Nav bar

Jumatano, 27 Aprili 2022

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI KUPOKEA MELI YA UVUVI YA WAWEKEZAJI JIJINI DAR ES SALAAM

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kushoto) akisalimiana na Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Suleiman Makame (wa pili kulia)baada ya kuwasili bandarini Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupokea meli ya Uvuvi ya Wawekezaji kutoka nchini Uhispania meli ambayo itakuwa inafanya kazi ya kuvua samaki katika bahari kuu. (21.03.2022)* 

 Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Suleiman Makame (kulia) akisalimiana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Christina Ishengoma (kushoto) wakati wakiwasili bandarini Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupokea meli ya Uvuvi ya Wawekezaji kutoka nchini Uhispania meli ambayo itakuwa inafanya kazi ya kuvua samaki katika bahari kuu. Katikati ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki. (21.03.2022)* 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) akimkabidhi Kibali cha kuvua nje ya mipaka ya Tanzania kwa Meneja wa Vyombo Vya Uvuvi vya Kampuni ya Albacora ya nchini Uhispania, Bw. Imanol Loinaz mara baada ya kuwasili kwa meli ya PACIFIC STAR itakayokuwa inafanya kazi ya uvuvi wa bahari kuu. Waziri Ndaki amekabidhi kibali hicho bandarini Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Suleiman Makame na kushoto ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega. (21.03.2022)*  

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Mhe. Suleimani Makame (kulia) akimkabidhi Leseni ya uvuvi wa bahari kuu kwa Meneja wa Vyombo Vya Uvuvi vya Kampuni ya Albacora ya nchini Uhispania, Bw. Imanol Loinaz mara baada ya kuwasili kwa meli ya PACIFIC STAR itakayokuwa inafanya kazi ya uvuvi wa bahari kuu. Waziri Masoud amekabidhi kibali hicho bandarini Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki na kushoto ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega. (21.03.2022)* 

Meli ya Uvuvi ya Wawekezaji wa Kampuni ya Albacora ya nchini Uhispania ikiwa imewasili kwenye bandari ya Dar es Salaam. (21.03.2022)* 


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni