Nav bar

Jumatatu, 25 Aprili 2022

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO MIFUGO NA MAJI WAKIKAGUA UJENZI WA BWAWA LA KUNYWESHEA MAJI MIFUGO CHALINZE

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki akitoa ufafanuzi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji wakati ilipotembelea Kijiji cha Chamakweza wilayani Chalinze mkoa wa Pwani kukagua ujenzi wa Bwawa la kunyweshea Maji Mifugo. Kushoto ni Mhe. Dkt. Chistina Ishengoma ambaye ndio Mwenyekiti wa Kamati hiyo. (18.03.2022)* 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Viongozi, Wataalam na Wafugaji wakati walipokuwa wanatembelea kukagua Bwawa la kunyweshea Maji Mifugo la Chamakweza wilayani Chalinze mkoa Pwani. (18.03.2022)* 
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christina Ishengoma (wa pili kutoka kushoto) akijiridhisha kama maji yanatoka kwenye bomba wakati Kamati hiyo ilipofika kukagua ujenzi wa Bwawa la kunyweshea Maji Mifugo la Chamakweza wilayani Chalinze mkoa Pwani. Kulia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki. (18.03.2022)* 

*Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Dkt. Asimwe Rwiguza (kulia) akitoa maelezo mafupi juu ya ujenzi wa Bwawa la kunyweshea Maji Mifugo la Chamakweza wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ilipotembelea mradi huo. (18.03.2022)* 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni