHARI KUONDOA MIGOGORO NA WAVUVI

Picha
Na. Edward Kondela   Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amekitaka Kitengo cha Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) kuhakikisha hadi kufikia Mwezi Agosti Mwaka 2021 kinaweka alama za mipaka katika maeneo yote ya hifadhi za bahari ili kuondoa migogoro kati yao na wavuvi.   Akizungumza jana (23.02.2021) na wananchi katika Kata ya Jibondo iliyopo Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani, Waziri Ndaki ametaka kuwekwa kwa alama za mipaka hiyo baada ya baadhi ya wananchi kulalamikia kutozwa faini mara kwa mara kwa tuhuma za kufanya shughuli za uvuvi kwenye maeneo hayo ambayo hayaruhusiwi kisheria kwa shughuli hizo.   Aidha, Waziri Ndaki akiwa ameambatana na naibu waziri wa wizara hiyo Mhe. Pauline Gekul, amewataka wavuvi kuhakikisha pindi wanapokamatwa kwa makosa mbalimbali ambayo ni kinyume na sheria ya uvuvi kuhakikisha wanapatiwa risiti inayotambulika na serikali ya kieletroniki (EFD) na kuonya watumishi wa serikali wanaopokea fedha za faini bila kutoa risiti...

TALIRI YAJIKITA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFUGAJI

Picha
  Na Mbaraka Kambona, Mpwapwa   Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Jonas Kizima amesema utafiti wanaoufanya umejikita katika kutatua changamoto za mbegu bora za mifugo na mbegu bora za malisho kwa wafugaji ili sekta ya mifugo iweze kuchangia vyema katika pato la Taifa.   Dkt.  Kizima aliyasema hayo alipotembelea kukagua shughuli zinazofanywa na Kituo cha TALIRI Mpwapwa kilichopo Wilayani Mpwapwa, Mkoani Dodoma Februari 18, 2021.   Alisema kuwa lengo la utafiti wanaoufanya ni kuhakikisha wanapata mbegu bora za mifugo na kuzalisha mbego bora za malisho ya mifugo ambazo zitakazosaidia kutatua changamoto za upatikanaji wa mbegu bora za mifugo zinazohimili mazingira yaliyopo na malisho inayoikabili nchi kwa sasa.   Aliongeza kuwa kwa sasa taasisi hiyo inaendelea na kufanya Tathmini ya ubora, ustahimilivu na makuzi ya malisho ya mifugo yatakayofaa kwa chakula cha kutosha kwa ajili ya mifugo.   Kwa ...

MAWAKALA WA KUKU WASIOTAMBULIKA KUKAMATWA

Picha
Na. Edward Kondela   Chama cha Wafugaji wa Kuku wa Nyama   nchini (TABROFA) kimetakiwa kuwa na ushirikiano ili kutokomeza changamoto wanazozipata wafanyabiashara wa kuku hasa mawakala wasiotambulika wanaouza vifaranga vya kuku wa nyama pamoja na vyakula vya kuku kwa bei ya juu katika maeneo mbalimbali nchini.   Akizungumza katika mkutano wa wafanyabiashara na wazalishaji wa vifaranga vya kuku wa nyama jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amesema mawakala wanaotumiwa na wenye viwanda vya kutotolesha vifaranga kama hawajasajiliwa wakamatwe.   “Kuanzia sasa mawakala wa wauzaji wa vifaranga vya kuku pamoja na chakula cha kuku nataka wafuatiliwe na waeleze wapi walisajiliwa”. Amesema Mhe.Ndaki.   Aidha, Mhe. Ndaki amewataka wafugaji wote wanaouza kuku wa nyama   kujisajili   Bodi ya Nyama nchini (TMB) kwa ajili ya biashara kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa atakayekaidi.   Pia, waziri huyo...

WAZIRI NDAKI AKUTANA NA MWAKILISHI WA UMOJA WA MATAIFA KWENYE PROGRAMU YA CHAKULA DUNIANI UN WFP

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kushoto) akijadili jambo na mwakilishi wa Umoja wa Mataifa kwenye programu ya Chakula Duniani UN WFP, Bi. Sarah Gordon - Gibson mara baada ya kuwasili na kujitambulisha na kuangalia maeneo ya mashirikiano ofisini kwake mtumba jijini Dodoma. (16.02.2021) Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa nne kutoka kulia) akiongea na mwakilishi wa Umoja wa Mataifa kwenye Programu ya Chakula Duniani UN WFP, Bi. Sarah Gordon - Gibson (wa tatu kutoka kulia) pamoja na maafisa wengine alioambatana nao wakati walipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma lengo likiwa ni kujitambulisha na kuangalia maeneo ya mashirikiano. (16.02.2021) Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kutoka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na mwakilishi wa Umoja wa Mataifa kwenye programu ya Chakula Duniani UN WFP Bi. Sarah Gordon - Gibson (wa pili kutoka kulia) na Maafisa wengine walioambatana nae mara baada ya kujitambulisha na kuangalia maeneo ...

UHABA WA WATAALAM WENYE UJUZI KILIO KWA WAWEKEZAJI

Picha
Na Mbaraka Kambona, Pwani   Mratibu na Mkurugenzi wa Operesheni, Kiwanda cha Kutengeneza Chanjo cha Hester, Tina Towo Sokoine amesema kuwa lengo la kiwanda hicho ni kutumia Wataalam wa ndani lakini uhaba wa Wataalam wa masuala ya sayansi wenye ujuzi hasa wa vitendo unaelekea    kukwamisha dhamira yao hiyo.   Towo aliyasema hayo alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa kiwanda hicho kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani Februari 13, 2021.   Alisema kuwa kwa sasa wana wataalamu watatu tu kutoka nje ya nchi ambao wamewaajiri katika Kiwanda hicho lakini    kwa hali ilivyo wanaona watashindwa na labda wanaweza kuomba vibali vingine vya kuajiri wataalamu kutoka nje.   “Nia yetu ni kufanyakazi na Watanzania tu lakini bado vijana wengi tunaowafanyia usahili wanakosa ujuzi hasa wa vitendo, tunaiomba Serikali na Vyuo vinavyoandaa h...

PROF. GABRIEL AELEZA KWA UFUPI UMUHIMU WA KIWANDA CHA ACE LEATHER TANZANIA Ltd.

Picha
  Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akieleza kwa ufupi umuhimu wa Kiwanda cha Ace Leather Tanzania Ltd katika kuleta maendeleo ya Sekta ya Mifugo hususan katika tasnia ya ngozi mapema leo wakati wa uzinduzi wa Kiwanda hicho uliofanyika Mkoani Morogoro Februari 12, 2021. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakata Ngozi cha Ace Leather Tanzania Ltd kilichopo Kihonda, Mkoani Morogoro Februari 12, 2021. Kulia kwake ni Mmiliki wa Kiwanda hicho, Rostam Aziz. Wa kwanza kulia, mstari wa nyuma ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel. Wengine ni Viongozi Wakuu wa Serikali na baadhi ya wamiliki wa kiwanda hicho. Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akimueleza jambo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (katikati) walipokutana katika uzind...

NARCO YAAGIZWA KUWANYANG'ANYA VITALU WALIOKIUKA MKATABA

Picha
Na Mbaraka Kambona,   Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki ameiagiza Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kuwanyang'anya wale wote walioshindwa kuendeleza vitalu walivyokodishwa   katika ranchi za kampuni hiyo kwa sababu wamekiuka masharti ya mkataba.   Ndaki alitoa agizo hilo alipokutana na Viongozi wa Chama cha Wafugaji katika kikao cha kujadili Maendeleo ya Sekta ya Mifugo kilichofanyika jijiji Dodoma Februari 10, 2021.   Alisema kuwa kuna watu wengi wamekodishwa maeneo katika ranchi za taifa lakini wamezitelekeza na wengine wamekodisha watu wengine ambao wanatumia maeneo hayo kinyume na makubaliano ya mkataba.   "Ikifika tarehe 15 mwezi huu, wale wote waliochukua vitalu na wamekodisha watu wengine wanyang'anywe maeneo hayo na hatutajali mikataba yao kwani wameshakiuka masharti," alisema Ndaki   Aliongeza kwa kusema kuwa baada ya tarehe 15 kupita wataanza kuwasaka wote waliochukua maeneo hayo na kuwanyang'anya ili wapewe wafugaji m...

WATUMISHI WA UMMA WANAOINGIZA KWA MAKUSUDI MIFUGO KWENYE HIFADHI NA KUNYANYASA WAFUGAJI WAONYWA

Picha
Na. Edward Kondela   Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amesema atazungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii kuhusu kitendo cha baadhi ya watumishi wa umma walio chini ya wizara hiyo, ambao wamekuwa wakiielekeza mifugo kwa makusudi kuingia kwenye hifadhi za taifa ili waikamate na kuwaonea wafugaji kwa kuwalipisha tozo pamoja na kutaifisha mifugo hiyo.   Waziri Ndaki amezungumza hayo jana (09.02.2021) wakati akihitimisha ziara yake ya siku mbili Mkoani Kilimanjaro, kwa kuzungumza na baadhi ya wafugaji katika Wilaya ya Siha mkoani humo mara baada ya kutembelea Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) na Ranchi ya West Kilimanjaro   zilizopo katika wilaya hiyo ili kujionea namna wanavyotekeleza majukumu yao.   Amesema kitendo hicho cha kifisadi hakiwezi kuvumilika na kwamba watuhumiwa wote watatafutwa na kukamatwa ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa ikiwemo kufukuzwa kazi.   “Ninajua kuna wakati tunaonewa unakuta ng’ombe wak...