DKT. MADELE AFUNGUA MAFUNZO YA MFUMO WA JINSIA GALS KUCHOCHEA UZALISHAJI WA MAZIWA

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, 𝐃𝐤𝐭. 𝐅𝐚𝐛𝐢𝐚𝐧 𝐌. 𝐌𝐚𝐝𝐞𝐥𝐞,leo Septemba Mosi, 2026  amefungua rasmi mafunzo ya siku sita ya kuwajengea uwezo Wakufunzi kuhusu 𝐌𝐟𝐮𝐦𝐨 𝐰𝐚 𝐉𝐢𝐧𝐬𝐢𝐚 𝐤𝐰𝐚 𝐕𝐢𝐭𝐞𝐧𝐝𝐨 (𝐆𝐀𝐋𝐒), yanayoratibiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP).

Mafunzo hayo yanayofanyika katika Hoteli ya Edema jijini Dodoma yamelenga kuwaandaa washiriki ambao ni Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka katika Halmashauri mbalimbali nchini kuwa Wakufunzi na Mawakala wa Mabadiliko watakaofikisha maarifa ya GALS hadi ngazi ya jamii, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na ushirikishwaji wa wanawake na wanaume katika kupanga, kuweka malengo ya kaya na biashara, kufanya maamuzi na kusimamia rasilimali kwa pamoja.⁣

Dkt. Madele amewataka washiriki kuhakikisha elimu hiyo inaleta mabadiliko ya kimtazamo, usawa na maamuzi ya pamoja katika kaya, ili ongezeko la uzalishaji wa maziwa utakaochangia kipato, lishe bora na maisha bora kwa familia za wafugaji.⁣

Kupitia mfumo wa GALS, Mradi wa C-SDTP unalenga kuzijengea kaya ushirikiano na maendeleo jumuishi na endelevu.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Dkt. Fabian Madele akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya siku sita kuhusu Mfumo wa Jinsia kwa Vitendo (GALS)kupitia Mradi wa C-SDTP yanayofanyika katika Hoteli ya Edema jijini Dodoma Septemba 01, 2026 .

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Dkt. Fabian Madele akizungumza na Washiriki wa Mafunzo kuhusu Mfumo wa Jinsia kwa Vitendo (GALS) wakati wa  kufungua mafunzo hayo  ya siku sita yanayofanyika katika Hoteli ya Edema jijini Dodoma, uzinduzi wake umefanyika leo Septemba 01, 2026 .

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko Bw. Edson Kilyemi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni Rasmi kuhutubia wakati wa ufunguzi wa Mfumo wa Jinsia kwa Vitendo (GALS) yaliyofanyika jijini Dodoma Hoteli ya Edema leo Septemba 01, 2026.

Mwakilishi wa Mratibu wa Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) Bw. Godluck Masawe akieleza hatua za utekeleza wa mradi huo na uendeshaji wa mafunzo hayo wakati wa ufunguzi wa Mfumo wa Jinsia kwa Vitendo (GALS) leo Septemba 01, 2026 .

Washiriki wa Mfumo wa Jinsia kwa Vitendo (GALS) wakisikiliza hotuba ya Mgeni Rasmi wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo uliofanyika Hoteli ya Edema jijini Dodoma leo Septemba 01, 2026.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

WATAALAMU WATAKIWA KUKUSANYA TAKWIMU SAHIHI ZA KITAFITI

TANZANIA DAIRY BOARD

SHAMBA LA KITULO KUWA KITOVU CHA NG’OMBE BORA WA MAZIWA NCHINI