Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2021

SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA AAT

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amewaeleza viongozi wa Chama cha Ukuzaji Viumbe Maji Tanzania (AAT) kuendelea kushirikiana na serikali ili kuongeza uzalishaji wa viumbe hao.   Waziri Ndaki ameyasema hayo leo (27.07.2021) ofisini kwake jijini Dodoma wakati alipotembelewa na viongozi wa AAT waliokuwa na lengo la kujitambulisha na kumuelezea mpango mkakati wao wa miaka mitano pamoja na namna walivyojipanga kushirikiana na serikali katika kufanikisha malengo yaliyowekwa na wizara.   Wizara inayo malengo ya kuongeza uzalishaji katika eneo la ukuzaji viumbe maji ili kuhakikisha uzalishaji huu una kuwa sawa na ule wa maji ya asili. Kwa kufanya hivi uzalishaji wa samaki hapa nchini utakuwa umeongezeka na hivyo kusaidia kukuza uchumi kupitia sekta ya uvuvi.   Aidha, amewaeleza viongozi hao kuwa wizara itaendelea kushirikiana na AAT katika kazi wanayoifanya kwa kuwa malengo ya serikali ni kushirikiana na sekta binafsi katika kukuza uchumi kupitia sekta ya uvuvi, huku...

NARCO YAELEKEZWA KUIPATIA KITALU KAMPUNI YA CHOBO

Picha
NARCO YAELEKEZWA KUIPATIA KITALU KAMPUNI YA CHOBO   Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki ameielekeza Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kuipatia Kampuni ya Chobo Kitalu Mbadala katika eneo la Mradi wa Mwisa II lililopo Wilayani Muleba, Mkoani Kagera baada ya kuchelewa kuendeleza Kitalu cha awali alichopewa katika Ranchi ya Mabale na kupelekea wawekezaji wengine kutumia eneo hilo.   Ndaki alitoa agizo hilo alipokutana na mwekezaji huyo jijini Dodoma Julai 27, 2021 na kukubaliana kuwa Wizara itampatia eneo lingine katika mradi wa Mwisa II ili aweze kuendeleza uwekezaji katika sekta ya mifugo.   Kufuatia makubaliano hayo, Waziri Ndaki ameielekeza NARCO kushughulikia jambo hilo kwa haraka ili mwekezaji huyo aweze kuendelea na shughuli zake za uwekezaji nchini.   “Kama nilivyosema sisi tuko tayari kushirikiana na Chobo pamoja na wawekezaji wengine kwa lengo la kuongeza tija kwenye sekta ya mifugo ili kutimiza malengo ya Tanzania ya Viwanda,” alisema N...

WATENDAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI WAWEKWA KITIMOTO

Picha
Na Mbaraka Kambona, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka Watendaji wanaofanya kazi ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali katika Minada, Mialo na Vituo vya Ukaguzi kufanya kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu huku akionya kuwa hawataweza kuendelea kuwa na Mtendaji atakayejihusisha na vitendo vinavyosababisha upotevu wa mapato ya Serikali. Waziri Ndaki aliyasema hayo katika kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa mwaka uliopita na kuweka malengo mapya ya ukusanyaji mapato kwa mwaka 2021/ 2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021. Akiongea na Watendaji hao aliwaeleza bayana kuwa ili waweze kufikia malengo ya kukusanya Shilingi Bilioni 90 walizojiwekea kukusanya kwa mwaka huu wa fedha ni lazima wafanye kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu kinyume na hapo hawatafanikiwa kufikia malengo. "Katika kipindi ambacho nimekuwa hapa Wizarani nimepata taarifa nyingi kuhusu baadhi yenu kujihusisha na vitendo vya upotevu wa mapato, acheni kufanya hivyo kwa sa...

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIFO VYA SAMAKI ENEO LA FUKWE YA BAHARI YA HINDI MKOANI DAR ES SALAAM

Picha
 

NDAKI ATOA SOMO KWA VIONGOZI, WATENDAJI WA WIZARA YAKE.

Picha
·   Ulega asisitiza sheria ya mabondo na sera ya kopa mbuzi lipa mbuzi  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka viongozi  wa Wizara hiyo kufanya kazi bila woga na kuwatengenezea mazingira rafiki ya utendaji kazi watumishi walio chini yao. Ndaki ameyasema hayo leo (19.07.2021) kwenye Ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Magufuli eneo la Mtumba jijini Dodoma wakati wa kikao baina yake na viongozi wa idara, vitengo na wakuu wa taasisi zote zilizopo chini ya wizara hiyo ambapo amewasisitiza kudumisha ushirikiano baina yao na watumishi waliopo chini yao. “Niwaombe viongozi wote mliopo hapa, ondoeni hofu wakati wote wa utendaji kazi wenu kwa sababu mimi sipo upande wa mtu yoyote hapa hata nikikupa kazi ifanye bila kuhofia labda naweza kuwa nimekupa kama kipimo flani” Amesema Ndaki. Aidha Ndaki amewataka viongozi hao kutowalinganisha watumishi waliopo chini yao wakati wa utekelezaji wa majukumu mbalimbali kwa kuwa   uwezo wa mtumishi mmoja hauwezi kufa...

MKAKATI WA KOPA MBUZI LIPA MBUZI KUANZA, CHANJO ZA MIFUGO ZATAKIWA VIJIJINI

Picha
Na. Edward Kondela Serikali imesema Ranchi ya mifugo ya Mkata iliyopo Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro itakuwa sehemu ya kuzalisha mbuzi kwa wingi kwa ajili ya mkakati wa kopa mbuzi lipa mbuzi ambao unatarajia kuanza hivi karibuni lengo likiwa ni kuwa na mbuzi wa kutosha kwa ajili ya soko la nje ya nchi. Akizungumza na uongozi wa ranchi na Wilaya ya Kilosa, wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja katika Ranchi ya Mkata, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalllah Ulega amesema ni muhimu kuangalia namna bora ya kufanya ufugaji wa kibiashara katika ranchi hiyo. Amesema serikali imechagua Ranchi ya Mkata kuwa kituo cha kuzalisha mbuzi kwa wingi ambacho watakuwa wanasambaza katika maeneo mbalimbali nchini. "Tutakayempa tutataka tujue yupo wapi na ana mbuzi wangapi ili tuwatambue na tuwaingize katika mfumo wetu wa takwimu za kibiashara ili iwapo tunapata mteja wa kilo 50 kwa mwezi kweli tuwe na uhakika wa kupata kilo hizo 50 kwa mwezi.” Amesema Mhe. Ulega Kutokana na mkakati huo wa k...

TANZANIA YAKATAA NYONGEZA YA RUZUKU KWENYE UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki leo (15.07.2021) amekataa nyongeza ya ruzuku kwenye shughuli za uvuvi ambapo amesema kuwa hatua hiyo itawawekea mazingira magumu wavuvi waliopo hapa nchini kutokana na kutokuwa na miundombinu ya kisasa ya kufanya shughuli hizo hasa katika eneo la bahari kuu ikilinganishwa na makampuni yanayotoka nje ya nchi. Ndaki ameyasema hayo alipokuwa akiwasilisha taarifa ya wizara yake  kwenye mkutano wa kamati ya majadiliano ya biashara (TNC) ngazi ya mawaziri ambao ulikuwa ukijadili mkataba wa  kuondoa  ruzuku  katika shughuli za uvuvi ambapo amesema kuwa kwa hivi sasa Tanzania bado haijapiga hatua kubwa kwenye uvuvi wa bahari kuu hivyo ongezeko hilo la ruzuku litatoa fursa nzuri zaidi kwa makampuni ya uvuvi ya yaliyopo kwenye nchi zilizoendelea. “Kwanza sisi bado hatujaanza kutoa ruzuku kwa wavuvi wetu lakini pia makampuni haya kutoka nje yakipata ruzuku hiyo yatakwenda kuvua mahali popote kwenye samaki na kwa kuwa wao wana nyenzo za ...

MAZUNGUMZO YA UBORESHAJI WA TAFITI KATIKA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UVUVI

Picha
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uvuvi Bw. Stephen Lukanga  amesisitiza uvuvi endelevu ili kuleta faida za kiuchumi kwa Taifa na kwa Wananchi walio Katika mnyororo wa thamani. Lukanga amesema hayo leo 15.07.2021 kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi wakati wa ufunguzi wa warsha ya Mazungumzo juu ya matumizi ya Utafiti Katika kufanya maamuzi ya Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi (science- management Dilogue) uliofanyika Katika Ukumbi wa Mkapa Jijini Dodoma. Amesema Serikali kupitia Idara za Maendeleo ya Uvuvi imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa Uvuvi Katika Bahari ya Hindi unakuwa endelevu na wa manufaa zaidi . Bw. Lukanga alieleza kuwa , Serikali ilisaini Barua ya makubalianao na Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa chini ya mpango wa EAF - Nansen kutekeleza Mradi mdogo wa Utekelezaji wa mpango wa Usimamizi wa Samaki wanaopatikana Katika tabaka la juu la maji Katika Ukanda wa Bahari ya hindi. “Lengo la Mradi ni kusaidia Utekelezaji wa mpango wa Usimamizi wa samaki wanao...

ULEGA ATAKA SEKTA YA MIFUGO KUJIENDESHA KIBIASHARA

Picha
Na. Edward Kondela Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega ameagiza shamba la malisho ya mifugo lililopo Vikuge Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani, kujiendesha kibiashara na kusambaza mbegu za malisho kutoka nchini China ijulikanayo kama JUNCAO maeneo mbalimbali nchini kwa kuwa ina sifa ya kustahimili sehemu yenye ukame ili wafugaji wapande malisho hayo. Wakati akihitimisha ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo (13.07.2021) Naibu Waziri Ulega, amesema hayo wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya shamba hilo na kumuagiza Katibu Mkuu anayeshugulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kuhakikisha aina mpya ya malisho hayo inasambazwa na kusimamia vyema ili mradi huo uweze kuwa na tija kwa taifa hususan kwa wafugaji vijijini. Mhe. Ulega amesema mbegu za malisho ya JUNCAO zisambazwe kuanzia ngazi ya mikoa wilaya hadi vijiji lengo likiwa kudhibiti mifugo na wafugaji kuhamahama kutafuta malisho. Amefafanua kuwa hataki kuona mambo yanayoanzishwa kwa ajili ya kunufaisha wananchi ...

NDAKI AAGIZA ULINZI KUWEKWA KWENYE SHAMBA LA UZALISHAJI MIFUGO - MABUKI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki ameagiza eneo la shamba la uzalishaji mifugo lililopo wilayani Misungwi mkoani Mwanza kulindwa na Suma JKT, Polisi pamoja na kujengewa fensi (uzio) ili kuimarisha ulinzi na usalama wa eneo hilo.   Hii ni baada ya Waziri huyo kufanya ziara jana ya kutembelea shamba la Mabuki pamoja na taasisi zilizomo ndani yake ambapo alielezwa kuwepo kwa uchungaji haramu na uchomaji moto pamoja na tishio la usalama kwa wanafunzi na watumishi katika shamaba hilo.   Ndaki amesema,eneo hilo ni kubwa na lipo wazi kwa hali hiyo  siyo salama kila mtu anaweza kuingia na kufanya jambo lolote hivyo waangalie uwezekano wa kuweka fensi ili mtu atakaye bomoa na kuingia itakuwa rahisi kumdhibiti.   Amesema,eneo hilo linapaswa kulindwa na Suma JKT,hivyo alimuagiza Mkurugenzi wa Utafiti ,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya  Mifugo na Uvuvi Dkt.Angello Mwilawa pamoja na uongozi wa kituo hicho kukaa pamoja na kuangalia ni walinzi wa ngapi wana...

SEKTA YA UVUVI KUFANYA MAPITIO YA BAADHI YA SHERIA NA KANUNI – MHE. NDAKI

Picha
Sekta ya Uvuvi imepanga kufanya mapitio ya baadhi ya sheria na kanuni za uvuvi ili ziweze kuendana na mazingira ya sasa.   Haya yamesemwa (13.07.2021) na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki wakati alipozungumza na wadau wa sekta ya uvuvi wa mkoa wa Kagera kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.   Waziri Ndaki alisema kuwa kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa wadau kuwa baadhi ya sheria na kanuni za uvuvi zimekuwa kikwazo katika utekelezaji wa shughuli zao. Hivyo wizara imeona ni muda muafaka kufanya mapitio ya baadhi ya sheria na kanuni hizo ili ziendane na mazingira ya sasa na kutokuwa kikwazo katika ufanyaji wa shughuli za uvuvi.   Lakini pamoja na mapitio hayo ya sheria na kanuni, wadau wa sekta ya uvuvi wametakiwa kuhakikisha wanafuata taratibu zote zilizopo katika utekelezaji wa shughuli zao za uvuvi na sio kusubiri mpaka wafuatiliwe. Aidha Waziri Ndaki aliwasihi wadau hao kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kwenye udh...

ZIARA YA NDAKI YAWA DAWA YA MIGOGORO MKOANI KAGERA

Picha
Ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Mashauri Ndaki mkoani Kagera imekuwa dawa ya utatuzi wa migogoro ya ardhi kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.   Waziri Ndaki amefanya ziara ya siku nne mkoani Kagera kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi iliyokuwepo katika maeneo yanayomilikiwa na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) katika Ranchi za Mabale wilayani Misenyi, Kagoma na Mwesa wilayani Muleba mkoani Kagera.   Akizungumza na uongozi wa mkoa wa Kagera ambapo pia alikuwepo Katibu Mkuu anayesimamia sekta ya mifugo baada ya kumaliza ziara yake, Waziri Ndaki alisema kuwa ziara hiyo imekuwa muhimu na yenye mafanikio makubwa kwake na kwa sekta ya mifugo kwani uwepo wa migogoro husababisha kupungua kwa kasi ya ukuaji wa sekta ya mifugo.   Katika ranchi hizo kulikuwa na wananchi ambao walikuwa wanakaa kwa muda mrefu na kufanya shughuli zao za maendeleo katika maeneo hayo. Hivyo kutokana na hilo kulikuwepo na migogoro kati ya wananchi hao na wawek...

ULEGA ATAKA KUMALIZIKA KWA MIGOGORO NA CHANJO KUFIKISHWA VIJIJINI

Picha
Na. Edward Kondela Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) ameusisitiza uongozi wa Mkoa wa Pwani kutumia mkakati wa uvunaji wa mifugo kama mkakati wa kumaliza migogoro ya wafugaji na wakulima pamoja na kuondokana na tatizo la uhaba wa malighafi katika viwanda vya kuchakata nyama mkoani humo. Naibu Waziri Ulega amesema hayo (12.07.2021) alipokutana na uongozi wa mkoa huo ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge, wakati akitoa taarifa ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani Pwani na kufafanua kuwa ni vyema uongozi huo ukafanya tathmini ya kina kwa kuunda kamati maalum ili kutafuta suluhu ya migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji mkoani humo. Amesema viongozi ndani ya mikoa yote nchini ni vyema wakaunda kamati maalum za wataalamu kwenda wilayani hadi vijijini ili kutafuta ufumbuzi wa haraka na kudumu wa kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji, ukiwemo mkakati wa kuhakikisha wafugaji wanavuna mifugo yao kwa kuuza katika viwanda vya kuchakat...