Nav bar

Jumatano, 27 Aprili 2022

KIKAO CHA MAFUNZO REJEA YA UFUGAJI SAMAKI KWA MAAFISA UGANI MJINI SONGEA



Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Bw. Emmanuel Kisongo akifungua kikao cha mafunzo rejea ya ufugaji samaki kwa maafisa ugani (hawapo pichani) kutoka halmashauri za mikoa ya Mbeya, Songwe, Katavi, Kigoma na Ruvuma na kuwataka maafisa hao kuwa chachu ya kuhamasisha ufugaji samaki kwa wananchi. Mafunzo hayo yameandaliwa na Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na yanafanyika kwa siku nne Mjini Songea. (21.03.2022)* 

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia aliyekaa) akiwa pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangyise (wa pili kutoka kushoto aliyekaa) wakisaini mkataba wa Makubaliano ya Kujenga, Kuanzisha na Kusimamia Kituo cha Taifa cha Ukuzaji Viumbe Maji bahari kati ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa halfla fupi ya uwekaji saini mkataba huo iliyofanyika kwenye Shule Kuu ya Sayansi na Teknolojia ya Uvuvi - Kampasi ya Kunduchi Jijini Dar es Salaam. (22.03.2022)* 

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini Mkataba wa Makubaliano ya Kujenga, Kuanzisha na Kusimamia Kituo cha Taifa cha Ukuzaji Viumbe Maji bahari kati ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo amemtaka mkandarasi kumaliza kazi aliyopewa kwa wakati na kwa kuzingatia ubora. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye. Hafla hiyo imefanyika kwenye Shule Kuu ya Sayansi na Teknolojia ya Uvuvi - Kampasi ya Kunduchi Jijini Dar es Salaam. (22.03.2022)* 

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini Mkataba wa Makubaliano ya Kujenga, Kuanzisha na Kusimamia Kituo cha Taifa cha Ukuzaji Viumbe Maji bahari kati ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Hafla hiyo imefanyika kwenye Shule Kuu ya Sayansi na Teknolojia ya Uvuvi - Kampasi ya Kunduchi Jijini Dar es Salaam. (22.03.2022)*

Picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa saba kutoka kulia) na Viongozi na Wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Wizara ya Mifugo na Uvuvi mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya utiaji saini Mkataba wa Makubaliano ya Kujenga, Kuanzisha na Kusimamia Kituo cha Taifa cha Ukuzaji Viumbe Maji bahari kati ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na Wizara ya Mifugo na Uvuvi. (22.03.2022)* 


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni