Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2022

RUANGWA WAKABIDHIWA VIFARANGA VYA KUKU ZAIDI YA 3000

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa vifaranga vya kuku 3060 kwa vikundi  vya  wanawake Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi ikiwa ni katika utekelezaji wa sera ya kuwakwamua wananchi kiuchumi. Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaranga hivyo Februari 9, 2022 kwa vikundi vya kina mama,  Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Mafunzo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi,  Dkt Hassan Mruttu alisema mradi huo wa ufugaji kuku utakuwa wa shamba darasa. Alisema Wizara iliona ni vyema kuanza kutoa kuku kwa vikundi viwili (2) cha Alonga na Kichawana kama shamba darasa ambapo baada ya wiki 4 watatakiwa kusambaza katika vikundi vingine ili navyo viweze kufuga. "Sisi kama Wizara tunatekeleza ilani ya CCM tukiwa chini ya Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye ni mbunge wa hapa kwa hiyo katika kubuni namna ya kumkwamua mwanachi tukasema hatuwezi kumfikia mtu mmoja bali kwa kuanzisha mashamba darasa ambapo  vikundi vinakuwa vikijifunza na baada ya w...

WAFANYABIASHARA WA NJE WANAONUNUA MAZAO YA UVUVI KATIKA MIALO KUCHUKULIWA HATUA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Mwanza Waziri wa Mifugo na uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amewaagiza Watendaji wa wizara hiyo kwa kushirikiana na Watendaji wa Halmashauri kote nchini kuhakikisha wafanyabiashara wanaotoka nje ya nchi wananunua mazao ya uvuvi katika masoko yaliyopangwa na serikali na sio kwenye mialo kama baadhi yao wanavyofanya sasa ili kuepuka kupoteza mapato ya serikali yatokanayo na mazao hayo.  Waziri Ndaki alitoa agizo hilo wakati alipofanya kikao kilichohusisha watendaji wa wizara ya mifugo na uvuvi (sekta ya uvuvi), wafanyabiashara na wadau wa sekta hiyo kutoka halmashauri ya jiji la Mwanza Februari 2, 2022. Alitoa agizo hilo baada ya wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katika soko la Kimataifa la Kirumba kumweleza kuwa wapo baadhi ya wafanyabiashara kutoka mataifa ya jirani ambao wananunua mazao ya uvuvi katika mialo badala ya kwenda sokoni na kusababisha serikali kukosa mapato. “Kama kuna wafanyabiashara kutoka nje ya nchi wanakwenda kununua maza...

ULEGA ALIHAKIKISHIA BUNGE MAFANIKIO YA WAVUVI KWENYE UCHUMI WA BULUU*

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amelihakikishia bunge kuwa uchumi wa buluu kwa upande wa Tanzania bara utatekelezwa katika eneo kubwa zaidi kutokana na kuamua kuutekeleza katika vyanzo vyote vya maji vilivyopo nchini. Mhe. Ulega ameyasema hayo wakati akijibu swali la mmoja  wa wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ambaye alitaka kufahamu namna uchumi wa buluu unavyotekelezwa kwa upande wa Tanzania bara wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika  (03.02.2022) kwenye moja ya kumbi za Bunge jijini Dodoma Mhe. Ulega amesema kuwa upande wa Tanzania bara una vyanzo vingi zaidi vya maji ikilinganishwa na Zanzibar  na tayari Wizara yake imeanza hatua ya awali ya utekelezaji wa dhana hiyo kwa vitendo kwa   kuwaelimisha wavuvi juu ya fursa mbalimbali zilizopo kwenye mazao mbalimbali ya Uvuvi. “Mhe. Mwenyekiti hivi karibuni nilikuwa mkoani Tanga nikiwaelimisha wananchi juu ya fursa mbalimbali zilizopo kwenye uch...

SERIKALI YAELEZA MIKAKATI YA KUKABILIANA NA ATHARI ZA UKAME KWENYE MIFUGO

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, upande wa sekta ya Mifugo imebainisha mikakati iliyoiweka ili kukabiliana na athari za ukame ulioiathiri mifugo katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango kwa upande wa sekta hiyo, Mbaraka Stambuli wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya robo mwaka mbele ya kamati ya kudumu ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye kikao kilichofanyika  (02.02.2022) kwenye moja ya Kumbi za Bunge jijini Dodoma. “Mhe. Mwenyekiti moja ya mikakati tuliyoiweka kama Wizara ni kupeleka lita 2906 za dawa ili kuua kupe na mbung’o katika Halmashauri zilizoathirika zaidi lakini pia Wizara inajenga majosho 32 yenye thamani ya shilingi milioni 500 ili kuchochea uogeshaji kwa lengo la kudhibiti magonjwa kwenye maeneo yaliyoathirika zaidi” Amesema Stambuli. Stambuli amebainisha mkakati mwingine kuwa ni pamoja na Wizara yake  kushirikiana na Wizara ya Maji kuchimba visima virefu 6 katika Wilaya za Simanjiro, Same, ...

UZALISHAJI VIFARANGA VYA SAMAKI WAWEKEWA MKAKATI ENDELEVU

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeweka mikakati endelevu ya kuhakikisha inazalisha kwa wingi vifaranga vya samaki na kutoa elimu juu ya ufugaji wa samaki kwa wananchi ili kuongeza tija na kipato kwa Wafugaji na Taifa kwa ujumla. Mkurugenzi wa Ukuzaji Viumbe  Maji wa  Wizara hiyo , Dkt. Nazael  Madalla  alisema hayo Februari 1,2022  katika mafunzo rejea kwa maofisa ugani wa halmashauri za  mikoa ya Dar es Salaam, Tanga , Arusha , Pwani na Kilimanjaro yanayofanyika Mkoani Morogoro. Dkt. Madalla alisema mafunzo hayo yamelenga   kuhamasisha,  kuendeleza , kusimamia tasnia ya ukuzaji viumbe maji nchini na kuzalisha kwa tija . Aliendelea kusema kuwa vituo vinavyozalisha vifaranga wa samaki kwa Sasa ni vitatu ambavyo ni  Ruhila kilichopo  mkoa wa Ruvuma,  Mwamapuli  mkoani Tabora, na Kingolwira Morogoro. Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo,  mwaka 2020/2021 vituo hivyo  vitatu viliwezakuzalisha jumla ...

SERIKALI YAENDELEA KUWAJALI WAVUVI WADOGO

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi Sekta ya Uvuvi imeendelea kuwajali wavuvi wadogo kwa kuanzisha mradi wa kupunguza umasikini na kuongeza usalama wa chakula na lishe unaozingatia usawa wa kijinsia.   Hayo yamesemwa leo (03.02.2022) na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Sekta ya Uvuvi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Amos Machilika wakati akifungua Warsha ambayo imewashirikisha wadau mbalimbali kutoka katika taasisi za serikali, mashirika binafsi, Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na baadhi ya Halmashauri zenye shughuli za uvuvi. Warsha hiyo imefanyika katika ukumbi wa Hotel ya Edema Manispaa ya Morogoro.   Bw. Machilika amesema kuwa katika kutekeleza Mwongozo wa Hiari wa kuendeleza uvuvi mdogo, Wizara imeandaa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutekeleza mwongozo huo ambao ulipitishwa na wadau wote na sasa unakwenda kutekelezwa.   Lengo la kuwa na warsha hiyo ya wadau ni kuwakutanisha wadau na kuwafahamisha kuhusu...

WAFUGAJI KIBAHA WAKABIDHIWA DUME LA KISASA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe.  Abdallah Ulega amekabidhi Ng'ombe dume wa kisasa kwa wafugaji wa kijiji cha Miziguni kata ya Magindu, halmashauri ya Kibaha Vijijini, Mkoani Pwani kwa ajili ya kuboresha koosafu za mifugo yao. Akizungumza wakati wa kukabidhi dume hilo Januari 30, 2022 Naibu Waziri Ulega alisema kuwa Ng'ombe huyo ametolewa na mdau wa mifugo kutoka shamba la Canbe ikiwa ni katika jitihada za kuunga mkono Serikali ya awamu ya sita katika ufugaji wa kisasa na kuboresha Mifugo. Aliwataka wafugaji hao kuweka utaratibu mzuri kwa watu wote ambao wanahitaji mbegu ya dume hilo pamoja na kulitunza vizuri ili liweze kuhudumia majike mengi na kwa muda mrefu zaidi. "Nawaombeni sana dume hili litumike kwa ajili ya kuboreshea mifugo yetu, wekeni utaratibu mzuri wafugaji wote wanaotaka kupandisha majike yao wasikose fursa hiyo hapa, pia mlifanyie uchunguzi wa mara kwa mara lisije likapata ugonjwa wa kutupa mimba kwasababu atakuwa anahudumia mitamba mingi kwa hiy...