WARSHA YA KUKUSANYA MAONI YA MAANDALIZI YA MPANGO KAZI WA KITAIFA KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MWONGOZO WA HIARI WA KUENDELEZA SEKTA YA UVUVI MDOGO NCHINI YAFANYIKA MKOANI KIGOMA.

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Merisia Mparazo akifungua warsha ya kukusanya maoni ya Maandalizi ya Mpango Kazi wa Kitaifa kwa ajili ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini kwa muktadha wa kuhakikisha usalama wa chakula na kupunguza umasikini. Warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) mkoani Kigoma leo. (16.09.2020).

Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Kitaifa cha Maandalizi ya Mpango wa Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa Kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini, Alhaj Yahya Mgawe akishiriki kusimamia zoezi la ukusanyaji wa maoni ya Mpango huo kwenye warsha iliyofanyika kwenye ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) mkoani Kigoma leo. (16.09.2020).

Sehemu ya washiriki (wadau wa sekta ya Uvuvi) wa warsha ya kukusanya maoni ya Maandalizi ya Mpango Kazi wa Kitaifa kwa ajili ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini kwa muktadha wa kuhakikisha usalama wa chakula na kupunguza umasikini wakifuatilia kwa makini maelekezo ya wataalam wa Uvuvi kwenye warsha iliyofanyika kwenye ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo Uvuvi (FETA) mkoani Kigoma leo. (16.09.2020).

Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Emanuela Mawoko (mwenye tisheti ya bluu), akisimamia zoezi la kukusanya maoni ya Maandalizi ya Mpango Kazi wa Kitaifa kwa ajili ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza Sekta ya Uvuvi Mdogo nchini kwa muktadha wa kuhakikisha usalama wa chakula na kupunguza umasikini. Warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) mkoani Kigoma leo. (16.09.2020).




 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO