TADB YAOMBWA KUENDELEA KUWASAIDIA WAVUVI NCHINI
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuwasaidia wavuvi katika mambo matatu ikiwemo kuwaondoa wavuvi kutoka kwenye uvuvi wa maji ya ndani na kuwapeleka kuvua kwenye maji ya Kitaifa kwa kutumia maboti ya kisasa badala ya mitumbwi na ngalawa. Ombi hilo lilitolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah alipokuwa akiongea na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Frank Mugeta, alisema uvuvi wa samaki katika ukanda wa bahari unaweza kuongezeka iwapo wataweza kuwasaidia wavuvi katika mambo mbalimbali. Pia, kuwaondoa wavuvi wadogo wadogo kutoka kwenye uvuvi wa maji ya ndani na kuwapeleka kuvua kwenye maji ya Kitaifa kwa kutumia maboti ya kisasa badala ya mitumbwi na ngalawa ambazo wengi wao bado wanazitumia. “Sasa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na sekta binafsi imeanza kutekeleza baadhi ya ...