HABARI PICHA NA MATUKIO
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akifanya tathmini ya ubora wa samaki aina ya jodari katika Soko la Samaki la Msasani jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani inayoaadhimisha Novemba 21 kila mwaka. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akikagua mwalo wa Soko la Samaki la Msasani jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili katika soko hilo kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani inayoadhimishwa Novemba 21 kila mwaka. Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji Dkt. Nazael Madala akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah wakati akizungumza na baadhi ya washiriki wakiwemo wavuvi kwenye maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani yaliyofanyika katika Soko la Samaki Msasani jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mvuvi Duniani yaliyofanyika katika S...