DKT. BASHIRU AKAGUA NA KUZINDUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MARA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekagua na kuzindua miradi ya mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara na kueleza kuwa serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika kutenga fedha kwa wakati katika ujenzi na uboreshaji miundombinu ya barabara, umeme na maji ili miradi hiyo ikamalishwe kwa wakati.

Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo Agosti 11, 2026  wakati wa ziara yake maalum  ya siku nne inayolenga kutembelea, kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara.

Katika ziara hiyo Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezindua Daraja la Majengo mapya - Pambazuko lenye thaman ya zaidi ya shilingi milioni 287 ambalo litaunganisha Kata za Bweri na Rwamlimi ndani ya Manispaa ya Musoma.

Pia, alitembelea na kukagua ujenzi wa Soko la Nyayo, Kituo cha Mabasi na Barabara za mitaa ndani ya Manispaa ya Musoma, kuweka jiwe la Msingi la Madarasa matano, matundu ya vyoo na Ofisi katika shule ya Msingi Jitirola na kukagua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kiriba iliyojengwa kwa nguvu za wananchi na serikali ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Kwa Upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Mtambi amesema mradi wa ujenzi wa soko, Kituo cha Mabasi na Barabara za Mitaa ndani ya Manispaa ya Musoma utafungua fursa ya uwekezaji na uzalishaji kiuchumi ambapo jumla ya gharama za mradi huo ni shilingi biloni 19.6.

Ziara hiyo ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa mkoani Mara inatarajiwa kuendelea hapo kesho Agosti 12, 2026 katika Wilaya ya Butiama na Bunda.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (watatu kulia) akizindua Mradi wa ujenzi wa Daraja la Mawe la Pambazuko - Majengo Mapya katika Manispaa ya Musoma wakati wa Ziara yake Maalum inayolenga kukagua na kuzindua mirado inayotekeleza na Serikali Mkoani Mara, kuanzia leo Agosti 11 hadi 14, 2026, wa kwanza Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi.

Daraja la Pambazuko -Majengo Mapya litakalounganisha Kata ya Bwere na Rwamlimi  limezinduliwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa wakati wa Ziara yake Maalum mkoani Mara , leo Agosti 11, 2026.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (watatu kushoto) akipitishwa kwenye mchoro wa ujenzi wa Soko la Nyayo Mhandisi wa ujenzi wa mradi huo wakati wa ziara yake Mkoani Mara leo Agosti 11, 2026.

Muonekano wa Ujenzi wa Soko Nyayo ndani ya Manispaa ya Musoma Mkoani Mara ambalo Ujenzi wake utagharimu shilingi bilioni 4.95.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa alijikumbushia enzi zake akiwa Mwalimu, baada ya kuzindua Madarasa matano, matundu sita na Ofisi ya Shule ya Msingi Jitirola katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma wakati wa Ziara yake leo Agosti 11, 2026.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

WATAALAMU WATAKIWA KUKUSANYA TAKWIMU SAHIHI ZA KITAFITI

UTEKELEZAJI WA UFUGAJI SAMAKI KWA VIZIMBA WAANZA ZIWA TANGANYIKA

TANZANIA DAIRY BOARD