Nav bar

Alhamisi, 17 Septemba 2020

MAFUNZO YA WAPANGA MADARAJA NA WAKAGUZI WA NGOZI YAFANYIKA KWA KANDA YA MASHARIKI

 

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo na Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura akifungua Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Profesa Elisante Ole Gabriel, katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam. Lengo la Mafunzo hayo ni Kuwajengea uwezo wa kiutendaji wakaguzi na wapanga madaraja ya Ngozi hapa nchini. (16.09.2020)

Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi Kanda ya Mashariki wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufunguzi iliyokuwa ikitolewa na Mgeni rasmi hayupo katika picha. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam leo. (16.09.2020)

Mshauri wa Masuala ya Ngozi hapa nchini, Bw. Emmanuel Muyinga akichangia hotuba ya ufunguzi wa Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi yaliyofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam. Bw. Muyinga ameipongeza Wizara kwa kufanya maamuzi ya uteuzi na usajili wa wakaguzi wa Ngozi. (16.09.2020)

Washiriki wa Mafunzo ya Wapanga Madaraja na Wakaguzi wa Ngozi kutoka Kanda ya Mashariki, Mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es Salaam na Tanga wakiwa katika Picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo na Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam leo. (16.09.2020)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni