Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2024

PROF. SHEMDOE AONGOZA TIMU YA WATALAAM KUTOKA TANZANIA MKUTANO WA IOTC BANGKOK, THAILAND

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa 13 wa Kamati ya Wataalam ya Vigezo vya Mgawanyo wa Mavuno ya Samaki aina ya Jodari na Jamii zake (13th Technical Committee on Allocation Criteria - TCAC13) ya Kamisheni ya Jodari ya Bahari ya Hindi (Indian Ocean Tuna Commission (IOTC) unaofanyika Bangkok, Thailand kuanzia tarehe 21 hadi 24 Oktoba 2024.  Prof. Shemdoe ameongoza Timu hiyo ya wataalam akiwa ameongozana na Maafisa wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) akiwemo Dkt. Emmanuel Sweke, Mkurugenzi Mkuu wa DSFA. Katika kuhakikisha mgawanyo huo wa samaki unakuwa sawa kwa nchi wanachama, kamati hiyo ya IOTC iliundwa  katika kikao chake cha 14 kilichofanyika Busan, Korea tarehe 1 hadi 5 Machi, 2010 kwa lengo la "kujadili vigezo vya ugawaji kwa ajili ya usimamizi wa rasilimali za Jodari katika Bahari ya Hindi na kupendekeza mfumo mzuri wa mgao.  Aidha,  kwa takribani miaka 13 sasa Kamati hiyo imeende...

TANZANIA KUWA MWENYEJI MKUTANO WA JUKWAA LA TASNIA YA KUKU NA NDEGE WAFUGWAO KWA NCHI ZA SADC

Picha
Na. Stanley Brayton Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Jukwaa la Tasnia ya kuku na ndege wafugwao kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika unaotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 16 hadi 17 Octoba, 2024 Serena Hotel jijini Dar Es Salaam. Akizungumza leo tarehe 11 Oktoba, 2024  jijini Dodoma, wakati wa mkutano na waandishi wa habari kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdala Ulega, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Riziki Shemdoe, amesema lengo la mkutano huo ni kukuza fursa za ajira nje na ndani ya nchi pamoja na kujadili na kubadilishana uzoefu wa sekta hiyo  na nchi za SADC. “mkutano huo utatoa nafasi kwa Tanzania kuonyesha fursa za uwekezaji zilizopo katika Tasnia ya kuku na ndege wafugwao kuongeza wigo wa masoko ya bidhaa hizo katika nchi za SADC na kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi za SADC katika Tasnia hiyo” amesema Prof. Shemdoe. Prof. Shemdoe ameshukuru uongozi wa awamu ya sita...

TANZANIA NA IRAN ZA SAINI HATI SABA ZA MAKUBALIANO ILI KUKUZA DIPLOMASIA YA UCHUMI

Picha
Na. Stanley Brayton Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kiislam ya Iran zimesaini hati saba  za makubaliano ili kukuza diplomasia ya uchumi baina ya mataifa hayo mawili. Hafla ya kusaini hati hizo za makubaliano imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, tarehe 19 Oktoba, 2024, katika mkutano wa tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano baina ya Tanzania na Iran. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Waziri wa Kilimo wa   Jamhuri ya Kiislaam ya  Iran, Mhe. Golamreza Nouri Ghezelcheh walishuhudia zoezi hilo la uwekaji saini hati hizo lililohusisha Wizara za Kisekta, baadhi ya Taasisi za Umma na Taasisi binafsi.  Akizungumza wakati akifungua mkutano huo uliohusisha Viongozi wa ngazi za juu za Serikali za nchi hizo, wakiwemo Mawaziri, Mhe. Balozi Kombo amemshukuru Mhe. Golamreza Nouri kwa jitihada zake za kuimarisha ushirikiano wa uwili n...

NWM-DKT. BITEKO: ASILIMIA 55 YA KAYA NCHINI ZINAFANYA SHUGHULI ZA UFUGAJI KUKU

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Dotto Biteko amesema asilimia 55 ya kaya nchini zinafanya shughuli za ufugaji kuku uliopelekea ongezeko la uchumi jumuishi unaolenga kujenga kesho iliyo bora. Amyasema hayo leo tarehe 16 Oktoba, 2024 katika ukumbi wa Serena Hotel Dar Es Salaam wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Jukwaa la Tasnia ya Kuku na Ndege wafugwao kwa Nchi za Kusini mwa Afrika. “Tasnia hii imeajiri zaidi wanawake na vijana, vilevile inazalisha malighafi za viwanda, inachangia usalama wa chakula na lishe na upatikanaji wa fedha za kigeni”  Aidha Dkt. Bitteko amesema lengo la mkutano huo ni kujadili na kubadilishana uzoefu kutoka nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), pamoja na kubainisha fursa za kimkakati zinazohusu tasnia ya kuku na ndege wafugwao. Naye, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Abdallah Ulega amesema kuwa kuku ni mifugo rafiki na mifugo hiyo haihitaji eneo kubwa katika kuitunza, inazal...

DKT. MPANGO AZIPONGEZA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA SHUGHULI ZAKE

Picha
Na. Stanley Brayton Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, amezipongeza Sekta za Mifugo na Uvuvi kwa utekelezaji mzuri wa shughuli zake ambazo zimelenga kukuza shughuli za ufugaji na uvuvi kwa kuendana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kuhudumia wananchi na kuwapa maisha Bora. Akizungumza, Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango leo Oktoba 8, 2024 katika Ziara yake wilayani Igunga, Mkoani Tabora, Dkt. Mpango amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi inafanya vizuri katika kuhakikisha mifugo bora inapatikana kwa wananchi kwa kutoa pembejeo bora kwa wafugaji na wavuvi, vilevile kutoa mikopo kwa wafugaji na wavuvi pamoja na kuwapatia mbegu bora za vifaranga vya samaki pamoja na madume Bora ya ng'ombe. Kwa Upande wake, Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo imefanya mambo mengi sana kwa watanzania na ata katika Wilaya ya ...

DKT. MHINA AIPA HEKO MRADI WA AgResults KWA UTEKELEZAJI MZURI

Picha
Na. Stanley Brayton Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina amepongeza utekelezaji wa Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa (AgResults Tanzania Dairy Productivity Challenge) kwa utekelezaji mzuri wa kukuza Sekta ya Mifugo, ususani katika kuboresha mahusiano mazuri kati ya wafugaji na maafisa wa malisho pamoja na maafisa Mifugo, na kutoa pembejeo kwa wafugaji na utoaji wa huduma za Ugani ili kukuza Sekta hii ya Mifugo.  Akizungumza, katika Kikao cha kufunga Mradi wa Utatuzi wa Changamoto za Uzalishaji wa Maziwa,  kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi - Mtumba, Octoba 01, 2024, mkoani Dodoma, Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Mhina amesema anawapongeza maafisa wa Mradi wa AgResults kwani wametumia namna mbalimbali ili kuweza kuwafikia wafugaji wadogo na kuweza kuwapatia huduma mbalimbali za ugani, ikiwa ni pamoja na kutoa pembejeo za Mifugo. “mradi huu umefika mpaka kwa wafugaji mbaim...