Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2021

TADB YAOMBWA KUENDELEA KUWASAIDIA WAVUVI NCHINI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuwasaidia wavuvi   katika mambo matatu ikiwemo kuwaondoa wavuvi   kutoka kwenye uvuvi wa   maji ya ndani na kuwapeleka kuvua kwenye maji ya Kitaifa kwa kutumia maboti ya kisasa badala ya mitumbwi na ngalawa. Ombi hilo lilitolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah alipokuwa akiongea na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania  (TADB) wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Frank Mugeta,   alisema uvuvi wa samaki katika ukanda wa bahari unaweza kuongezeka iwapo wataweza kuwasaidia wavuvi katika mambo mbalimbali. Pia, kuwaondoa wavuvi wadogo wadogo kutoka kwenye uvuvi wa   maji ya ndani na kuwapeleka kuvua kwenye maji ya Kitaifa kwa kutumia maboti ya kisasa badala ya mitumbwi na ngalawa ambazo wengi wao bado wanazitumia. “Sasa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na sekta binafsi imeanza kutekeleza baadhi ya ...

WAKAGUZI WATAKIWA KISIMAMIA UBORA WA VYAKULA VYA MIFUGO

Picha
Serikali imewataka wakaguzi wa maeneo ya malisho na rasilimali za vyakula vya mifugo kuhakikisha mifugo inapatiwa vyakula vyenye ubora na stahiki ili kuondokana na madhara ya sumukuvu yanayoweza kuwaathiri walaji wa nyama, mayai, maziwa na bidhaa nyingine za mazao ya mifugo. Rai hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bw. Peter Nyakigera wakati akifungua mafunzo ya wakaguzi wa maeneo ya malisho na rasilimali za vyakula vya mifugo yaliyofanyika leo Agosti 12, 2021 katika ukumbi wa siasa ni kilimo Mkoani Iringa. Nyakigera alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa wakaguzi walio kwenye mamlaka za serikali za mitaa kwa vile yatasaidia kutatua changamoto ya ubora na viwango hafifu vya vyakula vya mifugo vinavyotumiwa na wafugaji walio wengi ambapo hata vifo vya baadhi ya mifugo vimesabishwa na kutumia baadhi ya rasilimali za vyakula vyenye sumukuvu. “Tanzania ni nchi ya pili kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo Afrika ikiwa na ng’ombe milioni 33.4, mbuzi milioni 21.29, k...

TANZANIA KUUZA NYAMA NCHINI SAUDIA ARABIA

Picha
  Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel amekutana na Ujumbe kutoka nchini Saudi Arabia kwa lengo la kuweka mazingira mazuri ya kufanya biashara ya nyama na nchi hiyo. Prof. Ole Gabriel alikutana na Ujumbe huo kutoka Saudi Arabia ulioongozwa na Mkaguzi,   Mamlaka ya Dawa na Chakula, Saudi Arabia, Ahmed Alhajouj jijini Dar es Salaam Agosti 7, 2021. Kwa mujibu wa Prof. Gabriel kabla ya kukutana nao, ujumbe huo ulipata fursa ya kukagua maeneo mbalimbali yanayohusika na uchakataji wa mazao ya mifugo ikiwemo Machinjio, Maabara na Shirika la Viwango Tanzania(TBS) ambapo kote wamejirisha na kutoa mapendekezo kadhaa ya kuboresha ili biashara hiyo iweze kufanyika kwa viwango vinavyohitajika na nchi hiyo.   Alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameielekeza Wizara hiyo kutafuta masoko nje ya nchi hivyo Wizara inaendelea kufanya jitihada ikiwemo hatua hiyo ya kutafuta soko katika nchi Saudi Arabia. ...

TUSISUBIRI KUSUKUMWA, TUFANYE KAZI-Prof. Ole Gabriel*

Picha
Katibu Mkuu wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka watumishi wote wa Sekta yake kutosubiri kushinikizwa ili watimize wajibu wao. Prof. Ole Gabriel ameyasema hayo leo (06.08.2021) alipokutana na watumishi hao kwa lengo la kutathmini mipango na malengo mbalimbali yanayotarajiwa kutekelezwa na sekta hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. “Tusisubiri kusukumwa, wakurugenzi na wakuu wa vitengo simamieni hilo na kuhakikisha watu wenu wa chini wanatimiza wajibu wao ipasavyo” amesema Prof. Ole Gabriel. Prof. Ole Gabriel amewaahidi watumishi hao kuwa katika mwaka huu wa fedha Sekta yake itaendelea kuboresha mazingira yao ya kazi na kuwaongezea morali ya kufanya kazi. “Watu wengi sana wanahamia kwenye Sekta yetu kwa hivi sasa na tunawakaribisha sana na wale wanaotaka kuhama walete maombi yao nami ntapitisha haraka sana ila nawakumbusha kuwa pindi wakitaka kurejea mchakato huo hautakuwa mwepesi” Amesisitiza Prof. Ole Gabriel. Katika hatua nyingine Prof. Ole ...

SERIKALI YAOMBWA KUSITISHA UCHINJAJI WA PUNDA SHINYANGA.

Picha
Serikali imeombwa kusitisha uchinjaji na uuzaji wa ngozi na malighafi zitokanazo na punda katika machinjio ya Shinyanga na kuwachukulia hatua watu wote waliobainika kukiuka haki za wanyama. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Shirika la Ulinzi na Utetezi wa haki na Ustawi wa Wanyama Arusha (ASPA) Bw. Livingstone Masija leo Agosti 6, 2021 Jijini Dodoma mbele ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel baada ya ukaguzi uliofanyika juni 20 mwaka huu na kubaini ukiukwaji mkubwa wa haki za mnyama punda kwa kuwafanyiwa mateso makubwa. Alisema, miongoni wa vitendo vinavyofanyika ni pamoja na kuwakosesha malisho kwa muda mrefu, kuchinja punda walio na mimba, kuchinja punda wakati wengine wanawaangalia na kuwapiga na vitu vizito kichwani pindi mashine zimeharibika na kukaa na majeraha bila ya kutibiwa. “kwa sababu watu wako pale wameaminiwa na Serikali lakini namna ya utekelezaji wao wa majukumu ni shida, wameambiwa wasimamie punda wachinjwe 20 kwa siku  l...

WAFUGAJI KUNUFAIKA NA MBEGU BORA ZA MIFUGO YA ASILI*

Picha
  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki ametoa wito kwa wafugaji wa mifugo ya asili kuunga mkono mkakati wa uboreshaji kosaafu za mifugo  nchini ili kupata tija zaidi kwa taifa kwa kuwa koo za mifugo zinazopatikana hapa nchini ni nzuri. Waziri Ndaki amebainisha hayo leo (03.08.2021) jijini Dodoma wakati akizindua mpango mkakati wa uboreshaji kosaafu za mifugo nchini wenye lengo la kuhakikisha kosaafu hizo zinazopatikana katika Bara la Afrika na maeneo mengine duniani zinahifadhiwa na kudumishwa kwa ajili ya maendeleo ya nchi na raia wake. “Ilikuwa lazima mkakati uzinduliwe leo kuhakikisha yale yaliyosemwa kwenye Sera ya Mifugo mwaka 2006, sasa yanakamilishwa kwa sababu tunaweza kuboresha kosaafu ya mifugo lakini hatukuwa na mikakati ya namna sera hiyo inaweza kuboresha kosaafu ya mifugo yetu ya asili.” Amesema Mhe. Ndaki Aidha Waziri Ndaki amesema hapa nchini kuna mifugo ya aina nyingi na hizo zote ni kosaafu za mifugo ambazo zinatakiwa kulindwa kuhifadhiwa na ...

KATIBU MKUU, WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI, (MIFUGO) PROF. ELISANTE OLE GABRIEL VISIWANI ZANZIBAR.

Picha
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akiongea na  Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo (Zanzibar), Dkt. Soud Hassan alipomtembelea Waziri huyo Ofisini kwake. Prof. Ole Gabriel alifanya ziara  Visiwani Zanzibar Agosti 2, 2021 kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano baina ya Sekta ya Mifugo, Tanzania bara na Sekta ya Mifugo,  Zanzibar, pia kufanya uhamasishaji wa ufugaji wa kisasa Visiwani humo.  Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akikagua moja kati ya aina mbalimbali za malisho ya mifugo zinazofanyiwa Utafiti  na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo, Zanzibar (ZALIRI) alipotembelea taasisi hiyo iliyopo Visiwani Zanzibar Agosti 2, 2021.    Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (wa kwanza kushoto) akiongea na Viongozi wa Kiwanda cha kuzalisha maziwa cha Azam Kilichopo Fumba, Visiwani Zanzibar. Prof. Ole Gabriel alifanya ziara k...

SERIKALI YAANZA KUSAKA MATOKEO CHANYA YA ZAO LA MWANI*

Picha
  Serikali imesema itaendelea kuwawezesha wakulima wa zao la mwani kwa vifaa pamoja na utaalamu ili waweze kuzalisha kwa wingi na ubora unaohitajika sokoni. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amesema hayo (01.08.2021) akiwa katika Kijiji cha Zingibari kilichopo Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga, wakati akitoa vifaa vyenye thamani ya Shilingi Milioni Nne kwa ajili ya kilimo cha mwani kwa vikundi vitatu vya wakulima wa zao hilo na kufafanua kuwa serikali itaendelea kutoa bure vifaa hivyo kwa wakulima wa mwani katika mwambao wa pwani ya Bahari ya Hindi ili kuhakikisha zao hilo linalimwa kwa wingi nchini. Akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Tanga, Mhe. Ndaki amesema kutokana na zao la mwani kuwa la kiuchumi kwa wananchi wa mwambao wa pwani ya Bahari ya Hindi, serikali imeanza kuweka mazingira mazuri ya uwezeshaji na kutafuta masoko ya uhakika ili wakulima waweze kunufaika kiuchumi. "Huu msaada wa vifaa kwa ajili ya kilimo utafika katika maeneo yote yenye uzal...

BODI YA NYAMA YATAKIWA KUANZISHA MFUMO WA KUWATAMBUA WANENEPESHAJI MIFUGO

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Abdallah Ulega ameiagiza Bodi ya Nyama nchini kuanzisha mfumo utakaosaidia wafugaji kunenepesha mifugo yao ili waweze kunufaika zaidi na fulsa za masoko ya ndani na nje ya nchi kwani mahitaji ya nyama ni makubwa.   Amesema hayo wakati akizungumza katika mkutano maalumu na wafugaji wa kienyeji, wafugaji wa kisasa pamoja na taasisi wezeshi za wafugaji wafuge kibiashara ili waweze kutoshereza soko la ndani na soko kubwa la nje ya nchi katika ukumbi wa Mvuvi house jijini Dar es salaam.   Mheshimiwa Ulega alisema elimu ya kutosha iendelee kutolewa ili kuwajengea uwezo wa kunenepesha mifugo yao hata wafugaji wa kienyeji katika ng’ombe, mbuzi na kondoo wao wa asili maana taifa limepata fulsa kubwa huko katika nchi za uarabuni hivyo mahitaji ya nyama ni makubwa.   Alisema katika halmashauri zote nchini wafugaji wa fundishwe namna moja ya kunenepesha na kuzalisha kwa wingi mifugo yao huku wakijua soko la ndani na nje ya nchi l...

KATIBU MKUU SEKTA YA UVUVI DKT. RASHID TAMATAMAH AFANYA MAZUNGUMZO NA WASHAURI KUTOKA AGRONOMOS SIN FRONTERAS FOUNDATION.

Picha
  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washauri kutoka Agronomos Sin Fronteras Foundation, wa pili kutoka kulia ni Dkt. Miguel Salvo Mendivil, wa  pili kutoka kushoto ni Bw. Klaus Poppe na watumishi wa Sekta ya Uvuvi  mara baada ya kufanya mazungumzo ofisini kwake leo 02/08/2021 Mtumba Jijini Dodoma, lengo likiwa ni kusaidia kuweza kupata  msaada kutoka  Serikali ya Spain kupitia mfuko wao unaojulikana kama COVID - 19 Recovery Fund, Aidha miradi iliyopendekezwa kuwasilishwa kwa ajili ya msaada huo  ni pamoja na ujenzi wa kiwanda cha kuchakata Mazao ya Uvuvi kupitia Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), kuangalia uwingi  wa samaki katika ukanda wa uchumi wa Bahari kuu, kufanya ubia na makampuni ya Spain katika Uvuvi wa Bahari kuu kupitia TAFICO na kuingiza masuala ya ufugaji viumbe maji katika mradi wa Kilimo unaotarajiwa kuanzishwa Mkoani Iringa.