Nav bar

Jumanne, 18 Agosti 2020

HABARI PICHA ZA MAONYESHO YA NANENANE KWENYE MIKOA YA DODOMA NA ARUSHA, TAREHE 07/08/2020

Mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya ndani, Mhe. George Simbachawene akiangalia mbegu bora za malisho ya wanyama zinazozalishwa na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo(TARILI) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Nzuguni, Kanda ya Kati, Dodoma Agosti 7, 2020. 


Afisa Mauzo, Kampuni ya Inas, Hussein Juma(kulia) akimkaribisha Mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. George Simbachawene kuonja vipande vya Nyama   vilivyokaushwa na kutafunwa kama kichangamsha mdomo alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Nzuguni, Kanda ya Kati, Dodoma Agosti 7, 2020. 

 


Mkuu wa Kitengo cha Uhimilishaji, Kanda ya Kati, Idara ya Uzalishaji na Masoko, Denis Sichwale(Kulia) akitoa maelezo kuhusu Uhimilishaji kwa Mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. George Simbachawene alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea kwenye Viwanja vya Nzuguni, Kanda ya Kati, Dodoma Agosti 7, 2020. 

 


 

Mratibu wa Maonesho, banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bezia Rwongezibwa (wa pili kulia) akimkaribisha Mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. George Simbachawene (kushoto, aliyevaa kaunda suti) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Kanda ya Kati, Dodoma leo Agosti 7, 2020. 


ARUSHA


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna Mgwira akipata maelezo ya ufugaji wa sungura kutoka kwa mtaalam wa sungura wa kampuni ya SAORE, Bw. Isack John kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (07/08/2020) 

 


Mkufunzi kutoka Wakala ya vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA), Bw. Ijumaa Bakari akitoa maelezo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (07/08/2020) 

 


Msambazaji wa madini ya Mifugo kutoka kampuni ya usambazaji wa madini (JOSERA), Bw.  Elirehema Laizer akitoa elimu ya madini na umuhimu wake kwa Mifugo kwa wadau waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (07/08/2020) 


Daktari wa Mifugo kutoka kituo cha Uhimilishaji NAIC, Bw. Elibariki Njiku akitoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Suye waliotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye maonyesho ya nanenane yanayoendelea kwenye kiwanja cha Themi Mkoani Arusha. (07/08/2020) 

 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni