Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2020

KONGAMANO LA NGOZI

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

TANZIA

Picha
 

SIKU YA UNYWAJI MAZIWA SHULENI

Picha
 

TANZIA

Picha
 

WATENDAJI WA SHAMBA LA LANGWILA WATAKIWA KUZINGATIA TARATIBU ZA UPANDAJI MALISHO.

Picha
Mkufunzi Mkuu wa Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Kejeri Gilla amesema ni vema kufanya kilimo cha malisho ya mifugo kwa mzunguko katika eneo moja kwa muda usiozidi miaka mitano ili kuzalisha kwa wingi na kupunguza kiwango cha magugu.   Dkt. Gilla alisema hayo wakati wa ziara ya watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye shamba la malisho la Langwila lililopo mkoani Mbeya walipotembelea kujionea shughuli zinazoendelea shambani hapo.   "Tusibuni namna ya kuotesha malisho bali twende kwa utaratibu unaotakiwa na hii itasaidia kupata muda wa kurutubisha ardhi na kupata malisho yaliyo bora," Alisema Dkt. Gilla   Hata hivyo Dkt. Gilla amesema ili kuweza kuwa na mbegu bora ni vyema kuvuna kwa wakati, kuchakata na kuhifadhiwa vizuri ili kuepuka kuoza kwa mbegu na kuwa na utaratibu wa kuhakikisha ubora wa mbegu za malisho.   Aidha, alishauri kupitia Idara ya Uendelezaji wa Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo isaidie kutengeneza duka la m...

MAFUNZO YA WAPANGA MADARAJA NA WAKAGUZI WA NGOZI YAFANYIKA KWA KANDA YA MASHARIKI

Picha
  Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo na Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura akifungua Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Profesa Elisante Ole Gabriel, katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam. Lengo la Mafunzo hayo ni Kuwajengea uwezo wa kiutendaji wakaguzi na wapanga madaraja ya Ngozi hapa nchini. (16.09.2020) Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi Kanda ya Mashariki wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufunguzi iliyokuwa ikitolewa na Mgeni rasmi hayupo katika picha. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam leo. (16.09.2020) Mshauri wa Masuala ya Ngozi hapa nchini, Bw. Emmanuel Muyinga akichangia hotuba ya ufunguzi wa Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi yaliyofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam. Bw. Muyinga ameipongeza Wizara kwa kufanya maamuzi ya uteuzi na usajili wa wakaguzi wa ...

SIKU YA UNYWAJI MAZIWA SHULENI

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

WARSHA YA KUKUSANYA MAONI YA MAANDALIZI YA MPANGO KAZI WA KITAIFA KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MWONGOZO WA HIARI WA KUENDELEZA SEKTA YA UVUVI MDOGO NCHINI YAFANYIKA MKOANI KIGOMA.

Picha
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Merisia Mparazo akifungua warsha ya kukusanya maoni ya Maandalizi ya Mpango Kazi wa Kitaifa kwa ajili ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini kwa muktadha wa kuhakikisha usalama wa chakula na kupunguza umasikini. Warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) mkoani Kigoma leo. (16.09.2020). Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Kitaifa cha Maandalizi ya Mpango wa Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa Kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini, Alhaj Yahya Mgawe akishiriki kusimamia zoezi la ukusanyaji wa maoni ya Mpango huo kwenye warsha iliyofanyika kwenye ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) mkoani Kigoma leo. (16.09.2020). Sehemu ya washiriki (wadau wa sekta ya Uvuvi) wa warsha ya kukusanya maoni ya Maandalizi ya Mpango Kazi wa Kitaifa kwa ajili ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini kwa muktadha wa kuh...

SIKU YA UNYWAJI MAZIWA SHULENI

Picha
 

WATAALAM WA MIFUGO WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO.

Picha
  Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Hezron Nonga amewasihi watumishi wa umma kuwa wazalendo kwa kutimiza wajibu wao na kuwatia moyo kwamba wapo hapo kwa makusudi ya Mwenyezi Mungu.   Prof. Nonga amesema hayo katika shamba la kuzalisha mitamba Saohill Mkoani Iringa wakati wa majadiliano ya namna watakavyoboresha na kufanya shamba hilo kuzalisha zaidi na kupata mafanikio makubwa.   "Kutotimiza yale mnayopaswa kufanya ni dhambi kama dhambi zingine na tukiendelea kuwaza hasi hatutakuwa wazalendo na wala hatutaendelea,” Alisema Prof. Nonga.   Prof. Nonga amesisitiza kutengenezwa kwa programu nzuri itakayosaidia kujua magonjwa ya mifugo ili kusaidia kutoeneza magonjwa kwa mifugo mingine na kuwa na utaratibu wa kuchanja mifugo kila mara.   "Tuwe na mikakati ya kutambua magonjwa ili kusaidia katika udhibiti wa magonjwa na vifo pamoja na uongozi mzuri ili kusaidia shamba kuendelea," alisisitiza Prof. Ezron Non...

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

SERIKALI YAZIDI KUWEKA MIKAKATI ILI WAFUGAJI WAWE NA NG’OMBE BORA.

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel amesema serikali imelenga kuhakikisha wafugaji nchini wanakuwa na ng’ombe bora, wenye kutoa nyama bora na maziwa mengi wanaopatikana kwa njia ya uhimilishaji (kumpatia ng’ombe mimba kwa njia ya mrija).   Prof. Gabriel amesema hayo katika Kijiji cha Matebete Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wakati akizindua rasmi kambi ya uhimilishaji katika kijiji hicho kwa wafugaji wa jamii ya kimasai na kuwataka waache kufuga kwa mazoea bali wawe na ng’ombe bora na wenye tija huku akiwalenga zaidi akinamama nchini kujikita katika ufugaji wa kisasa.   “Haya ni mafanikio makubwa niwaombe akinamama wengine Tanzania waige mfano wa kina mama wenzano wa jamii ya kimasai walioamua kufuga kisasa kwa kuwa na ng’ombe bora hatuwezi kuendelea kwenye ufugaji wa zamani lazima tufuge kisasa na uhimilishaji unafanyika kwa ng’ombe yeyote hata wa kienyeji.” Amesema Prof. Gabriel   Prof. Gabriel akizungumzia faida za uhim...

WAVUVI WADOGO KUINULIWA KIUCHUMI

Picha
  Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha Uandaaji wa Mpango wa utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuhakikisha Uvuvi Mdogo Unakuwa Endelevu, Alhaj Yahya Ibrahim Mgawe akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha ya Uandaaji wa Mpango huo iliyofanyika kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma. (15.09.2020) Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, Bw. Ferdinand Filimbi akifungua warsha ya uandaaji wa Mpango wa utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuhakikisha Uvuvi Mdogo Unakuwa Endelevu iliyofanyika kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma. (15.09.2020) Bi. Upendo Hamidu akiwasilisha mada kwenye warsha ya uandaaji wa Mpango wa utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa Kuhakikisha Uvuvi Mdogo Unakuwa Endelevu iliyofanyika kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma. (15.9.2020) Baadhi ya washiriki wa warsha ya uandaaji wa Mpango wa utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa Kuhakiki...

WATUMISHI WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WATEMBELEA OFISI ZA ZVC, TVLA MKOANI IRINGA.

Picha
Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakiongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Bw. Zachariyya Kera walifanya ziara ya kutembelea ofisi za Kituo cha Huduma za Mifugo cha Kanda (ZVC) na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Mkoani Iringa kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na ofisi hizo.   Akiongea wakati wa ziara hiyo kwenye ofisi za ZVC na TVLA zilizopo Mkoani Iringa, (14.09.2020), Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Zachariyya Kera alitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwataka wafanyakazi kujua haki zao za msingi na kufuatilia kwa wakati.   "Watumishi waelimishwe kuhusu haki zao na wapate stahiki zao kwa wakati," alisema Bw. Kera.   Katika ziara hiyo Watumishi hao walipata fursa pia ya kutembelea Kiwanda cha Maziwa cha ASAS kilichopo Mkoani humo na kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa katika kiwanda hicho.   Aidha, watumishi hao wa ZVC na TAVLA walitumia nafasi hiyo kumue...