Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2021

WANAWAKE WANAOJIHUSISHA NA UVUVI WATAKIWA KUWA WABUNIFU

Picha
Wanawake wanaojihusisha na   shughuli za uvuvi wametakiwa kuwa wabunifu ikiwa ni pamoja na kujengeana uwezo Ili kukuza biashara zao huku wakikumbushwa    kujilinda dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi. Ushauri huo umetolewa (24.06.2021)   na Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mara, Bi. Neema Ibamba katika warsha ya siku tatu ya wadau hao Mjini Musoma Mkoani Mara. Ibamba amesema kuwa   biashara yoyote inahitaji ubunifu   na kwamba wadau hao kutoka Mikoa ya Kanda ya ziwa lazima waende na wakati. Aliongeza kuwa ubunifu unaotakiwa ni pamoja na kuwa na vifungashio vizuri   vya kisasa kwa ajili ya bidhaa zao pamoja na kuangalia fursa nyingine za masoko zinazowagusa. Aidha katika kukuza kipato cha familia, Ibamba amewataka wanawake kuendelea kushirikiana na waume zao badala ya kuwadharau kutokana na kipato wanachopata. "Biashara ama kupata kipato kisiwe kigezo cha kufanya dharau kwa wanaume wenu kwa kuwa mna pesa, hakikisheni kile mnachokipata m...

KAMATI YARIDHISHWA NA ELIMU YA UVUVI HARAMU BWAWA LA MTERA

Picha
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji imeridhishwa na elimu iliyotolewa kuhusu uvuvi haramu kwa wavuvi wa bwawa la Mtera.   Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dkt. Christine Ishengoma ameyasema hayo leo (19.06.2021) baada ya kamati kumaliza ziara yake kwenye kijiji cha Misisiri wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma na kijiji cha Mnadani wilaya ya Iringa ambapo walizungumza na wavuvi na wananchi wa maeneo hayo.   Dkt. Ishengoma amesema katika vijiji vyote walivyopita wamekuta wavuvi na wananchi kwa ujumla wanayo elimu kuhusu uvuvi haramu na wanashiriki katika kudhibiti kwa kukamata nyavu haramu na kuziteketeza.   Wavuvi wametakiwa kuendelea kudhibiti uvuvi haramu katika bwawa hilo ambalo kwa sasa samaki wamepungua katika baadhi ya maeneo kutokana na Uvuvi haramu.   Dkt. Ishengoma amewaahidi wananchi wa kijiji cha Mnadani kuwa atalifikisha tatizo la wingi wa viboko katika bwawa hilo kwa Waziri wa Maliasili na Utalii ili aweze kulishighulikia.   ...

TAASISI ZA BIMA NA ZA FEDHA ZATAKIWA KUWA MKOMBOZI WA WAFUGAJI NA WAVUVI

Picha
Taasisi za bima na za kifedha zimetakiwa kuwa mkombozi kwa wafugaji na wavuvi kwa kuhakikisha wanakuwa na uwezo wa kuwa na bima ya mifugo na samaki itakayowasaidia kuwa na ulinzi wa uwekezaji wao na kuweza kukopesheka.   Haya yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega leo Juni 17, 2021 wakati akifungua kikao cha Wadau wa Dawati la Sekta Binafsi ambalo lipo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye ukumbi mdogo wa wizara uliopo kwenye ofisi za NBC jijini Dodoma.   Ulega amesema kuwa wafugaji na wavuvi wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kutokopesheka kirahisi na taasisi za kifedha na hivyo kuwafanya washindwe kuitumia fursa ya mikopo ambayo ipo ili kukuza mitaji yao na hatimaye kuongeza mitaji na kipato pia.   “Kutokana na changamoto hii, wizara imeona ni vema kuwakutanisha wadau wanaohusika ili wote kwa pamoja tujadili tatizo nini na nini kifanyike ili tutakapotoka hapa tuwe na suluhisho ambalo litajibu tatizo la wafugaji na wakulima...

KIKAO CHA WADAU WA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
 

MAAFISA UVUVI 11 WAKABIDHIWA VITAMBULISHO VYA UKAGUZI WA MAZINGIRA

Picha
Maafisa Uvuvi kumi na moja (11) kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi wamekabidhiwa vitambulisho vitakavyowawezesha kufanya ukaguzi wa mazingira katika shughuli zote zinazofanyika katika maeneo ya uvuvi nchini.   Maafisa hao walikabidhiwa vitambulisho hivyo baada ya kupatiwa mafunzo ya ukaguzi wa mazingira na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) yaliyofanyika  Julai 20 hadi 22, 2020 jijini Dar es Salaam. Wakati akikabidhi vitambulisho hivyo, Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Bw. Magesa Bulayi katika tukio lililofanyika jijini Dodoma Julai 14, 2021, alisema kuwa anawakabidhi vitambulisho hivyo na ni imani yake kuwa  wataalamu hao  wa ukaguzi wataweza kusaidia kutatua vikwazo vinavyorudisha nyuma juhudi za Wizara katika kukabiliana na uharibifu wa mazingira katika maeneo ya uvuvi. Alisema sekta imekuwa ikikabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu wa mazingira unaotokana na shughuli mbalimbali za ki...

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE KILIMO, MIFUGO NA MAJI YAPEWA SEMINA KUHUSU NARCO

Picha
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji imepewa semina kuhusu Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kwa malengo ya kujua majukumu yake, muundo wake, utekelezaji wa bajeti, mafanikio, changamoto na mikakati ya kutatua changamoto hizo.   Kamati imepatiwa semina hiyo leo (11.06.2021) katika ukumbi wa Msekwa D uliopo ndani ya Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma ambapo viongozi wa Wizara waliongozwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega.   Akizungumza kuhusu semina hiyo Mhe. Ulega amesema kuwa wizara imeona ni wakati muafaka kufanya semina kuhusu NARCO ili wajumbe wa kamati hiyo waweze kuielewa na kutoa maoni yao ambayo yatasaidia sana katika kuhakikisha kampuni hiyo inaendelea kuimarika kwa kuongeza uzalishaji wa mitamba, nyama na kuzidi kuchangia kwenye pato la taifa.   Mhe. Ulega amesema kuwa Kampuni hiyo ya Ranchi za Taifa ilipita katika kipindi kigumu na hivyo kushindwa kujiendesha lakini kutokana na jitihada mbalimbali zilizofanywa na w...

MENEJA MACHINJIO YA DODOMA APEWA MIEZI 3 KUBORESHA MIUNDOMBINU

Picha
Na Mbaraka Kambona, Dodoma   Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega ametoa miezi mitatu (3) kwa Meneja wa Machinjio ya Dodoma, Victor Mwita kufanya maboresho ya miundombinu iliyopo katika machinjio hayo ili iweze kutoa huduma inayostahiki na kuchangia ipasavyo katika pato la taifa.   Waziri Ulega alitoa maelekezo hayo wakati alipofanya ziara ya kukagua machinjio hayo yaliyopo jijini Dodoma Juni 8, 2021 ambapo pamoja na mambo mengine alimtaka meneja huyo kutumia vyema mapato wanayokusanya ili kuboresha miundombinu ya machinjio hiyo.   “Natoa miezi mitatu (3) ya kuboresha miundombinu ya machinjio hii, na mimi nitakuwa nakuja hapa kila mwezi kuangalia ni maboresho gani mmeyafanya, madhumuni yetu machinjio hii iweze kutoa mchango unaohitajika kwa taifa,” alisema Ulega   Alisema kuwa lengo la Serikali ya awamu ya sita ni kuona machinjio hiyo inafanya kazi katika uwezo wake uliosimikwa ili mchango wa sekta ya mifugo katika pato la taifa uweze kuone...

SERIKALI KUFUTA KODI YA ONGEZEKO LA THAMANI KWENYE VIFAA VYA UVUVI

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalla Ulega amesema Serikali imefuta Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye vifaa vingi vya uvuvi ikiwemo injini za kupachika, nyuzi za kushonea nyavu, nyavu za uvuvi na vifungashio ili kuwasaidia wavuvi kupata zana za uvuvi kwa bei nafuu. Mhe. Ulega aliyasema hayo Juni 09, 2021, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti maalum, Mhe. Sylivia Sigula ambaye alitaka kufahamu mpango wa Serikali katika kuwawezesha wavuvi wa Ziwa Tanganyika wavue kisasa ili kupata kipato Zaidi na kutoa ajira kwa vijana. "Kupitia Sheria ya Fedha ya Mwaka 2011 na Sheria ya Mamlaka ya Mapato ya mwaka 2014, Serikali imefuta Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye vifaa vingi vya uvuvi ikiwemo injini za kupachika, nyuzi za kushonea nyavu, nyavu za uvuvi na vifungashio ili kuwasaidia wavuvi kupata zana za uvuvi kwa bei nafuu," alisema Mhe. Ulega Alisema kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ili wavuvi wapate mikopo ya masharti na riba nafuu kutoka k...

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA UVUVI BAHARI KUU - ULEGA

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema Serikali inaendelea na juhudi za Kuimarisha uvuvi wa bahari kuu kwa kufufua Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) ili kuiwezesha nchi kunufaika na rasilimali za uvuvi hususan zile zilizopo katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari na Bahari Kuu. Mhe. Ulega aliyasema hayo Juni 07, 2021 wakati akijbu swali la Mbunge wa Kawe, Mhe. Askofu Josephat Gwajima ambaye alitaka kufahamu mpango madhubuti wa kutumia Bahari kwa programu za uvuvi wa Bahari Kuu na michezo ya bahari ili kutengeneza ajira kwa vijana wa Jimbo la Kawe hasa ikizingatiwa nusu ya Jimbo hilo  lipo mwambao wa Bahari ya Hindi. Alisema hadi sasa Serikali ina mpango wa kununua meli tano (5) za uvuvi ambazo zitavua katika maji ya kitaifa, bahari kuu, pamoja na kutoa leseni kwa meli kubwa zinazomilikiwa na Sekta Binafsi.   Aliongeza kuwa Serikali ina mpango wa Kujenga Bandari ya Uvuvi katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi ambapo uwepo wa Bandari hiyo utawe...

SEKTA ZA MIFUGO TANZANIA BARA NA ZANZIBAR ZAIMARISHA USHIRIKIANO.

Picha
  Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kiutendaji katika ngazi za idara na taasisi zikiwemo Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Zanzibar (ZALIRI)  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Prof. Elisante Ole Gabriel alisema hayo wakati wa mapitio ya taarifa ya kikao cha wataalam wa sekta ya Mifugo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kilichofanyika Juni 04, 2021 Jijini Dar es salaam. Alisema utaandaliwa mkakati wa pamoja wa mawasiliano katika sekta hizo za pande mbili ili wadau pia watambue ushirikiano huo ambao umelenga kukuza uzalishaji katika sekta ya Mifugo hapa nchini. Alisema pamoja na mambo mengine wataangalia namna ya kuwepo kwa urahisi wa utekelezaji wa vibali vya mazao ya mifugo ili vibali ambavyo vimetolewa Zanzibar vitambulike bara na vilivyotolewa bara vitambulike Zanzibar. "U...