Nav bar

Alhamisi, 27 Agosti 2020

ZIARA YA MAKATIBU WAKUU WILAYANI MAFIA.

 

Kaimu Muhifadhi Mfawidhi, Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU), Bw. Amin Abdallah (kushoto) akisoma taarifa ya utekelezaji wa Majukumu ya taasisi hiyo kwa Makatibu Wakuu kutoka Wizara nne tofauti walipotembelea taasisi hiyo. Kulia ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah. (22.08.2020)

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia) akieleza jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Bw. Shaib Nnunduma (kushoto) wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu na Mkuu huyo wa Wilaya pamoja na kamati yake ya ulinzi na usalama ya Wilaya kilichofanyika katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya. (22.08.2020)

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (Kulia) akiongea na Watumishi wa Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) (hawapo pichani) alipotembelea Taasisi hiyo iliyopo katika eneo la Hifadhi ya Bahari ya Kisiwa cha Mafia. Kushoto ni Kaimu Muhifadhi Mfawidhi, Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU), Amin Abdallah. (22.08.2020)

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (Kulia) akiongea na Watumishi wa Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) (hawapo pichani) alipotembelea Taasisi hiyo iliyopo katika eneo la Hifadhi ya Bahari ya Kisiwa cha Mafia. Kushoto ni Kaimu Muhifadhi Mfawidhi, Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU), Amin Abdallah. (22.08.2020)

Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Bw. Shaib Nnunduma (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu walipotembelea Ofisi yake. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Injinia Joseph Malongo, wa pili kulia ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah. Wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, Gerald Mweli na wa pili kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Alloyce Nzuki. Wengine pichani ni Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Kisiwani Mafia.

Mhifadhi Mshirikishi Jamii, Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU), Albert Makala (katikati) akieleza jambo mbele ya Makatibu Wakuu katika kikao kilichofanyika kwenye Ofisi za MPRU zilizopo Kisiwani Mafia. Kulia anayemuangalia ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Alloyce Nzuki. Wengine pichani ni Watumishi wa MPRU. (22.08.2020)

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa pili kutoka kulia waliosimama mbele) akiwa na Makatibu wa Wakuu wenzake, kutoka kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Injinia Joseph Malongo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, Bw. Gerald Mweli na wa pili kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Alloyce Nzuki wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) walipotembelea ofisi za MPRU. (22.08.2020).

Makatibu wa Wakuu kutoka Wizara nne tofauti wakimsikiliza Mwenyekiti wa Wavuvi wanaoishi katika Kisiwa cha Nyororo kilichopo katika Kisiwa cha Mafia, Bw. Likua Said Mchomoko (kulia aliyevaa Tshirt ya Njano) alipokuwa akitoa maelezo kuhusu shughuli za uvuvi wanazozifanya katika eneo hilo. Wa kwanza kutoka kulia waliosimama ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Injinia Joseph Malongo na wa pili kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, anayesimamia Elimu, Bw. Gerald Mweli. Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Alloyce Nzuki na wa pili kutoka kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah. (23.08.2020)





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni