BI. MEENA AONGOZA KIKAO CHA MAGEUZI YA SEKTA YA MAZIWA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Utekelezaji wa Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi, leo Februari 27, 2026, jijini Dar es Salaam ameongoza kikao muhimu cha wajumbe wa kamati hiyo kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Kikao hicho kililenga kupitia kwa pamoja hatua za utekelezaji wa mradi tangu kuanza kwake hadi sasa, pamoja na kujadili mikakati madhubuti ya kuendeleza utekelezaji wake kwa ufanisi zaidi.
Bi Meena amesisitiza kwa wajumbe pamoja na sekretarieti ya kamati umuhimu wa kuwa na mgawanyo sahihi wa majukumu, ushirikiano wa karibu pamoja na mawasiliano yenye tija. Hatua hizi ni muhimu ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa wakati na kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti Mwenza wa kamati hiyo ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Bw. Selehe Juma, ameipongeza kamati hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania Bara na Visiwani katika kutekeleza mradi huo.



Maoni
Chapisha Maoni