KIKAO CHA MAFUNZO REJEA YA UFUGAJI SAMAKI KWA MAAFISA UGANI MJINI SONGEA
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Bw. Emmanuel Kisongo akifungua kikao cha mafunzo rejea ya ufugaji samaki kwa maafisa ugani (hawapo pichani) kutoka halmashauri za mikoa ya Mbeya, Songwe, Katavi, Kigoma na Ruvuma na kuwataka maafisa hao kuwa chachu ya kuhamasisha ufugaji samaki kwa wananchi. Mafunzo hayo yameandaliwa na Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na yanafanyika kwa siku nne Mjini Songea. (21.03.2022)* Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia aliyekaa) akiwa pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangyise (wa pili kutoka kushoto aliyekaa) wakisaini mkataba wa Makubaliano ya Kujenga, Kuanzisha na Kusimamia Kituo cha Taifa cha Ukuzaji Viumbe Maji bahari kati ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa halfla fupi ya uwekaji saini mkataba huo iliyofanyika kwenye Shule Kuu ya Sayansi na Teknolojia ya Uvuvi - Kampasi ya Kunduchi Jijini Dar es Salaam. (22.03.20...