Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2021

MAUAJI YA MKULIMA YAWE MWANZO NA MWISHO, FUATENI SHERIA, WAZIRI MKUU KITETO IKO SALAMA." WAZIRI NDAKI

Picha
Na. Edward Kondela Serikali imewataka wakulima na wafugaji wanaofanya shughuli zao kwenye maeneo wasiyoruhusiwa, kuondoka mara moja na kuwataka wafuate sheria, taratibu na kanuni za nchi ambapo wakulima na wafugaji wanatakiwa kuwa kwenye maeneo waliyotengewa kisheria bila kuingiliana. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amebainisha hayo (24.01.2021) akiwa katika Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara kutatua mgogoro wa matumizi ya ardhi uliojitokeza hivi karibuni kati ya wakulima na wafugaji katika ukanda wa malisho ya mifugo wa vijiji vya Amei, Loolera, Lesoit na Lembapuri, mgogoro ambao umesababisha kifo cha mkulima Bw. Emelian Malima miaka 45 anayedaiwa kuuwawa na wafugaji (20.01.2021) katika eneo la ukanda wa malisho ya mifugo. Akizungumza na baadhi ya wakulima na wafugaji wanaofanya shughuli zao katika vijiji hivyo, Waziri Ndaki amesema serikali imekuwa ikitenga matumizi bora ya ardhi maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Wilaya ya Kiteto na kwamba maeneo ya wakulima yametengwa kwa ...

NGURUWE WENYE THAMANI YA MILIONI 370 WAMEKUFA KWA HOMA, SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KUDHIBITI

Picha
Na Mbaraka Kambona, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amesema Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha ugonjwa wa homa ya Nguruwe ulioikumba Mikoa ya Kanda ya Ziwa hivi karibuni unadhibitiwa, huku akisema kuwa tangu ugonjwa huo uanze mpaka sasa umeshasababisha vifo vya Nguruwe 1500 wenye thamani ya shilingi milioni 375. Ndaki aliyasema hayo Januari 23, 2021 jijini Dodoma alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari kuhusu hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali katika kuudhibiti ugonjwa huo uliokumba Mikoa ya Kanda ya Ziwa.  Alisema kuwa vifo hivyo vimesababisha hasara ya moja kwa moja kwa wafugaji kwa sababu kipato hicho kilichopotea ilikuwa wakipate wafugaji huku akiwataka wafugaji hao kuwa watulivu na kufuata maelekezo ya serikali ili ugonjwa huo uweze kudhibitiwa kwa haraka. Aliongeza kuwa  ugonjwa huo unaosababishwa na virusi unahama kutoka kwa nguruwe pori na  Ngiri na unasambaa kupitia  njia ya Maji, Damu au Kinyesi. Ndaki alisema kuwa Halma...

MWONGOZO WA UTOAJI WA CHANJO ZA MIFUGO NCHINI WAZINDULIWA, KULINDA AFYA YA MNYAMA

Picha
Na. Edward Kondela Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amezindua mwongozo wa utoaji wa chanjo dhidi ya magonjwa ya mifugo nchini, wenye lengo la kuhakikisha sekta binafsi na umma zinajua haki na wajibu katika zoezi zima la utoaji wa chanjo na kuhakikisha afya ya mnyama inabaki salama. Waziri Ndaki amebainisha hayo (22.01.2021) jijini Dodoma wakati akizindua mwongozo huo baada ya hivi karibuni kuagiza kusimamishwa kwa muda, utoaji wa chanjo unaofanywa na halmashauri nchini kupitia kampuni walizoingia nazo mikataba, baada ya kubaini chanjo kutolewa kiholela kwa mifugo bila kuwepo utaratibu sahihi na kusababisha madhara kwa mifugo na hasara kwa mfugaji. Kufuatia hali hiyo, Waziri Ndaki amesema katika kuhakikisha mwongozo wa utoaji wa chanjo dhidi ya magonjwa ya mifugo nchini, unakuwa na tija kwa taifa ametaka kuwepo kwa haki na wajibu kwa wadau wote wa mifugo ili kuelewa vyema haki na wajibu huo katika kusimamia mwongozo huo na kufikia matokeo chanya katika kuboresha afya ya mif...

MHE. NDAKI ATEMBELEA SHAMBA LA MFUGAJI JOSAM NTANGEKI LILILOPO KWENYE RANCHI YA KIKURURA WILAYANI KARANGWE, MKOA WA KAGERA.

Picha
  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (katikati) akitoa maelekezo mara baada ya kufika kwenye shamba la Mfugaji anayefahamika kwa jina Josam Ntangeki lililopo kwenye ranchi ya Kikukurura wilayani Karagwe Mkoa wa Kagera jana (19.01.2021). Wengine pichani ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel (wa kwanza kushoto) na Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa Bw. Noeli Byamungu (wa kwanza kulia). Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini (TDB) Bw. Noely Byamungu (katikati) akimweleza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kutoka kulia) juu ya namna Bodi inavyompa ushirikiano Mmoja wa wawekezaji wa Ng'ombe wa Maziwa waliopo kwenye ranchi ya Kikulula Bw. Josam Ntangeki (wa pili kutoka kushoto), baada ya Mhe. Mashimba kutembelea ranchi hiyo jana (19.01.2021). Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) na katibu Mkuu wa wizara hiyo (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel wakikagua moja ya ng'ombe waliopo kwenye kitalu cha Mwekez...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YATOA MAFUNZO KWA WADAU WA UVUVI WA KATA YA MIGOLI MKOANI IRINGA

Picha
  Afisa Uvuvi Mwandamizi (WMUV), Hamidu Njegite (aliyesimama katikati) akiwaeleza wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa faida za kuunda ushirika wakati wa Mafunzo rejea kwa wadau hao, yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika katika mwalo wa Migoli na Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021) Diwani wa kata ya Migoli, Mhe. Benitho Kayugwa (aliyevaa suti nyeusi) akifungua Mafunzo rejea ya wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa yaliyokuwa pia na lengo la kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika vya wavuvi. Mafunzo hayo yanafanyika katika mwalo wa Migoli na Chapuya, kata ya Migoli, Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. (18/01/2021) Mkufunzi Mwandamizi (WMUV), Bi. Kresensia Mtweve (aliyesimama katikati) akiwaeleza wadau wa uvuvi wa kata ya Migoli, halmashauri ya Wilaya ya  Iringa jinsi ya kupunguza upotevu wa mazao ya u...

MAAFISA MIFUGO RUDINI KAZINI - GEKUL

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul amewataka Maafisa Mifugo kote nchini kurudi kazini na kushirikiana kwa ukaribu na Chama cha Wafugaji nchini kushughulikia changamoto mbalimbali za wafugaji tofauti na hali ilivyo hivi sasa ambapo Wafugaji wengi bado wameendelea kukosa huduma kwa wakati. Mhe. Gekul ameyasema hayo leo (14.01.2021) wakati akizindua kikao kazi cha chama hicho kwenye ukumbi wa hoteli ya Royal Village jijini Dodoma ambapo alisema kuwa Wizara haitamvumilia Afisa Mifugo ambaye hatotimiza wajibu wake ipasavyo kwa kushindwa kutoa huduma stahiki kwa wafugaji hali inayosababisha watu wengi kukata tamaa kwenye shughuli za ufugaji. "Mfugaji anampigia simu mtaalam na kumsubiri kwa saa kadhaa bila kupata msaada wowote wa kitaalam mpaka mifugo inakufa, kwa kweli hilo sisi hatuwezi kukubali kuona likiendelea" Alisema Mhe.Gekul. Mhe. Gekul alisifu jitihada za Chama Cha Wafugaji nchini kwa jitihada mbalimbali ambazo imeendelea kuzifanya ili kuboresha mazingira y...

KIKAO KAZI CHA KUANDAA MWONGOZO WA KUSIMAMIA RASILIMALI ZA UVUVI KWENYE MAJI MADOGO NA MAENEO OEVU NCHINI

Picha
Kaimu Katibu Mkuu Sekta ya Uvuvi, Bw. Amosi Machilika akisoma hotuba kwa niaba ya Katibu Mkuu Sekta ya Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah wakati wa kikao kazi cha kuandaa mwongozo wa kusimamia Rasilimali za Uvuvi kwenye maji madogo na maeneo oevu nchini kwenye ukumbi wa Chuo cha mipango jijini Dodoma. 14/01/2021 Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi, Bi. Merisia Sebastian Mparaza akieleza lengo la kuandaa mwongozo wa kusimamia Rasilimali za Uvuvi kwenye maji madogo na maeneo oevu nchini wakati wa kikao hichi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi leo kwenye ukumbi wa Chuo cha mipango jijini Dodoma. 14/01/2021 Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Ismail Kimirei akichangia mada wakati wa kikao cha kuandaa mwongozo wa kusimamia Rasilimali za Uvuvi kwenye maji madogo na maeneo oevu nchini wakati wa kikao hichi jijini Dodoma. 14/01/2021   Mkurugenzi wa Idara  ya Utafiti, Mafunzo na Ugani  Sekta ya Uvuvi, Dkt. Erastus Mosha akichangia hoja kwenye kikao kazi cha kuandaa ...

WALIOKAIDI MKATABA WA NARCO KIKAANGONI NDANI YA SIKU KUMI

Picha
Na. Edward Kondela Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki ametoa siku kumi kwa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kubaini na kuwanyang’anya maeneo, wawekezaji waliopatiwa vitalu katika ranchi za taifa ambao wamebadili matumizi ya ardhi kinyume na makubaliano ya mikataba yao. Waziri Ndaki amebainisha hayo jana (12.01.2021) wakati alipotembelea Ranchi ya Usangu iliyopo Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo na kufanya mkutano wa hadhara na baadhi ya wawekezaji, wakulima na wafugaji, ambao wanafanya shughuli zao katika ranchi hiyo na kubaini kuwa baadhi ya wawekezaji waliopatiwa vitalu na NARCO kwa ajili ya kufuga na kulima malisho ya mifugo wamekuwa wakikodisha maeneo hayo kwa wakulima na wafugaji kinyume na mkatabata. “NARCO siku kumi nadhani zinawatosha kubaini watu wanaojiita wawekezaji, waliobadilisha matumizi ya ardhi ambayo siyo kufuga wala malisho wanyang’anywe maeneo kwa kuwa wameenda kinyume na utaratibu wa mkataba kati y...

WAKAGUZI WA NGOZI WATAKIWA KUSIMAMIA UZALISHAJI WA NGOZI BORA

Picha
Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura amewataka wakaguzi wa zao la Ngozi wa Kanda ya Mashariki kusimamia ubora wa Ngozi zinazozalishwa.   Bura ameyasema hayo leo (12.01.2021) wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa Ngozi wa Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro) yanayofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam.   Wakaguzi hao wa Ngozi wametakiwa kusimamia uzalishaji wa zao hilo katika hatua zake zote ili kupata Ngozi zinazofaa kusindikwa katika viwanda.   Aidha, wakaguzi hao wametakiwa kutumia sheria namba 18 ya mwaka 2008 inayolenga kuboresha zao la ngozi ili wadau waweze kuzalisha ngozi bora inayokidhi mahitaji ya viwanda vyetu na hatimaye kuwa na tija ya uzalishaji wa zao hilo.   Bura amesema uzalishaji wa ngozi za ng’ombe na mbuzi kwa siku ni vipande 31,000 lakini ni asilimia 10 tu ya ngozi zinazopelekwa viwandani hufaa kwa ajili ya kusindikwa, na asilimia ...

GEKUL ATEMBELEA WAKALA YA MAABARA YA VETERINARI KIBAHA MKOANI PWANI

Picha
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu, Wakala ya Maabara ya Veterinari (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi akimuonesha Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul moja ya chanjo wanazozalisha alipotembelea Kituo cha Wakala hiyo cha kutengeneza chanjo kilichopo Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani Januari 11, 2021. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu, Wakala ya Maabara ya Veterinari (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi akimuonesha Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul moja ya chanjo wanazozalisha alipotembelea Kituo cha Wakala hiyo cha kutengeneza chanjo kilichopo Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani Januari 11, 2021. Meneja Uzalishaji wa Kiwanda cha TANCHOICE, Selo Luwongo (kushoto) akimuonesha Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul (wa tatu kutoka kushoto) mbuzi waliochinjwa na kuhifadhiwa katika chumba chenye baridi kali kwa ajili ya kusafirishwa kuuzwa nje ya nchi. Gekul alitembelea kiwanda hicho kilichopo Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani Januari 11, 2021. Meneja Uzalishaji wa Kiwanda cha TANCHOICE, Selo Luwongo (wa ...

FETA WATAKIWA KUONGEZA KASI YA KUZALISHA WATAALAM KUIMARISHA UVUVI WA BAHARI KUU

Picha
  Na Mbaraka Kambona,   Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul ameitaka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kuongeza kasi ya kuzalisha Wataalam watakaokuwa na uwezo wa kuendesha Meli za uvuvi wa bahari kuu zitakazonunuliwa na Serikali ili kuongeza ajira na kukuza uchumi wa nchi kupitia uchumi wa bluu.   Gekul alitoa kauli hiyo alipofanya ziara katika ofisi za Wakala hiyo zilizopo Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani mwishoni mwa wiki.   Alisema kuwa mpango wa serikali katika miaka hii mitano chini ya uongozi wa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ni kununua meli nane zitakazotumika kwenye shughuli za uvuvi wa bahari kuu, hivyo ni muhimu kuongeza kasi ya kutoa wataalam ambao wataweza kuziendesha meli hizo pindi zitakapofika.                                     Aliongeza kuwa m...

GEKUL AMPA MKURUGENZI ILALA SIKU 7 KUMLIPA MKANDARASI

Picha
Na Mbaraka Kambona,   Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kuhakikisha kuwa ndani ya siku 7 anamlipa Mkandarasi anayejenga Machinjio ya Vingunguti shilingi bilioni 5 anazodai ili aweze kukamilisha ujenzi huo.   Gekul alitoa agizo hilo alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa machinjio hayo yaliyopo jijini Dar es Salaam Januari 8, 2021.   Alisema kuwa hali za machinjio nyingi kwa sasa sio nzuri, Wanyama wanachinjwa katika mazingira machafu na sio salama kwa walaji huku akisema machinjio hayo ya Vingunguti yatakuwa mkombozi kwa wananchi wa Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.   “Kwa hiyo Mkurugenzi hakikisha ndani ya siku 7 kuanzia leo tarehe 8 unamlipa Mkandarasi ili kazi hii ikamilike kama ambavyo Mhe. Rais, Dkt. John Magufuli alivyoagiza,” aliagiza Gekul   Gekul aliendelea kusisitiza kuwa kukamilika kwa ujenzi huo ni lazima uende sambamba na ununuzi wa magari kwa ajili ya kubebea nyama ...