Nav bar

Ijumaa, 19 Mei 2023

WAZIRI ULEGA AFANYA KIKAO NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WAFUGAJI TANZANIA

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (kulia) akimpa maagizo Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Bw. Evance Ntiyalunduwa  kwenye kikao cha  Waziri na Viongozi wa Chama cha wafugaji Tanzania (CCWT) (hawapo pichani) ambapo Viongozi hao walimtembelea Waziri kwa lengo la kujadiliana mambo mbalimbali yanayohusu ufugaji,  kikao hicho kilifanyika katika ofisi za wizara zilizopo jengo la NBC, Dodoma, Tarehe 10.05.2023.

Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Bw. Evance Ntiyalundura(wapili kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega(wakwanza kulia) kwenye kikao cha Waziri na viongozi wa chama cha Wafugaji Tanzania ambao walimtembelea Waziri kwa lengo la kujadiliana mambo mbalimbali yanayohusu Mifugo, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi za Wizara zilizopo jengo la NBC,  Jijini Dodoma.  Tarehe 10.05.2023.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akiongea jambo kwenye kikao na Wadau wa sekta ya Uvuvi kutoka Ziwa Tanganyika na Wataalamu wa Wizara. (Hawapo pichani) ambapo wadau hao waliwasilisha hoja zao na waziri amezipokea na kuagiza Wataalamu wa Wizara kumpatia taarifa za maboresho ya kiutafiti ambazo zilifanywa na TAFIRI ya mwaka 2020. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi za Wizara hiyo zilizopo,jengo la NBC, Dodoma. 10 Mei 2023.

Wadau wa sekta ya uvuvi kutoka ziwa Tanganyika na Wataalamu wa sekta Uvuvi kutoka Wizarani wakimsikilliza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) (wakwanza kulia)alipokuwa akitoa maelekezo 10.05.2023, kwenye kikao ambacho kilifanyika kwa lengo la kutoa hoja na kuzitolea ufafanua kuhusu Uvuvi  wa Ziwa Tanganyika, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi za Wizara zilizopo jengo la NBC, Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni