Nav bar

Jumanne, 26 Mei 2020

MAAZIMIO YA MKUTANO WA MAWAZIRI WA KILIMO, USALAMA WA CHAKULA, KILIMO, MIFUGO NA UVUVI (SADC jijini Dsm, (22.05.2020)




* Mkutano umetoa miezi mitatu kwa kila mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kufanya tathmini ya madhara ya ugonjwa wa Covid - 19 katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.

* Mkutano umeweka mikakati ya usalama wa chakula na lishe katika ukanda wa SADC licha ya changamoto mbalimbali.

* Mkutano umeazimia mikakati ya kulinda magonjwa yanayovuka mipaka yanayohusu mimea na wanyama na kuathiri kilimo na mifugo.

* Mikakati imewekwa kutathmini namna wavuvi wanavyoathirika na ugonjwa wa Covid - 19.

* Mikakati imewekwa kwa shughuli za uvuvi katika ukuzaji viumbe kwenye maji hususan kwa nchi zizisizokuwa na maji ya asili (maziwa, bahari na mito).

* Mkutano umeweka mikakati ya nchi wanachama wa SADC kujilinda na ugonjwa wa covid - 19.



Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (Mb) ambaye pia Mwenyekiti wa Mawaziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula, Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) (kulia), akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel ambaye ni mwenyekiti wa maafisa waandamizi wa SADC katika sekta hizo, wakiimba wimbo wa taifa kabla ya kuanza kwa mkutano wa SADC kwa njia ya video 'video conference' jijini Dar es Salaam. (22.05.2020) 




Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (Mb) ambaye pia Mwenyekiti wa Mawaziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula, Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) akizungumza na mawaziri 11 kati ya 16 wakati wa mkutano wa SADC kwa njia ya video 'video conference' jijini Dar es Salaam. (22.05.2020) 



Baadhi ya maafisa waandamizi kutoka Tanzania, wakifuatilia mkutano wa mawaziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula, Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa njia ya video 'video conference' jijini Dar es Salaam. (22.05.2020) 



Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (Mb) ambaye pia Mwenyekiti wa Mawaziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula, Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) akionyesha ishara ya kuwaaga mawaziri 11 kati ya 16 wa SADC (hawapo pichani) walioshiriki  mkutano wa SADC kwa njia ya video 'video conference'. (22.05.2020) 




Picha ya pamoja ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (Mb) ambaye pia Mwenyekiti wa Mawaziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula, Kilimo, Mifugo na Uvuvi akiwa na baadhi ya maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Kilimo ambao wamehudhuria mkutano wa SADC kwa njia ya video 'video conference' jijini Dar es Salaam. (22.05.2020) 



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni