Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2025

BI. MEENA AHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Na. Stanley Brayton   Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amewataka Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa na Ushirikiano katika utekelezaji majukumu Wizarani hapo. Bi. Meena amesema hayo Juni 28, 2025 wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Nyaraka za Ofisi baina yake na Mtangulizi wake Prof. Riziki Shemdoe katika hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya wizara hiyo yaliyopo Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. Aidha Bi. Meena amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini na kumteua katika nafasi hiyo ambapo ameahid kutekeleza maelekezo yote aliyopewa wakati akiapishwa. Kwa upande wake aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, amewashukuru Watumishi wote wa Wizara hiyo, kwa ushirikiano alioupata na kazi kubwa waliyoifanya katika kipindi chake.  Vilevile, Prof. Shemdoe amewasihi Watumishi wote kuishi kama familia, kuombeana mema na kuheshimiana ikiwa ni pamoja na ku...

TAKRIBAN WATANZANIA MILIONI 6 WANAJIHUSISHA NA SHUGHULI ZA UVUVI - RAIS DKT SAMIA

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kutokana na uwekezaji katika sekta ya Uvuvi mazao ya uvuvi yameongezeka kutoka tani 4077.18 zenye thamani ya shilingi bilioni 2.77  mwaka 2020/2021 hadi kufikia tani  543598.9  zenye thamani ya shilingi bilioni 3.04 mwaka 2025. Mhe. Dkt. Samia amesema hayo wakati akihutubia na kuhitimisha shughuli za Bunge la Jamhuri za Bunge Muungano wa Tanzania hafla iliyofanyika Bungeni Jijini Dodoma leo Juni 27, mwaka 2025. Aidha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan serikali amesema takriban watanzania milioni 6 wanajihusisha na shughuli za uvuvi . Pia, amesema kuwa kukamilika kwa bandari ya uvuvi ya Kilwa Masoko kunatarajiwa kuzalisha  ajira  takriban elfu 30,000 ambapo hadi sasa ujenzi wa bandari hiyo unaogharimu shilingi bilioni  279.5 umefikia asilimia 81.9.

MASOKO YA NYAMA NJE YA NCHI YAFUNGUKA MIAKA 4 YA RAIS SAMIA

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema jitihada za serikali ya awamu ya sita za kufungua masoko nje ya nchi zimeongeza mauzo ya nyama kwa upande wa sekta ya Mifugo kutoka Dola za marekani milioni 4.2 mwaka 2020/2021 hadi kufikia Dola za Marekani milioni 61. 4 Mwaka 2025. Mhe. Dkt. Samia amesema hayo wakati akihutubia na Kuhitimisha shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hafla inayofanyika Bungeni Jijini Dodoma leo Juni 27, mwaka 2025. Aidha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan serikali itabeba nusu ya gharama ya chanjo ya ng’ombe,Mbuzi na Kondoo huku gharama zote za chanjo ya Kuku zitabebwa na serikali. Pia Rais Mhe. Dkt. Samia ametoa rai kwa wabunge kuhimiza wananchi kuwa na matumizi bora ya ardhi baina ya wafugaji na wakulima kwa kufanya ufugaji wa kisasa.

SEKTA YA UVUVI YATAJWA KUWA NA MAENEO MAHSUSI YA KIMKAKATI, KUPITIA TEKNOLOJIA

Picha
Na. Edward Kondela Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman amesema Sekta ya Uvuvi inayo maeneo mahsusi ya kimkakati ili kukuza sekta hiyo kupitia teknolojia. Akizungumza jijini Dar es Salaam (25.06.2025) wakati akizindua ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi, ametaja maeneo hayo kuwa ni ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani. “Ripoti itasaidia mahitaji mahsusi ya kufahamu teknolojia ya namna gani inahitajika na kipindi gani ili wakulima wa mwani kuwa na uhakika wa mbegu zinazotumika, mahitaji ya soko na ufugaji wa mazao ya samaki kuwa na tija kwa wananchi.” amesema Mhe. Othman Amefafanua kuwa kwa muda mrefu dunia imekuwa ikikabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi hivyo umuhimu wa tekonolojia ni dhahiri katika kufanya tathmini halisi ili kwenda na wakati. Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede akimwakilisha Waziri ...

MILIONI 268 ZATUMIKA UKARABATI MNADA WA KINTINKU MANYONI

Picha
Na. Hamis Hussein Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha kwa asilimia 100 ujenzi wa uzio wenye mzunguko wa mita za mraba 500 katika Mnada wa Kinyinku wilayani Manyoni wenye thamani ya shilingi milioni 268, fedha zilizotengwa katika bajeti ya mwaka 2022/ 2023 ikiwa ni sehemu ya ukarabati wa miundombinu kwa ajili ya mazingira wezeshi ya biashara ya mifugo na mazao yake nchini. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti leo Juni 23, Mwaka 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Manyoni Mashariki Mhe. Dkt. Pius Chaya, lililohoji ni  lini  serikali itakamilisha ujenzi wa uzio wa mnada wa Kintinku uliopo Halmashauri  ya Wilaya ya Manyoni mkoani Singida. Aidha Mhe. Mnyeti ameongeza kuwa  serikali itaendelea kuboresha mindombinu muhimu kurahisisha biashara hiyo katika maeneo mbalimbali nchini.

WAZALISHAJI WA CHANJO ZA MIFUGO KUUNGANA AFRIKA

Picha
Na Daudi Nyingo ◼️ Waandaa Mwongozo wa Kudhibiti Chanjo Wasajili wa Chanjo na Wakurugenzi wanaosimamia uzalishaji wa chanjo za mifugo kutoka nchi 25 za ukanda wa Afrika wamekutana nchini Tanzania kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo. Mkutano huu umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam. Akifunga mkutano huo tarehe 17 Juni 2025, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, alisema kuwa mkutano huo umekuja kwa wakati muafaka kwani siku ya jana, tarehe 16 Juni 2025, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizindua rasmi kampeni ya chanjo za mifugo kitaifa, na ameidhinisha fedha kwa ajili ya kuchanja ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku, sambamba na kuwawekea utambuzi. “Kikao hiki kina lengo la kuandaa mwongozo ambao utatumika na wazalishaji wa chanjo katika nchi hizo 25, hasa katika kupambana na sotoka ya mbuzi na kondoo. Pia wanakus...

RAIS SAMIA ATOA RUZUKU YA BIL. 216 CHANJO ZA MIFUGO 2025/2029

Picha
Na. Omary Mtamike ◼️Chanjo ya kuku sasa kutolewa bure ◼️akabidhi pikipiki 700 kwa Maafisa ugani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa ruzuku ya Shilingi Bil. 216 kwenye kampeni ya kuchanja mifugo na utambuzi kwa kipindi cha miaka 5 kuanzia mwaka huu. Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya chanjo hizo na Utambuzi wa Mifugo iliyofanyika kwenye Viwanja vya Nyakabindi mkoani simiyu Mhe. Dkt. Samia amewataka Wakuu wa Mikoa yote nchini kusimamia matumizi ya  vifaa hivyo na kuhakikisha vinatumika kwa maslahi ya wafugaji kama ilivyokusudiwa. Aidha Mhe. Dkt. Samia amebainisha kuwa hivi sasa Serikali imeanza kuona matunda ya mabadiliko ya ufugaji wa kisasa yaliyofanyika ambapo ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuboresha sekta hiyo ili tija iendelee kuonekana. "Serikali imedhamiria kutokomeza magonjwa ya Mifugo na ndio maana leo tunazindua mpango huu wa chanjo 2025/2029 na hapa kwa dhati kabisa nataka niwapongeze kabisa wafugaji ...

BALOZI DKT. NCHIMBI AHIMIZA KAMPENI YA TUTUNZANE ITUMIKE NCHI NZIMA

Picha
 Na Chiku Makwai- WMUV SIMIYU Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewahimiza wafugaji na wakulima kote nchini kuitumia kampeni ya Tutunzane ambayo imelenga kuimarisha maelewano na ustawi kati ya wakulima na wafugaji na kuondokana na migogoro ya matumizi ya ardhi. Balozi Dkt. Nchimbi amesema hayo leo Juni 15, mwaka 2025 katika eneo la Nyakabindi Wilaya ya Bariadi Mkoa wa Simiyu wakati akifungua Kongamano la wafugaji kwa mwaka 2025 ambapo amehimiza kampeni hiyo itumike nchi nzima kuimarisha umoja wa jamii ya wafugaji na wakulima. " Kampeni hii ya tutunzane iliyoanzishwa na Mkuu wa  Wilaya ya Mvomero imeonyesha thamani ya wafugaji na wakulima kwa kuimarisha maelewano baina yao kwani sisi sote ni taifa moja, hivyo kampeni hii ya tutunzane itumike nchi nzima ili wafugaji wote wanufaike" alisema Balozi Dkt. Nchimbi. Aidha Balozi Dkt. Nchimbi ameogeza kwa kusema kuwa Chama cha Mapinduzi kinadhamira ya kuinua ufugaji kwakutambua sekta ya mifungo ni sekta ...

DKT. ASHATU- WAFUGAJI KUUPOKEA UFUGAJI WA KISASA

Picha
 Na Chiku Makwai - WMUV SIMIYU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa wafugaji wameonyesha nia kuupokea ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija kwenye sekta ya mifugo nchini. Mhe. Dkt. Kijaji amesema hayo leo (Juni 15, 2025) wakati wa  Kongamano la Wafugaji Tanzania lililofanyika katika Viwanja vya Nanenane Nyakabindi vilivyopo Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu. “Tupo tayari kubadilika na kuanza kufuga kisasa kwa kutumia njia za kisasa ili kufikia mageuzi makubwa ya serikali kwenye Sekta ya Mifugo nchini” amesema Mhe. Dkt. Kijaji Aidha, amesema wizara imefanya mikutano na wafugaji wote nchini kwa kukutana na wawakilishi wao ili kujadili changamoto za sekta hiyo na kuzigeuza kuwa fursa ili kuiboresha Sekta ya Mifugo. Pia, amesema kwa kutambua mchango mkubwa unaotokaana na sekta hiyo serikali itaendelea kushirikiana na wadau wake wote waliopo katika mnyororo mzima wa Sekta ya Mifugo ili kuipa thamani sekta hiyo.  Ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa wa Simiyu kuj...

WAFUGAJI WAASWA KUFUGA KISASA ILI KUONGEZA TIJA

Picha
 Na. Stanley Brayton, WMUV  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amewataka wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kufuga kisasa ili kuongeza tija katika Mifugo. Akizungumza katika Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo yalioshirikisha nchi tatu ikiwemo Tanzania, Kenya na Namibia, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani, Mhe. Mnyeti, amesema Serikali awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa inaendelea na mchakato wa kuhamasisha wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kuingia kwenye Ufugaji wa kisasa wenye tija. “ni matumaini yangu kuwa wafugaji mtachangamkia fursa hii kwa kutafuta na kununua mbegu bora za mifugo zitakazowaletea tija zaidi kwenye ufugaji wenu kuliko kuendelea na Ufugaji wa kizamani usio na tija.” ameseama Mhe. Mnyeti  Aidha, Mhe. Mnyeti amesema maonesho haya ya mifugo yana lengo la kuhamasisha matum...

DKT. KIJAJI AKAGUA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA KAMPENI YA CHANJO ZA MIFUGO NA UTAMBUZI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametembelea na kufanya ukaguzi wa maandalizi ya Uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya mifugo na utambuzi leo, Juni 13, mwaka 2025 katika Viwanja vya nane nane eneo la Nyakabindi wilayani Bariadi Mkoa wa  Simiyu. Mhe. Dkt. Ashatu ameambatana na  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Riziki Shemdoe, Naibu Katibu Mkuu (Mifugo) Bw. Abdul Mhinte na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa wizara hiyo  Dkt. Benezeth Lutege. Katika Ukaguzi huo Waziri Dkt. Kijaji amekagua eneo la uzinduzi wa kampeni ya chanjo, sehemu ya itakayotumika kuwakabidhi vitendea kazi wataalam watakaotekeleza zoezi la Chanjo Kitaifa. Pia ametembelea eneo ambalo litafanyika Kongamano la Wafugaji siku ya Jumapili ya Juni 15, 2025 kabla ya Uzinduzi wa Kampeni ya Chanjo na Utambuzi Kitaifa Juni 16, mwaka 2025 mkoani Simiyu.

MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO KIDIJITALI WA UTAMBUZI WA MIFUGO YATOLEWA

Picha
Na Chiku Makwai-WMUV SIMIYU Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Abdul Mhinte amefungua mafunzo ya matumizi ya mfumo kidijitali  wa utambuzi wa mifugo kwa Waratibu wa Chanjo na Maafisa Tehama kanda ya ziwa. Akizungumza na wataalam hao leo Juni 12, 2025 Mkoani Simiyu Bw. Mhinte amesema kuwa lengo la kuwapatia mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa kuhusu matumizi ya mfumo huo wa kidijitali. Aidha Mhinte amewasisitiza kuwa ni wajibu wa kila mtaalam kutunza vifaa hivyo ili viweze kuwasaidia katika shuguli hiyo mpaka itakapo kamilika.