Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2019

HABARI PICHA NA MATUKIO

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akifanya tathmini ya ubora wa samaki aina ya jodari katika Soko la Samaki la Msasani jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani inayoaadhimisha Novemba 21 kila mwaka. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akikagua mwalo wa Soko la Samaki la Msasani jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili katika soko hilo kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani inayoadhimishwa Novemba 21 kila mwaka. Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji Dkt. Nazael Madala akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah wakati akizungumza na baadhi ya washiriki wakiwemo wavuvi kwenye maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani yaliyofanyika katika Soko la Samaki Msasani jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani yaliyofanyika katika S...

WAFUGAJI WAFURAHIA KUPATA MAENEO YA MALISHO

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega ametatua changamoto ya wafugaji na wananchi wa Kata ya Mabuki katika Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza kwa kusimamia upatikanaji wa shamba la hekta 450 kwa ajili ya kunenepeshea mifugo. Mhe. Ulega amesema shughuli za unenepeshaji wa ngombe unatakiwa kuanza mapema ili kuwasaidia wafugaji ambapo ametoa muda wa wiki moja kwa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) kampasi ya Mabuki, Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kituo cha Mabuki na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo wawe wameshaanza mchakato wa kuwapatia wafugaji maeneo hayo. Akizungumza na wafugaji na wananchi wa Kata ya Mabuki katika ziara ya siku moja wilayani Misungwi, Mhe. Ulega amesema wafugaji wengi nchini wanapata shida ya malisho kwa mifugo yao wakati wa kiangazi, hivyo ili kuongeza thamani na kufanya ufugaji kuwa na tija wizara imekuja na njia ya kisasa ya kunenepesha mifugo wakiwemo ngombe ambapo watakuwa wanauza kwa kumpima ng’omb...

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUSIMAMIA MASLAHI YA WAFUGAJI NA KUWATAKA KUFUATA SHERIA ZA NCHI.

Picha
Serikali imewataka wafugaji katika Wilaya za Chunya na Mbarali Mkoani Mbeya kufanya shughuli zao kwa kufuata sheria na taratibu za nchi ikiwemo ya kutoingiza mifugo katika maeneo ya Hifadhi za Taifa ya Ruaha na Pori la Akiba la Ruangwa, hali ambayo imekuwa ikisababisha migogoro kati ya wafugaji na askari wa Hifadhi za Taifa (TANAPA), wanaolinda hifadhi hizo ambapo baadhi ya migogoro hiyo imesababisha vifo vya wafugaji, askari na mifugo. Akizungumza Jumanne hii (19.11.2019) wakati wa kuhitimisha ziara ya siku mbili ya makatibu wakuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Sheria na Katiba, waliozuru baadhi ya maeneo yenye migogoro katika wilaya hizo, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka wafugaji kuacha tabia ya kuingiza mifugo katika maeneo ya hifadhi kwa ajili ya malisho kwa kuwa ni kinyume na taratibu za nchi. “Serikali inawataka wafugaji wote ku...

WAZIRI MPINA AZINDUA VITUO VYA UCHUNGUZI WA MAGONJWA YA MIFUGO SUMBAWANGA

Picha
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kwa pamoja vituo viwili vya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo (ZVC) na Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Kanda ya Magharibi- Sumbawanga na kutangaza msimamo wa Serikali ya awamu ya tano wa kupambana na magonjwa ya mifugo ili kuongeza uzalishaji wa mifugo na mazao yake nchini. Hivyo Serikali inawahakikishia wananchi uhakika wa upatikanaji wa chanjo kwa bei nafuu kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanyika ikiwa ni pamoja na Taasisi ya Chanjo (TVI) kuzalisha chanjo za kimkakati 11 ifikapo Juni mwakani na kwamba Serikali iko mbioni kutangaza bei elekezi ya Chanjo ili kuwadhibiti watu wachache waliokuwa wanawaibia wananchi. Aliongeza kuwa hivi sasa kuna ujenzi mkubwa wa Kiwanda kipya cha kuzalisha chanjo cha Hester Bioscience Africa Limited (HBAL) ambacho kitazalisha chanjo 27 ifikapo Juni na uwekezaji wake una thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 50 na kuwezesha upatikanaji wa chanjo zote kwa wafugaji wa ndani ya nchi,...

WAZIRI MPINA AZINDUA AGENDA ZA UTAFITI NA KUIBUA TAFITI ZILIZOFICHWA.

Picha
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua Agenda ya Kitaifa ya Utafiti wa Mifugo, Uvuvi na Ukuzaji wa Viumbe Maji ya mwaka 2020-2025 na kutangaza kuzifumua na kuziibua tafiti zote   zilizofanywa na wasomi na kutelekezwa kwenye makabati miaka ya nyuma na kuziingiza kwenye mfumo rasmi wa matumizi ili kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na maendeleo. Pia agenda hizo zitaleta msisimko mpya wa kufanya utafiti nchini na kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na maendeleo tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma ambapo tafiti nyingi zilifanywa na kutelekezwa kwenye makabati na watafiti mbalimbali wakiwemo Wanafunzi wa Shahada ya Uzamili (Masters Degree)   na Shahada ya Uzamivu (PHD) katika vyuo vikuu mbalimbali. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa agenda hizo kitaifa katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mazimbu mjini Morogoro, Waziri Mpina aliziagiza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo(TALIRI) na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi(TAFIRI) kubadilika ili kufany...