Nav bar

Jumatano, 9 Oktoba 2024

DKT. MPANGO AZIPONGEZA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA SHUGHULI ZAKE

Na. Stanley Brayton

Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, amezipongeza Sekta za Mifugo na Uvuvi kwa utekelezaji mzuri wa shughuli zake ambazo zimelenga kukuza shughuli za ufugaji na uvuvi kwa kuendana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kuhudumia wananchi na kuwapa maisha Bora.

Akizungumza, Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango leo Oktoba 8, 2024 katika Ziara yake wilayani Igunga, Mkoani Tabora, Dkt. Mpango amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi inafanya vizuri katika kuhakikisha mifugo bora inapatikana kwa wananchi kwa kutoa pembejeo bora kwa wafugaji na wavuvi, vilevile kutoa mikopo kwa wafugaji na wavuvi pamoja na kuwapatia mbegu bora za vifaranga vya samaki pamoja na madume Bora ya ng'ombe.

Kwa Upande wake, Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo imefanya mambo mengi sana kwa watanzania na ata katika Wilaya ya Igunga ikiwa ni kutoa elimu kwa wafugaji na wavuvi.

“tuna fursa ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba, na ya utengenezaji wa mabwawa ya kufugia samaki pamoja na kutoa madume Bora ya ng'ombe kama mbegu”, amesema Mhe. Mnyeti

Aidha, Mhe. Mnyeti amesema, Madume Bora ya ng'ombe yalishagawiwa katika baadhi ya wilaya, ikiwemo Wilaya ya Bahi, Serengeti na Bunda.

Vilevile, Mhe. Mnyeti amesema mpango huo ni endelevu hapa nchini, na Wizara inampango wa kusambaza madume hayo Bora ya ng'ombe katika wilaya zote nchini Tanzania ila yaweze kupanda ng'ombe wa kienyeji na kupata ng'ombe wengine walio Bora.


Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, akimuuliza swali Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (hayupo pichani), ni lini Wizara italeta Madume Bora ya ng'ombe Wilayani Igunga, ni katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Igunga - Tabora


Naibu Waziri Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti, akijibu swali la Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpangoni (hayupo pichani), kuwa Wizara italeta Madume Bora ya ng'ombe 20 Wilayani Igunga baada ya wiki tatu, ni katika Ziara ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Igunga - Tabora


Picha ni wananchi wakimsikiliza Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora ya Oktoba 8, 2024, Igunga - Tabora


Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bukene kuhusu umuhimu wa kuzingatia lishe Bora kwa watoto na mama wajawazito ili waweze pata Protini ya kutosha itakayowasaidia kukuza ufikiri wa mtoto na kusisitiza Maafisa kutoa elimu kuhusu lishe Bora ili jamii zielewe nini maana ya lishe bora na umuhimu wake, ni katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora


Naibu Waziri Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti, akisalimia wanakijiji wa Bukene na kutoa Salamu za Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ni katika Ziara ya kikazi Mkoani Tabora ya Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora



 Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango (aliyeshika bomba la maji), akifungua maji kama Ishara ya Uzinduzi  na Upanuzi wa Mradi wa Maji kutoka ziwa Viktoria kwenda Bukene, ni katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora, Wa tatu kulia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti


Picha ni Washiriki mbalimbali wakiwemo wakazi wa Bukene na Maafisa mbalimbali na Viongozi wa Serikali wakiwa katika Ziara ya kikazi Mkoani Tabora ya Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora





Jumanne, 1 Oktoba 2024

DKT. MHINA AIPA HEKO MRADI WA AgResults KWA UTEKELEZAJI MZURI

Na. Stanley Brayton

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina amepongeza utekelezaji wa Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa (AgResults Tanzania Dairy Productivity Challenge) kwa utekelezaji mzuri wa kukuza Sekta ya Mifugo, ususani katika kuboresha mahusiano mazuri kati ya wafugaji na maafisa wa malisho pamoja na maafisa Mifugo, na kutoa pembejeo kwa wafugaji na utoaji wa huduma za Ugani ili kukuza Sekta hii ya Mifugo. 

Akizungumza, katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa,  kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, mkoani Dodoma, Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Mhina amesema anawapongeza maafisa wa Mradi wa AgResults kwani wametumia namna mbalimbali ili kuweza kuwafikia wafugaji wadogo na kuweza kuwapatia huduma mbalimbali za ugani, ikiwa ni pamoja na kutoa pembejeo za Mifugo.

“mradi huu umefika mpaka kwa wafugaji mbaimbali maeneo ya vijijini kiasi kwamba umetoa huduma kwa wafugaji na mifugo yako kwa kuboresha malisho pamoja utoaji chanjo”, amesema Dkt. Mhina

Aidha, Dkt. Mhina amesema ni wajibu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha huduma zinawafikia wafugaji hadi vijijini, ikiwa ni pamoja na utoaji chanjo za mifugo na tiba kwa mifugo pamoja na pembejeo ili kuweza kuwapa huduma mbalimbali zitakazosaidia kuboresha mifugo na maisha ya wafugaji.

Vilevile, Dkt. Mhina amesema Wizara iangalie ni namna gani inaweza kuwafikia wafugaji Tanzania nzima ili kuhamasisha na kutoa mbegu Bora za madume ya ng'ombe kwa wafugaji na kuhakikisha matibabu ya mifugo yanapatikana kwa wakati.

Dkt. Mhina ametoa rai kwa maafisa wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuendelea kushirikiana na Sekta binafsi katika kuboresha huduma za mifugo, na kuhakikisha maziwa salama yanapatikana kwani asilimia kubwa ya watanzania hawanywi maziwa salama, na hii inatokana na maziwa mengi kuuzwa kienyeji, na mashirikiano hayo yatasaidia katika kuboresha usindikaji na utunzaji maziwa kwa njia ya usalama zaidi kiasi cha kutanua masoko nchini hadi nchi za nje.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina na ndiye Mgeni Rasmi, akitoa Hotuba fupi, katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa, uliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, Dodoma


Msimamizi wa Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa (AgResults Tanzania Dairy Productivity Challenge Project), Bi. Neema Mrema, akitoa Ripoti ya Utekelezaji wa Mradi wa AgResults, ni katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa, uliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, Dodoma


Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Stephen Michael, akitoa neno la Ukaribisho kwa washiriki, ni katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa, uliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, Dodoma