NZUNDA WATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI NA ASASI BINAFSI
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. Tixon Nzunda amewataka vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali pamoja na Asasi binafsi ili kuweza kupambana na tatizo la ukosefu wa Ajira nchini Nzunda ameyasema hayo jana tarehe 29Juni 2022 Mjini Morogoro wakati wa hafla ya tathimini na ufungaji wa mradi wa uchumi kwa Vijana uliokuwa unafadhiliwa na shirika la Care International Tanzania. "Kupitia maradi huu wa Uchumi kwa Vijana, baadhi ya vijana waliobahatika kuingia katika Mradi huu wameweza kunufaika na Mafunzo ya ufugaji na kujitegemea, sasa ni wajibu wao kuhakikisha elimu hii inawafikia vijana wengine pamoja na makundi mengine". Alisema Nzunda. Aidha, Nzunda aliongeza kwa kusema, “Ripoti ya mradi huu imeonyesha kwamba mpaka kufikia Mei 2022, vikundi 1040 viliundwa vikiwa na idadi kubwa ya Vijana wa Kike na wanawake kwa asilimia 64. Natoa pongezi za dhati kwa Halmashauri zote katika Mikoa ya Morogoro, Njombe na Mbeya kwani ndio waliosimamia ...