Machapisho

MAAFISA UGANI WA SINGIDA NA DODOMA WAPATIWA MAFUNZO REJEA KUHUSU UFUGAJI WENYE TIJA.

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa mafunzo rejea kwa maafisa ugani kutoka mikoa ya Singida na Dodoma ili kuwawezesha wagani hao kwenda kutoa elimu kwa wafugaji.   Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani, Dkt. Angello Mwilawa amesema wizara imekua ikitekeleza mikakati muhimu katika sekta ya mifugo ili kuweza kumsaidia mfugaji kufuga kisasa na kibiashara.   Mikakati hiyo ni pamoja na Uboreshaji wa Koosafu za mifugo nchini, Udhibiti wa magonjwa, Upatikanaji wa uhakika wa malisho na maji katika maeneo yaliyo na mifugo, Kuboresha uzalishaji ulio wa kibiashara na ustawishaji wa ndege wafugwao, Kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa migogoro ya ardhi, Kuhamasisha na kuanzisha vyama vya ushirika vya wafugaji na Kudhibiti upotevu wa mapato yatokanayo na mifugo pamoja na mazao yake.   Dkt. Mwilawa amesema katika kutekeleza mikakati hiyo wizara imekua ikipata changamoto nyingi ambazo ni uk...

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

WAVUVI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA, TARATIBU ZA UVUVI

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama, Mahmoud Kimbokota amewataka Wavuvi mkoani Lindi kuzingatia sheria na taratibu zinasimamia uvunaji wa rasilimali za Bahari.   Kimbokota aliyasema hayo alipokutana na timu ya Wataalamu wa Mradi wa Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Bahari Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOfish) walipokwenda kufanya ufuatiliaji na kutathimini maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtama, mkoani Lindi Septemba, 28, 2020.   Akiongea na timu hiyo wakati akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi wa SWIOfish, Kimbokota alisema kuwa Wavuvi wanatakiwa kutambua kuwa uvuvi ni shughuli rasmi ya kujipatia kipato kama zilivyo shughuli nyingine, hivyo ni lazima waiheshimu na kuithamini.   “Wavuvi ni lazima wazingatie sheria na taratibu, na wabadilike,ule uvuvi wa kutumia Mabomu, Kokoro na matumizi ya nyavu haramu waache, kila mvuvi awe mlinzi na mwalimu wa mwenzake, uvuvi haramu tuukomeshe sisi wenyewe,” ...

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

WADAU WA TAFICO WATAKIWA KUTOKA NA MAPENDEKEZO YA AINA YA VIFAA VYA MELI YA UVUVI.

Picha
  Wadau wa TAFICO wametakiwa kujadili na kutoka na mapendekezo ya aina ya vifaa vya uvuvi hususani vitakavyotumika katika ujenzi wa meli ya uvuvi itakayomilikiwa na shirika hilo kwa niaba ya serikali.   Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Bw. Emmanuel Bulayi leo tarehe 01/10/2020 wakati akifungua kikao cha wadau hao kilichowahusisha washiriki kutoka kampuni za uvuvi, TDB, THA, DMI, FETA, TAFIRI, TASAC, Menejimenti ya TAFICO, Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu na wawakilishi wa Idara ya Uvuvi.   Bw. Bulayi amesema serikali ilishatiliana saini na serikali ya Japan mkataba wa kuanza utekelezaji wa Programu ya Uchumi na Maendeleo ya Jamii utakaosaidia ununuaji wa vifaa vya uvuvi ikiwa ni pamoja na meli moja ya uvuvi.   “Kwa kuwa taratibu za awali zilishakamilika ambapo tayari mkandarasi kwa ajili ya kununua vifaa hivyo ameshapatikana CROWN AGENT kutoka Japan, kinachosubiriwa ni sisi kutoka na mapendekezo ya aina ya vifaa vya uvu...

KONGAMANO LA NGOZI

Picha