"WATANZANIA TUNYWE MAZIWA YA HAPA NCHINI"-ULEGA
Watanzania wametakiwa kuwa wazalendo kwa kunywa maziwa yanayotengenezwa hapa nchini ili kuendeleza uchumi wa viwanda na Taifa kwa ujumla. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati akifungua maadhimisho ya 23 ya wiki ya maziwa Mkoani Dodoma kwa njia ya kielectronic "Ninaomba Sana na ninawasisitiza watanzania lazima tuwe na wivu wa maendeleo kwa ajili ya Taifa letu, lazima tuwe na uzalendo wa Taifa letu" Ulega Pia ameongezea na kusema kuwa Mhe. Raisi wetu Dr John Joseph Pombe Magufuli ametupa Ari kubwa Sana ya uzalendo kwa kupenda vya kwetu. Imeelezwa kuwa sekta ya Mifugo katika Pato la Taifa hapa nchini inachangia kwa asilimia saba (7%) huku asilimia thelathini (30%) ikitokana na sekta ndogo ya maziwa hivyo asilimia 1.2% ya Pato zima la Taifa inatokana na sekta ya maziwa. Mhe. Ulega amesema Katika mwaka 2017/2018 kulikua na jumla ya viwanda (76,) lakini hivi Sasa tunajumla ya viwanda (99) kwa hivyo tunazidi...