RUANGWA WAKABIDHIWA VIFARANGA VYA KUKU ZAIDI YA 3000
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa vifaranga vya kuku 3060 kwa vikundi vya wanawake Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi ikiwa ni katika utekelezaji wa sera ya kuwakwamua wananchi kiuchumi. Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaranga hivyo Februari 9, 2022 kwa vikundi vya kina mama, Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Mafunzo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt Hassan Mruttu alisema mradi huo wa ufugaji kuku utakuwa wa shamba darasa. Alisema Wizara iliona ni vyema kuanza kutoa kuku kwa vikundi viwili (2) cha Alonga na Kichawana kama shamba darasa ambapo baada ya wiki 4 watatakiwa kusambaza katika vikundi vingine ili navyo viweze kufuga. "Sisi kama Wizara tunatekeleza ilani ya CCM tukiwa chini ya Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye ni mbunge wa hapa kwa hiyo katika kubuni namna ya kumkwamua mwanachi tukasema hatuwezi kumfikia mtu mmoja bali kwa kuanzisha mashamba darasa ambapo vikundi vinakuwa vikijifunza na baada ya w...