Nav bar

Jumatano, 19 Agosti 2020

HABARI PICHA ZA MAONYESHO YA NANENANE KWENYE MIKOA YA SIMIYU, LINDI, ARUSHA, MBEYA, DODOMA, TAREHE 08/08/2020











Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto) akitoa maelezo kuhusu mradi wa "deep sea" kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) baada ya Waziri Mkuu kufika kwenye mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi muda mfupi uliopita kwenye Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu (08.08.2020). 

 


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akitoa maelezo kuhusu teknolojia ya uhimilishaji kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) baada ya Waziri Mkuu kufika kwenye mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi muda mfupi uliopita kwenye Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu (08.08.2020), Wa pili kutoka kulia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina. 

 


Kutoka Kulia Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah wakipata maelezo namna mradi wa "deep sea" unavyofanya kazi muda mfupi baada Mhe. Waziri Mkuu kufika hapo leo (08.08.2020) kwenye Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu. 


Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga akiwakabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah, Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani Dkt. Angelo Mwilawa wakipokea zawadi ya kombe baada ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kushika nafasi ya pili kwenye maonesho ya Kilimo (NANE NANE) kwa upande wa Taasisi za Serikali wakati wa kilele cha Maonesho hayo kitaifa Mkoani Simiyu  (08.08.2020) 


Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akimkabidhi zawadi ya Kombe Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa masuala ya Mifugo (TALIRI) Dkt. Eliggy Shirima baada ya taasisi hiyo kushika nafasi ya pili kwa upande wa taasisi zilizo chini ya Wizara wakati wa kilele cha Maonesho ya Kilimo (NANE NANE) kitaifa Mkoani Simiyu  (08.08.2020).

 


Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani Dkt. Angelo Mwilawa, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah wakifurahia zawadi ya Kombe walilokabidhiwa baada ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kushika nafasi ya pili kwenye maonesho ya Kilimo (NANE NANE) kwa upande wa Taasisi za Serikali wakati wa kilele cha Maonesho hayo kitaifa Mkoani Simiyu (08.08.2020)


LINDI


Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Melkidezeky Kody akitoa maelezo kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba wakati alipotembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini katika viwanja vya Ngongo - Manispaa ya Lindi. (08.08.2020) 

 



Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba akizungumza na mmoja wa wajasiriamali, Hadija Malibiche (aliyebeba mtoto) wakati alipotembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini katika viwanja vya Ngongo - Manispaa ya Lindi. (08.08.2020) 


ARUSHA


Afisa Mfawidhi kutoka kituo cha Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Nyumba ya Mungu Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Godbless Msuya (kushoto) akitoa maelezo juu ya nyavu zinazoruhusiwa na zisizoruhusiwa kwenye uvuvi kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha (08/08/2020) 


Daktari wa Mifugo kutoka Wakala ya Maabara ya Vetenari Tanzania (TVLA), Bw. Rowenya Mushi akitoa maelezo na kuelekeza namna ya kutumia darubini kwa wanafunzi wa shule ya msingi Maromboso waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane Mkoani Arusha. (08/08/2020) 


Afisa Mifugo kutoka Idara ya Uendelezaji wa Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Bw. Francis Ndumbaro akitoa maelezo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha (08/08/2020) 

 


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dr. Asimwe Rwiguza akijadili jambo na maafisa kutoka Wizara hiyo kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane Mkoani Arusha (08/08/2020) 

 


MBEYA

Naibu spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dr. Tulia Akson akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya maonyesho ya nanenane yaliyofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale mkoani Mbeya tarehe 08.08.2020

 


Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi kabla ya kufunga maadhimisho ya maonyesho ya nanenane ambapo leo ndio ilikua kilele cha madhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya John Mwakangale- Mbeya tarehe 08.08.2020. 

 

DODOMA


Mratibu wa Maonesho, banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bezia Rwongezibwa(katika) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi, Kampuni ya Rushu, Mabula Charles (aliyeshika Kombe) ambaye ndiye aliyeibuka Mshindi wa kwanza katika kundi la Paredi- Wafugaji wakubwa, Ngombe wa Nyama. Wengine wanaofurahia ushindi huo ni watumishi wa Wizara na Wafanyakazi wa Kampuni ya Rushu. Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekuwa Mshindi wa Pili katika Kundi la Wizara za sekta ya uchumi- uzalishaji katika kilele cha kusherehekea Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji- Nane Nane iliyofanyika kwenye Viwanja vya Nzuguni, Dodoma Agosti 8, 2020. 

 


 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya Watu Wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa (kulia) akikabidhi cheti cha Ushindi wa Pili katika kundi la Wizara za sekta ya uchumi-uzalishaji kwa Mratibu wa Maonesho, banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bezia Rwongezibwa (wa kwanza kushoto) katika kilele cha kusherehekea Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji- Nane Nane iliyofanyika katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma Agosti 8, 2020. Wa pili kutoka kushoto ni Afisa Uvuvi Mkuu, Ezra Mutagwaba. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ukuzaji Viumbe maji, Dkt. Imani Kapinga. 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni