Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2022

NZUNDA WATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI NA ASASI BINAFSI

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. Tixon Nzunda amewataka vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali pamoja na Asasi binafsi ili kuweza kupambana na tatizo la ukosefu wa Ajira nchini Nzunda ameyasema hayo jana tarehe 29Juni 2022 Mjini Morogoro wakati wa hafla ya tathimini na ufungaji wa mradi wa uchumi kwa Vijana uliokuwa unafadhiliwa na shirika la Care International Tanzania. "Kupitia maradi huu wa Uchumi kwa Vijana, baadhi ya vijana waliobahatika kuingia katika Mradi huu wameweza kunufaika na Mafunzo ya ufugaji  na kujitegemea, sasa ni wajibu wao kuhakikisha elimu hii inawafikia vijana  wengine pamoja na makundi mengine". Alisema Nzunda.   Aidha, Nzunda aliongeza kwa kusema, “Ripoti ya mradi huu imeonyesha kwamba mpaka kufikia Mei 2022, vikundi 1040 viliundwa vikiwa na idadi kubwa ya Vijana wa Kike na wanawake kwa asilimia 64. Natoa pongezi za dhati kwa Halmashauri zote katika Mikoa ya Morogoro, Njombe na Mbeya kwani ndio waliosimamia ...

MAENEO YALIYOTENGWA KWA AJILI YA MALISHO YA MIFUGO YATAKIWA KUSAJILIWA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amesema kuwa maeneo yote ya malisho yaliyotengwa kwenye halmashauri yanatakiwa kusajiliwa na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.   Waziri Ndaki ameyasema hayo leo (26.06.2022) kwenye mkutano wa hadhara na wafugaji uliofanyika kwenye Kijiji cha Kongwa wilayani Morogoro ambapo aliwaeleza wafugaji hao kuwa halmashauri zikishatenga maeneo kwa ajili ya malisho zinatakiwa kuyawasilisha kwenye Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili yasajiliwe na kutangazwa kwenye gazeti la serikali.   "Halmashauri zinatakiwa mara baada ya kutenga maeneo ya malisho katika vijiji, zinatakiwa kuyawasilisha maeneo hayo Wizarani ili yasajiliwe na kutangazwa kwenye gazeti la serikali, kwa kufanya hivyo itakuwa ni vigumu mtu kubadilisha matumizi ya maeneo hayo kwa kuwa yatakuwa yanalindwa kisheria," alisema   Waziri Ndaki amewataka wafugaji hao kupanda malisho kwenye maeneo ambayo tayari yameshatengwa kwa ajili ya malisho badala ya kutegemea malisho ya asili peke...

NZUNDA AZINDUA MRADI WA UNENEPESHAJI, UZALISHAJI CHAKULA CHA MIFUGO

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda amezidua Mradi wa uandaaji wa lishe bora ya gharama nafuu kwa unenepeshaji wa Ng’ombe nchini uliofanyika kwenye ofisi za taasisi ya Utafiti wa Mifugo(TALIRI) kanda ya Mashariki jijini tanga Juni 23, 2022. Katika uzinduzi huo, Nzunda alisema kwamba mradi huo ni ushirikiano kati ya Wizara na COSTECH kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa nyama bora ambazo zinakwenda kuwa malighafi kwenye viwanda, lishe bora kwa wananchi, kupunguza pengo la vyakula vya mifugo kwa kutengeneza mashamba makubwa ya utafiti na mashamba darasa ya malisho ili wafugaji waweze kujifunza na kupata maeneo ya kufuga pamoja na  kutoa elimu kwa wafugaji, wasindikaji na wafanyabiashara wa mazao ya Mifugo. “Nimeona kazi nzuri mnazozifanya hasa kwenye kituo cha unenepeshaji wa Mifugo ya Nyama, ule ni mfano mzuri wa kuigwa, tunataka vituo hivyo viwe vingi zaidi, tuwawezeshe vijana wanaotoka vyuoni  mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri, tu...

WAZIRI NDAKI AKABIDHI INJINI ZA BOTI KWA AJILI YA WAVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amekabidhi injini za boti kwa ajili ya wavuvi katika Halmashauri za Wilaya za Pangani, Mtwara Mjini na Iringa.   Akizungumza kabla ya kukabidhi injini hizo leo (24.06.2022) Waziri Ndaki alisema kuwa Wizara imeendelea na utaratibu wake wa kuwawezesha wavuvi kwa kuwapatia vifaa vinakavyowasaidia kuongeza uwezo wa kuvua mazao ya uvuvi kwa wingi ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi hapa nchini.   “Injini za Boti tunazozikabidhi leo zina uwezo wa nguvu ya farasi 15 na tunazitoa kwenye Halmashauri za Wilaya za Pangani, Mtwara Mjini na Iringa ambapo kila Halmashauri itapata injini moja kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi kuongeza uwezo wao wa kuvua lakini pia kulinda rasilimali za uvuvi,” alisema   Waziri Ndaki amewasihi wavuvi kuhakikisha wanavitunza vifaa wanavyopatiwa na Wizara pamoja na Wadau wengine wa uvuvi na kuhakikisha wanavitumia kwa matumizi yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na ulinzi wa rasilimali za uvuvi. ...

VIJANA KUWEZESHWA UFUGAJI KIBIASHARA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ameitaka taasisi ya Utafiti wa Mifugo(TALIRI) na taasisi inayoshughulika na kilimo biashara(PASS) kupitia mradi wanaoutekeleza wa  kunenepesha mbuzi kuhakikisha vijana wengi wanapata ujuzi huo ili waweze kuwa na fursa pana ya ajira na kukuza uchumi wao . Ulega alitoa maelekezo hayo katika kikao kazi cha kupata taarifa ya utekelezaji wa mradi wa kunenepesha mbuzi unaotekelezwa kwa ushirikiano na taasisi hizo mbili kilichofanyika jijini Dodoma Juni 22, 2022. Alisema mradi huo ni lazima ujikite katika kuwasaidia vijana wengi kupata ujuzi wa kufuga kibiashara na kuwawekea mfumo mzuri utakaowasaidia kuwezeshwa kifedha ili wawe na mitaji ya kutosha kuendesha biashara ya mifugo. “Tunataka tutoe ajira kwa vijana, hivyo ni lazima kuwatengeneza vijana wengi watakaokuwa na ujuzi wa kunenepesha mifugo, sasa hivi wanaofanya unenepeshaji wapo na wanawezeshwa na benki zetu, lakini tunataka tupate vijana wengi zaidi watakaote...

TARILI, PASS WATAKIWA KUWA NA VIPAUMBELE VICHACHE

Picha
Na Mbaraka Kambona, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ameitaka taasisi ya Utafiti wa Mifugo(TALIRI) na taasisi inayoshughulika na kilimo biashara(PASS) kuhakikisha wanakuwa na  vipaumbele vichache watakavyoweza kutekeleza vyema ili mradi wa kunenepesha mbuzi wanaoutekeleza uweze kufikia malengo waliyokusudia. Ulega alitoa maelekezo hayo katika kikao kazi cha kupata taarifa ya utekelezaji wa mradi wa kunenepesha mbuzi unaotekelezwa kwa ushirikiano na taasisi hizo mbili kilichofanyika jijini Dodoma Juni 22, 2022. Alisema kwa sasa sekta ya mifugo inakabiliwa na changamoto kubwa ya malisho na uhaba wa malighafi zinazotokana na mifugo hivyo ni muhimu wakajikita katika kuzalisha malisho ili mifugo iwe na malisho ya kutosha wakati wote jambo litakalopelekea mifugo hiyo kuwa na uzito na kuwa na thamani sokoni. "Katika taarifa zenu nimewasikia hapa mmeeleza mambo mengi mnayotarajia kufanya kupitia mradi mnaotekeleza, ushauri wangu ni muhimu mkachagua mambo machache mtaka...

MIFUGO NA UVUVI YATUNUKIWA TUZO YA UTAWALA BORA

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Mifugo) imeshika nafasi ya pili kwenye tuzo za Utawala Bora zinazotolewa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kufanya vizuri kwenye upande wa utendaji bora katika utoaji wa huduma kwa watumishi na wananchi kwa mwaka wa fedha 2021/2022. Akipokea tuzo hiyo kwenye ofisi za Wizara zilizopo Mtumba Jijini Dodoma Juni 21, 2022 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Bwana Tixon Nzunda alisema kuwa tuzo hiyo imepatikana kutokana na ushirikiano mkubwa ulipo katika kufanya kazi kama timu, kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji kwa umma. “Nitumie fursa hii kuwashukuru watumishi wote wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwezesha tuzo hii kupatikana, tumefanyiwa tathimini kwenye eneo la utawala bora ambapo tumeshika nafasi ya pili, tuchukue hii kama changamoto kwa kufanya vizuri zaidi kwenye tuzo zingine,”  “Nishani hii ni kama chachu ya kufanya mabadiliko makubwa ili mwaka ujao tusiongoze tu kwenye ma...

KAMATI YA BUNGE YA KILIMO MIFUGO NA MAJI YAITAKA NAIC KUTOA ELIMU NA UHAMASISHAJI WA UHIMILISHAJI MBEGU BORA ZA MIFUGO

Picha
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Dkt. Christine Ishengoma amekitaka Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) kutoa elimu na uhamasishaji juu ya umuhimu na faida za kufanya uhimilishaji ili kuweza kupata mifugo na mazao bora ya mifugo. Maelekezo hayo yametolewa leo Juni 18, 2022 wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyotembelea kituo hicho pamoja na Chuo cha Mafunzo ya Mifugo Kampasi ya Tengeru mkoani Arusha ambapo walisema kuwa pamoja na kituo hicho kuwa cha muda mrefu na kuwa na matawi katika Kanda mbalimbali bado mwamko wa wafugaji katika kufanya uhimilishaji ni mdogo kutoka na wafugaji kukosa elimu sahihi juu ya suala hilo. Dkt. Ishengoma alisema kuwa kamati wametembelea na wameona teknolojia ya hali ya juu na yenye manufaa kwa wafugaji iliyopo katika kituo hicho lakini changamoto iliyopo ni mwitikio mdogo wa wafugaji katika kutumia teknolojia hiyo. “Tumeona kuanzia ukusanyaji wa mbegu na jinsi zinavyofanyiwa vipimo lakini pia tumeelezwa kila dume n...