Nav bar

Ijumaa, 19 Mei 2023

KIKAO CHA USHIRIKIANO BAINA YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KIMEFANYIKA WILAYANI CHAMWINO MKOANI DODOMA

 

Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa, Brigedia Generali Hassan Mabena akiongea wakati wa kufungua kikao cha ushirikiano wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Jeshi la Kujenga Taifa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Jeshi hilo Wilayani Chamwino jijini Dodoma,  Mei 16,2023.


Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Angello Mwilawa akichangia hoja wakati wa kikao kifupi cha ushirikiano wa Wizara hiyo na jeshi la kujenga Taifa chanye lengo la kuwainua vijana kiuchumi kupitia sekta ya mifugo kilichofanyika kwenye Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma Mei 16,2023.


Mkurugenzi wa Kilimo, mifugo na Uvuvi kutoka Jeshi la Kujenga Taifa,  Kanali Peter Lushika akieleza  namna wanavyowajenga vijana wao kuweza kujikwamua kiuchumi na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wakati wa kikao kifupi kilichofanyika kwenye ukumbi wa jeshi hilo Chamwino jijini Dodoma,  Mei 16,2023


Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Daudi Mayeji akiongea wakati wa kufunga kikao cha ushirikiano wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Jeshi la kujenga Taifa chenye lengo la kuwainua vijana kiuchumi kupitia  Sekta ya Mifugo kilichofanyika Chamwino Jijini Dodoma, Mei 16,2023.



Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia  Generali Hassan Mabena (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na watendaji kutoka jeshi la kujenga Taifa mara baada ya kikao kifupi cha ushirikiano wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Jeshi na Kujenga Taifa katika suala zima la kuwainua vijana kupitia  Sekta ya Mifugo, kilichofanyika Chamwino jijini Dodoma  Mei 16,2023.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni