SERIKALI YAANZISHA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA UVUVI

Na. Stanley Brayton

◾Vizimba vya Bahari kuanza.

◾Wizara kuanzisha Mikakati ya Kimageuzi Sekta ya Uvuvi yatajwa.

◾ Vifaranga vya Samaki maji baridi na maji chumvi kupandikizwa.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza utekelezaji wa Mpango Mkakati wa kufuga samaki kwa njia ya Vizimba katika bahari, mpango ambao utasaidia kuongeza Uzalishaji wa Samaki chumvi na Masoko nje ya nchi.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh, katika ziara yake ya kikazi Mkoani Tanga alipotembelea Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui kwa ajili ya kukagua Maendeleo ya Mradi wa kuzalisha chakula cha Samaki aina ya Viroboto maji (Atemia), leo Februari 27, 2026, amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa sasa ipo katika utekelezaji wa kukuza Viumbemaji kwa njia ya Vizimba kupitia bahari, mpango ambao utaongeza tija katika Sekta ya Uvuvi.

"Mpango huu ni mpango mzuri ambao utekelezaji wake unategemea kuanza kufanyika ndani ya miezi mitatu katika maeneo mbalimbali yenye bahari nchi.” amesema Prof. Sheikh

Aidha, Prof. Sheikh amesema Wizara ipo kwenye hatua ya kuanzisha programu ya Kitaifa ya ufugaji Samaki kwa ajili ya kuzalisha Vifaranga Bora vya Samaki na Viumbe vingine vya maji ya baridi ikiwemo kaa na jongoo bahari ili kuongeza Uzalishaji katika Sekta.

Vilevile, ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) na Idara ya Ukuzaji Viumbemaji (DAQ) kushirikiana katika kupandikiza vifaranga vya kaa na jongoo bahari na kuzalisha kwa wingi Vifaranga vya Samaki maji baridi na maji chumvi ili wananchi waweze kufuga na wavuvi waweze kupata mbegu hizo kwa wingi na urahisi zaidi.

Pia, Prof. Sheikh ameiagiza Taasisi ya TAFIRI na Idara ya Uzalishaji Viumbemaji (DAQ) kuandaa Mkakati wa Mageuzi wa Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbemaji  kwa mwaka 2026/2050 (National Fish Breeding Programs na Fisheries Fisheries and Aquaculture Transformation Strategy 2026-2050), ambao utaleta mabadiliko katika Sekta ya Uvuvi na unaoendana na Dira ya Taifa ya mwaka 2050.

Prof. Sheikh amewataka wananchi kutumia fursa hii adhim ili kuweza kunufaika na Ufugaji Samaki wa Vizimba kupitia bahari.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh (wa pili kushoto), akikagua Miundombinu na Maendeleo ya Mradi wa kuzalisha Mayai na Viroboto Maji (Atemia) kwa ajili ya chakula cha kulishia Samaki, Mradi unaotekelezwa na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui, Februari 27, 2026 Tanga.

Afisa Uvuvi Mkuu Idara ya Uvuvi Kituo cha Ubora na Masoko Kanda ya Ziwa Victoria, Bw. Prosper Mremi (wa pili kulia), akimuelzea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh (wa kwanza kulia) jinsi uzalishaji wa Viumbemaji unavyofanyika na vifaranga kutunzwa, mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui, Februari 27, 2026 Tanga.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh (wa kwanza kulia), akizungumza na Maafisa wa Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui na Maafisa wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kuhusu kuzalisha kwa wingi vifaranga vya Samaki maji chumvi, mara baada ya kuwasili katika eneo la Kituo hicho, Februari 27, 2026 Tanga.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh (wa nne kulia), akizungumza na Maafisa wa Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui na Maafisa wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kuhusu kuzalisha kwa wingi chakula cha vifaranga vya Samaki aina ya Viroboto maji (Atemia), mara baada ya kuwasili katika eneo la Kituo hicho, Februari 27, 2026 Tanga.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh (katikati), akiwasikiliza wadau wa Sekta ya Uvuvi, mara baada ya kuwasili katika eneo la Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui, Februari 27, 2026 Tanga, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Ismael Kimirei na kulia ni Afisa Mfawidhi Kituo cha Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Tanga (FRP), Bw. Omary Ally Mohammed.

Picha ni wadau wa Sekta ya Uvuvi, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh (hayupo pichani), mara baada ya kuwasili katika eneo la Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji Machui, Februari 27, 2026 Tanga.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO