TAMATAMAH AFUNGUA MKUTANO WA WADAU KUHUSU MJADALA WA VIWANGO VYA MAZAO YA DAGAA NA MWANI
Serikali imesema ipo katika mchakato wa kutengeneza viwango vya kitaifa vya ubora na usalama wa mazao ya Mwani na Dagaa ili kuyapa mazao hayo fursa pana ya masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi. Hayo yalisemwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah alipokuwa akifungua mkutano wa Wadau kuhusu mjadala wa viwango vya mazao ya Dagaa na Mwani uliofanyika jijini Dar es Salaam Agosti 24, 2020. Dkt. Tamatamah alisema kuwa kutengenezwa na kuanzishwa kwa viwango vya kitaifa vya ubora na usalama wa mazao hayo ya uvuvi kutaimarisha na kukuza soko la kitaifa na kimataifa la bidhaa zinazotokana na mazao hayo ya uvuvi. “Mazao ya Dagaa na Mwani kwa muda mrefu yamekuwa hayana viwango vya ubora jambo ambalo limekuwa likifanya bidhaa hizo kutokutambulika katika soko la kimataifa ndio maana sasa serikali imeamua kutengeneza viwango vya ubora vya mazao ya uvuvi hasa Daagaa na Mwani ili yaweze kupata masoko yenye uhakika ndani na nje ya nchi,”alisema Dkt. Tamatamah Alisema ku...