PROF. SHEMDOE AONGOZA TIMU YA WATALAAM KUTOKA TANZANIA MKUTANO WA IOTC BANGKOK, THAILAND
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa 13 wa Kamati ya Wataalam ya Vigezo vya Mgawanyo wa Mavuno ya Samaki aina ya Jodari na Jamii zake (13th Technical Committee on Allocation Criteria - TCAC13) ya Kamisheni ya Jodari ya Bahari ya Hindi (Indian Ocean Tuna Commission (IOTC) unaofanyika Bangkok, Thailand kuanzia tarehe 21 hadi 24 Oktoba 2024. Prof. Shemdoe ameongoza Timu hiyo ya wataalam akiwa ameongozana na Maafisa wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) akiwemo Dkt. Emmanuel Sweke, Mkurugenzi Mkuu wa DSFA. Katika kuhakikisha mgawanyo huo wa samaki unakuwa sawa kwa nchi wanachama, kamati hiyo ya IOTC iliundwa katika kikao chake cha 14 kilichofanyika Busan, Korea tarehe 1 hadi 5 Machi, 2010 kwa lengo la "kujadili vigezo vya ugawaji kwa ajili ya usimamizi wa rasilimali za Jodari katika Bahari ya Hindi na kupendekeza mfumo mzuri wa mgao. Aidha, kwa takribani miaka 13 sasa Kamati hiyo imeende...