Nav bar

Ijumaa, 22 Mei 2020

PROF. GABRIEL ATOA TAHADHARI YA CORONA KWA WAFANYAKAZI






Mwenyekiti wa baraza la Wafanyakazi Sekta ya Mifugo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel, amewataka watumishi wa Sekta ya Mifugo kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya virusi vya corona kwa kufuata maagizo yanayotolewa na wataalamu wa afya huku wakiendelea kuchapa kazi kwa bidii.



Akizungumza na wajumbe wa baraza la wafanyakazi kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya jiji la Dodoma leo,  Prof. Gabriel amesema 'Janga hili ni la kimataifa na kwa vyovyote vile mmesikia katika nchi mbalimbali."



Amesema "Kwa niaba ya sekta ya mifugo wafugaji wote wa Ng'ombe zaidi ya milioni 32.5 na Mbuzi ambao wako zaidi ya milioni 20 na kondoo zaidi ya milion 5.5, kuku zaidi ya milion 79 kwa kweli tunamshukuru sana Dkt. John Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchukua uamuzi mzito wa kutoipeleka nchi kwenye kufungiwa watu kukaa nyumbani (Lockdown).



Vilevile, amesema watumishi wanatakiwa kufanya mambo matatu, ya tahadhari, maombi ba na kuchapa kazi kwa bidii.



"Baadhi ya watu pengine hawafahamu, lakini kwenye sekta ya mifugo kuna athari ambayo tungeipata, sidhani hata kama tungeweza kuziba pengo hilo," Amesema Prof. Gabriel



"Hata hivyo kwenye sekta ya mifugo nyama zinazoliwa ni zaidi ya kilo za nyama  2,628,000 maana yake ingefanyika Lockdown na hizo nyama zisingeliwa na maziwa yanayonyweka ni lita 8,352,000 kwa maana pia maziwa hayo yasingenyweka.



Ameongezea kuwa fursa kubwa kwa wafugaji kufuga kisasa na kuwa na mifugo yenye tija na mahitaji yanapotokea ndani ya nchi huko duniani kunawezekana  kutumia hiyo kama fursa ya kuweza kupata mahitaji ya chakula.



Amewaasa pia watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na watumishi wazembe, wavivu na wabadhilifu hawatakuwa na nafasi katika sekta ya mifugo, akawasihi watumishi kufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi na kuendelea na ushirikiano maana ni jambo la muhimu sana.



Ameongeza kuwa watumishi wa sekta ya mifugo wasikubali wafugaji waonewe na kupondwa haki yao na mtu yoyote na kwa namna yoyote.



Kwa upande wa ufugaji, wafugaji kote nchini we wametakiwa kufuata sheria, taratibu na kanuni bila kukosea chochote na bila kujidanganya kwamba kuna watu wa kuwatetea pale wanapokiuka sheria kwa makusudi.



Mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi sekta ya mifugo ambae pia ni Katibu Mkuu wizara ya Mifugo na Uvuvi(mifugo) Prof, Elisante Ole Gabriel, akiongea na wajumbe wa baraza hilo (hawapo pichani) Kuhusu mambo ya kiutendaji kazi katika kipindi hiki cha  maambukizi ya virusi vya  Corona, na kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Covid 19, katika kikao cha baraza la wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji l Dodoma leo tarehe 12/05/2020. 

Bwana Andrew Ponda, akitoa neno la shukrani mara baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu wa baraza la wafanyakazi sekta ya Mifugo na Msaidizi wake Bi Suzan Silayo, leo  tarehe 12/05/2020 katika kikao cha baraza la wafanyakazi kilichofanyika Kwenye ukumbi wa Halamashauri ya jiji la Dodoma. 


Katibu Mkuu wa wizara ya mifugo na uvuvi, sekta ya mifugo katikati akiwa ni Mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi Prof, Elisante Ole Gabriel kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza hilo , mara baada ya kumaliza kikao cha Baraza la wafanyakazi kilichifanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma leo tarehe 12/05/2020. 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni