Nav bar

Jumanne, 1 Oktoba 2024

DKT. MHINA AIPA HEKO MRADI WA AgResults KWA UTEKELEZAJI MZURI

Na. Stanley Brayton

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina amepongeza utekelezaji wa Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa (AgResults Tanzania Dairy Productivity Challenge) kwa utekelezaji mzuri wa kukuza Sekta ya Mifugo, ususani katika kuboresha mahusiano mazuri kati ya wafugaji na maafisa wa malisho pamoja na maafisa Mifugo, na kutoa pembejeo kwa wafugaji na utoaji wa huduma za Ugani ili kukuza Sekta hii ya Mifugo. 

Akizungumza, katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa,  kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, mkoani Dodoma, Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Mhina amesema anawapongeza maafisa wa Mradi wa AgResults kwani wametumia namna mbalimbali ili kuweza kuwafikia wafugaji wadogo na kuweza kuwapatia huduma mbalimbali za ugani, ikiwa ni pamoja na kutoa pembejeo za Mifugo.

“mradi huu umefika mpaka kwa wafugaji mbaimbali maeneo ya vijijini kiasi kwamba umetoa huduma kwa wafugaji na mifugo yako kwa kuboresha malisho pamoja utoaji chanjo”, amesema Dkt. Mhina

Aidha, Dkt. Mhina amesema ni wajibu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha huduma zinawafikia wafugaji hadi vijijini, ikiwa ni pamoja na utoaji chanjo za mifugo na tiba kwa mifugo pamoja na pembejeo ili kuweza kuwapa huduma mbalimbali zitakazosaidia kuboresha mifugo na maisha ya wafugaji.

Vilevile, Dkt. Mhina amesema Wizara iangalie ni namna gani inaweza kuwafikia wafugaji Tanzania nzima ili kuhamasisha na kutoa mbegu Bora za madume ya ng'ombe kwa wafugaji na kuhakikisha matibabu ya mifugo yanapatikana kwa wakati.

Dkt. Mhina ametoa rai kwa maafisa wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuendelea kushirikiana na Sekta binafsi katika kuboresha huduma za mifugo, na kuhakikisha maziwa salama yanapatikana kwani asilimia kubwa ya watanzania hawanywi maziwa salama, na hii inatokana na maziwa mengi kuuzwa kienyeji, na mashirikiano hayo yatasaidia katika kuboresha usindikaji na utunzaji maziwa kwa njia ya usalama zaidi kiasi cha kutanua masoko nchini hadi nchi za nje.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina na ndiye Mgeni Rasmi, akitoa Hotuba fupi, katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa, uliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, Dodoma


Msimamizi wa Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa (AgResults Tanzania Dairy Productivity Challenge Project), Bi. Neema Mrema, akitoa Ripoti ya Utekelezaji wa Mradi wa AgResults, ni katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa, uliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, Dodoma


Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Stephen Michael, akitoa neno la Ukaribisho kwa washiriki, ni katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa, uliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, Dodoma






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni