Nav bar

Jumatatu, 25 Aprili 2022

UMUHIMU WA USHIRIKIANO BAINA YA VIONGOZI WA WILAYA YA MULEBA NA WAVUVI MKOANI KAGERA

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah akifafanua kwa wajumbe (hawapo pichani) katika kikao kilichomhusisha pia Mkuu wa Wilaya ya Muleba na maafisa wafawidhi wa Kanda ndogo za Bukoba na Muleba pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera, juu ya umuhimu wa ushirikiano baina ya viongozi wa Wilaya ya Muleba na wavuvi pamoja na kuhakikisha halmashauri ya wilaya hiyo inatoa vibali maeneo ya visiwani ili kuwaondolea kero wavuvi kusafiri mwendo mrefu kufuata vibali hivyo pamoja na wavuvi kuruhusiwa kuuza mazao ya uvuvi mahali popote nchini kwa kuzingatia sheria za nchi. (15.03.2022)* 

Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Emmanuel Bulayi (aliyesimama) akifafanua vifungu mbalimbali vya Sheria ya Uvuvi, kwa wajumbe katika kilichofanyika kwenye Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera, na kuwakutanisha Mkuu wa Wilaya ya Muleba na maafisa wafawidhi wa Kanda ndogo za Bukoba na Muleba pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama, ambapo lengo la kikao hicho ni kuondoa kero zinazoihusu sekta ya uvuvi katika wilaya hiyo. (15.03.2022)* 

 

Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Prof. Faustin Kamuzora, Mkuu wa wilaya ya Muleba Bw. Toba Nguvila, Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Emmanuel Bulayi, maafisa wafawidhi wa Kanda ndogo za Bukoba na Muleba pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama, mara baada ya kumaliza kikao kilichohusu namna ya kutatua kero mbalimbali zinazohusu sekta ya uvuvi. Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera. (15.03.2022)* 


 Akiwa Mkoani Geita katika Soko la Kimataifa la Kasenda lililopo Wilayani Chato, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah amezungumza na baadhi ya wadau wa sekta ya uvuvi na kuwajulisha namna uongozi wa wizara umefanya kikao na uongozi wa Mkoa wa Kagera na Wilaya ya Muleba na kukubaliana kuongeza ushirikiano na viongozi wa Mkoa wa Geita, Wilaya ya Chato pamoja na wadau wa sekta ya uvuvi ili wavuvi waweze kufanya shughuli zao bila kubughudhiwa na waruhusiwe kusafirisha mazao ya uvuvi popote nchini kwa kuzingatia sheria za nchi. (16.03.2022)* 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni