Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakiongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Bw. Zachariyya Kera walifanya ziara ya kutembelea ofisi za Kituo cha Huduma za Mifugo cha Kanda (ZVC) na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Mkoani Iringa kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na ofisi hizo. Akiongea wakati wa ziara hiyo kwenye ofisi za ZVC na TVLA zilizopo Mkoani Iringa, (14.09.2020), Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Zachariyya Kera alitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwataka wafanyakazi kujua haki zao za msingi na kufuatilia kwa wakati. "Watumishi waelimishwe kuhusu haki zao na wapate stahiki zao kwa wakati," alisema Bw. Kera. Katika ziara hiyo Watumishi hao walipata fursa pia ya kutembelea Kiwanda cha Maziwa cha ASAS kilichopo Mkoani humo na kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa katika kiwanda hicho. Aidha, watumishi hao wa ZVC na TAVLA walitumia nafasi hiyo kumue...